<?xml version='1.0' encoding='UTF-8'?><?xml-stylesheet href="http://www.blogger.com/styles/atom.css" type="text/css"?><feed xmlns='http://www.w3.org/2005/Atom' xmlns:openSearch='http://a9.com/-/spec/opensearchrss/1.0/' xmlns:georss='http://www.georss.org/georss' xmlns:gd='http://schemas.google.com/g/2005' xmlns:thr='http://purl.org/syndication/thread/1.0'><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684</id><updated>2011-10-23T01:49:21.478-07:00</updated><category term='MY STILL LIFE....'/><title type='text'>omarilyas</title><subtitle type='html'>Proud, conscious and committed Panafricanist always busy scheming for Africanjema – Democratic, Peaceful, United and Prosperous Africa for Africans by Africans…</subtitle><link rel='http://schemas.google.com/g/2005#feed' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/posts/default'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default?max-results=100'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/'/><link rel='hub' href='http://pubsubhubbub.appspot.com/'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><generator version='7.00' uri='http://www.blogger.com'>Blogger</generator><openSearch:totalResults>30</openSearch:totalResults><openSearch:startIndex>1</openSearch:startIndex><openSearch:itemsPerPage>100</openSearch:itemsPerPage><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-6839815976597326733</id><published>2011-10-23T01:41:00.000-07:00</published><updated>2011-10-23T01:49:21.551-07:00</updated><title type='text'>Let's Celebrate the Fall of Elder Comrade....</title><content type='html'>@Ilyas,O.S&lt;br /&gt;20th October 2011&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Salute to the Fallen Elder Comrade Moummar Qaddafi. Your erratic, autocratic and sometimes mediocrity behaviors will be a lesson to all and your unquestionable commitment for the grand Panafrican nationalism will always be cherished and inspire the youthful continent.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;You have gone the way you wanted and on the 1st ever Global Dignity day and also Africa's heroes day. Regards to Comrades Felix Moumie, Patrice Lumumba, Thomas Sankara and Samora Machel whom you shared the same spirit and so your fates.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Your fall should not mourned but celebrated by the conscious Afrika. It has awaken many of us, especially the youth of Afrika.It has reminded us on our of perpetual vigilance to protect our hard worn independence and our aspirations as dignified beings. It has united Afrikan hearts and minds. Both the born again democrats and un-repented centralists (they call them dictators).Those against and for status quo! &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;A lot have been and will be said about the autocratic era of Qaddafi but one thing I know from our history is if those internal and external opponents of Mwalimu Nyerere's ideology, policies and leadership succeeded in toppling him then, most of us we would be singing same tunes like those celebrating Qaddafi demise.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Its only that he saw it coming and stepped aside for us to establish and inspire mfumofisadi (corrupt system) we now suffering from that we recognized his noble contribution to our lives and the continent at the expense of our mediocre freedom we now abuse instead of using for our development.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Only when we became captives of domestic and foreign manyang'au whom Qaddafi called the "vultures" of the small people dignity we came to appreciate the blessing of having Mwalimu as our founding Elder Leader!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;As Comrade Samora Machel whom we are commemorating 25 anniversary of his death used to say...Aluta Continua&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-6839815976597326733?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/6839815976597326733/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=6839815976597326733' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/6839815976597326733'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/6839815976597326733'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2011/10/lets-celebrate-fall-of-elder-comrade.html' title='Let&apos;s Celebrate the Fall of Elder Comrade....'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-1329599135058845224</id><published>2011-09-28T01:38:00.000-07:00</published><updated>2011-09-28T02:56:02.675-07:00</updated><title type='text'>TULIKOTOKA: MWANZO WA SAFARI YA MWISHO YA CCM</title><content type='html'>Katika kuendeleza maoni yangu kuhusu umuhimu wa CHADEMA kushinda kwa kushindwa sasa ni vizuri kurudia makala hii hapa chini ambayo niliandika miaka sita iliyopita mara baada ya mchakato wa kupata mgombea nafasi ya Urais wa Jamhuri na Muungano kupitia tiketi ya CCM......&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;TULIKOTOKA: MWANZO WA SAFARI YA MWISHO YA CCM&lt;br /&gt;Na Ilyas, O.S&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;20/05/2005&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni ukweli usiopingika kuwa matokeo ya uchaguzi wa mgombea wa nafasi ya urais katika Chama Cha Mapinduzi yameweza kuliepusha kundi hili kisiasa katika hatari ya kugawanyika kwa kasi kama ilivyokuwa ikionekana awali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naongelea dhana ya kugawanyika kwa kasi tu, kwa kuwa nina uhakika kuwa mwenendo mzima wa siasa za uchaguzi huo na mambo kadhaa yaliyojitokeza katika siku za mwisho za shughuli hizo ndani ya chama hicho, zimeleta mgawanyiko mkubwa na wa hatari zaidi utakaodumu daima.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata kama kwa njia za ajabu mno ndugu hawa wameweza kumchagua mtu ambaye kwa maoni yao wana uhakika wa kuendelea kutawala watazania kwa miongo kadhaa ijayo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kuwa CCM ya sasa si ile tena iliyokuwa ikiwavutia watu kwa utulivu wake, uongozi wa kufuata maadili ya utanzania, falsafa zake zenye kujali utu, kupinga ubaguzi na mengineyo mengi mazuri yaliyokuwa yakitofautisha chama hiki na makundi mengine ya kisiasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chama cha mapinduzi kama ilivyo kwa vyama vingine vikubwa tawala barani afrika, kimepitia mabadiliko mbalimbali hadi kufikia sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mabadiliko hayo yameanzia kutoka kuwa chama cha ukombozi, kikaja kuwa chama cha kujenga utaifa na baadaye kuwa chama cha kuimarisha uchumi na kuboresha maisha ya watanzania kabla ya sasa kugeuka kuwa chama cha kuhakikisha kuendelea kubaki madarakani kwa tabaka tawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbadiliko huu umekuja kutokana na nguvu mbalimbali za kimfumo na mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi duniani ambayo yamepelekea washika dau wa chama hiki ambao mwanzo walijitahidi kukabiliana vilivyo, kuamua kufuata mkondo wa mabadiliko ili kuweza kuendelea kuongoza taifa hili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mfano mkubwa wa mabadiliko haya nje ya mipaka yetu ni chama cha Labour cha Uingereza kinachoongozwa na mwanasiasa “kijana” machachari Tony Blair. Chama ambacho wiki iliyopita kilipata pigo kubwa la kisiasa kwa kupoteza viti vingi katika baraza la wanaojiita wawakilishi wa makabwela.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama ilivyokuwa CCM, chama hiki kilianzishwa kama kundi la kutetea wafanyakazi na makabwela wa Taifa hilo la kibwanyenye. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama ilivyo kwa vyama vingi vya aina hii duniani, chama cha Labour kama kilivyokuwa CCM hapo awali, kilikuwa ni chama kinachoendeshwa na misingi na falsafa madhubuti za kutetea wanyonge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Falsafa na misingi ambayo walijiwekea ili kila anayetaka kuchaguliwa kukiongoza chama hicho na hivyo kugombea nafasi ya kuongoza serikali ya Uingereza alipaswa kuonyesha wazi kuwa ni mfuasi makini na mwaminifu wa misingi hiyo kwa kauli thabiti na vitendo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi duniani yalikipelekea chama hicho kukosa mvuto wa kuaminiwa na wapiga kura wengi na hivyo kuwekwa kando katika kuingoza Uingereza kwa miaka kadhaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali hiyo iliwapelekea kundi dogo la wanasiasa vijana machachari wa chama hicho akiwemo bwana Mandelson ambaye aliwahi kuishi Musoma, Tanzania kwa miaka kadhaa akitafiti siasa ya ujama na kujitegemea na utaalamu wa kiuongozi wa baba wa Taifa, kuja na mbinu mpya walioita LABOUR MPYA.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tofauti na Labour ya kihistoria, New Labour kama ilivyo CCM hivi sasa, ililenga matumizi ya siasa za kubabaisha zilizo tofauti na misingi na falsafa asilia ya chama hicho ili kuweza kuwalaghai wapiga kura waliokitupa, kukichagua na kukirudisha madarakani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwao wao ni kuwa mara baada ya kurudi madarakani wangeweza kuzirejesha siasa makini za kihistoria za chama hicho na hivyo kuendeleza misingi na falsafa zake asilia kwa mtindo unaoendana na wakati uliopo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama hapo baadae ilivyokuwa kwa upande wa wahafidhina wa chama cha Republican cha Marekani walipomchagua George W Bush kuwauzia fikira zao za kulinda nafasi ya ubabe wa marekani duniani, Mandelson na wenzake waliamua kumchagua mwanasiasa machachari aliyekuwa akikubalika wakati huo yaani Tony Blair kuongoza mpango huo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo yake ni hali inayonekana hivi sasa huko Uingereza. Sio tu chama hicho kimegeuka kuwa cha kinyang’au zaidi kuliko chama cha mahafidhina wa kijadi cha Conservative, hivi sasa kinaelekea kaburini kwa mwendo wa kasi mno.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kitu pekee kinachowezesha wao kuwa madarakani hadi hivi leo sio uhalali wa kidhati kutoka kwa wananchi isipokuwa propaganda za kuwapumbaza wapiga kura.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Propaganda zinazolenga kuwaweka mateka Waingereza walio wengi kwa kutumia dhana ya kuwa hakuna mwengine mwenye mvuto kama yeye anayeweza kuwalinda waingereza kwa madhila makubwa zidi kutoka kwa chama cha wahafidhina.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiangalia mlolongo mzima wa historia ya chama cha Labour ni wazi kuwa kuna mambo yanayoshabihiana na hali inayojikita ndani ya chama cha mapinduzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapo zamani hata baada ya kuruhusu siasa za vyama vingi  chama cha mapinduzi kilikuwa ni chama kilichokuwa kinapata wafuasi wengi kutokana na hali ya kuwa wengi wa wananchi hawa walikuwa wakijinasabisha na misingi na falsafa za chama hicho. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata kama wengi walikuwa wakikatishwa tamaa na matendo ya viongozi walio wengi wa chama hicho ambayo ni tofauti na sura yake asili, kuwepo kwa umakini wa kimaamuzi haswa yale makubwa kama vile mtiririko mzima wa kubadilishana madaraka kuliwapa faraja wanachi wengi waliokuwa wanaendelea kukata tamaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hili na lile la kuwepo kwa baadhi ya viongozi wachache ambao tofauti na walio wengi, kauli zao na matendo yao yenye kuonyesha kuendelea kwao kuamini misingi na falsafa asilia za chama hicho, kuliwapa moyo wa matumaini watanzania walio wengi, wanachama na wasio wanachama. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali hii iliweza kuwazuia wanachama waaminifu wa chama hicho vijana kwa wazee, wenye sifa za umakini wa hali ya juu kutokisusa ama kutohama chama hicho kwa muda mrefu sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wengi hawa walikuwa bado wakiamini kuwa ipo siku chama hiki kitapata uongozi imara na makini utakaowezesha kurudisha chama na nchi yetu katika mstari ulionyooka na kuachana na siasa za sera za kukurupuka kwa minajili ya kuwalaghai wapiga kura tu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndio maana hata hivi karibuni tulipokuwa tukishuhudia siasa chafu za kupindukia mipaka ya utanzania na ubinadamu kwa ujumla, bado walikuwepo waliukuwa wakiamini kuwa mwishoni busara za uongozi wa chama hicho zingesimama na kurekebisha mambo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo hilo halikutuokea na waliukuwa wakiaminiwa kwa kazi hiyo ama walinyamaza kimya, walinyamazishwa au waliamua kukubali yaishe na kubariki siasa chafu zenye kukiuka misingi madhubuti ya chama hicho kutawala maamuzi ya vikao vyake vikuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yote yanaweza kufumbiwa macho lakini kitendo cha Mwenyekiti wa chama hicho kuamua kuzuia taarifa ya siri ya sekretarieti ya maadili ya chama hicho iliyokuwa ikielezea vigezo vya kimaadili vya wagombea wote kuzungumziwa na wanakamati kuu ni kosa kubwa la kihistoria.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maelezo kuwa wote wametoa rushwa hivyo wote sawa, kwa kweli ni upuuzi wa hali ya juu ambao kamwe hakuna aliyefikiri kuna siku Mwenyekiti wa chama hicho anaweza akaufanya.&lt;br /&gt;Hata kama historia na tafiti mbalimbali zinaonyesha wazi kuwa chama hiki kimekuwa kikumbatia rushwa na kiongozi wake kuishia kutoa vitisho vya mdomo tu, lakini inapofika mkuu huyo anahalalisha uchafu huo ambao ni tofauti na nguzo kuu asili za chama hicho ati kwa kuepusha kubomoka kwa chama, ni wazi safari ya mwisho imewadia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lingine ni lile la kuruhusu wanakamati kuu ambao wengine ni viongozi waandamizi bila ya aibu kutumia siasa ya ubaguzi ndani ya vikao vikuu kama hivyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pale machizi mbalimbali walioshindwa maisha walipokuwa wakitumia siasa haramu na chafu kama hizo kwenye vyombo mbalimbali vya habari, halali na haramu, baadhi ya watanzania makini ambao ndio walikuwa ngome ya mwisho wa chama hiki waliweza kuelewa na kuvumilia. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini pale anapokuja mtu mkubwa kama waziri mwandamizi akasimama akipinga kuchaguliwa kwa fulani kwa kuwa amezaliwa akiwa na mchanganyo wa kabila au rangi fulani, na wakubwa hao wakapigia makofi, kunyamaza au Mwenyekiti akahalalisha jambo hilo kama ni demokrasia, kwa kweli hiyo ni ishara mbaya mno.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vilevile ni dalili mbaya pale wakuu wa chama hicho na haswa wazee wenye busara waliokuwa katika makuzi ya siasa asilia za chama hicho na wengine kushiriki katika ujenzi wake wanapokuwa tayari kuweka kando maslahi ya watanzania kwa ujumla na kujali ushindi wa chama tu kama dira yao kuu ya kufanya maamuzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ushindi ambao kwao wao ni muhimu tu kutokana na uhakikisho wa kuwa wao na vizazi vyao vitaendelea kuwa madarakani daima milele hata kama ishara zinaonyesha kupotea kabisa kwa utaifa wetu ambao ndio umekuwa nguzo yetu muhimu kama nchi na jamii staarabu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa ujumla ingawa wengi wanaamini kuwa chama cha mapinduzi kimeweza kuvuka mtihani mkubwa kwa ushindi, ni wazi kuwa ushindi huo unaendana na kujisimika rasmi kwa siasa mpya zisizojali misingi na falsafa asilia za chama hicho ambazo kwa kweli ndizo zimekuwa nguzo kuu za kuendelea kwa uimara wake wakati wote huu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siasa hizi mpya ambazo zinalenga wingi wa kura tu na sio mipango madhubuti ya muda mrefu yenye kulenga kustawisha jamii kwa mapana na marefu daima haziwezi kuifanya CCM kuendelea kuwa chama cheney mvuto asili ambo hata kama mambo hayaenda sawa wananchi wataendelea kukiamini na kikihamini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siasa hizi zinazofuata mbinu za soko huria ambazo zinalenga kumnadi mtu kama bidhaa nyingine sokoni zinafanya chama hicho kutegemea uhalali wa umaarufu wa mwanasiasa huyo tu na sio mapenzi na imani juu ya chama hicho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bahati mbaya umaarufu huu unajengwa na matarajio hewa ndani ya mioyo ya wananchi, ambayo ama kwa mapungufu ya kiutendaji ya mwanasiasa huyo au ya kimfumo ni vigumu kuyafanikisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo basi kukifanya chama hicho kuwa mateka wa mwanasiasa huyo na wajanja wachache waliomzunguka wanye uwezo wa kucheza na akili za wapiga kura kwa muda Fulani tu. &lt;br /&gt;Hawa huwezesha hilo kwa kutumia mbinu mbalimbali za kihadaa ambazo daima huishia ama kuvuruga jamii au kuchokwa na wapiga kura.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapo wanaofikiri kuwa kupatikana kwa mgombea na baadaye kiongozi mwenye mvuto kama aliyechaguliwa hivi karibuni kuwa ni silaha muhimu ya kuhakikisha uimara wa chama hiki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mimi nasema ndio lakini ni kwa muda mfupi tu na hiyo hiyo ndiyo silaha ya kujiangamiza kwa muda mrefu.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Ni wazi ushindi uliopatikana Dodoma hivi karibuni ni mwanzo wa safari isiyo rasmi ya mwisho ya chama cha mapinduzi.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-1329599135058845224?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/1329599135058845224/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=1329599135058845224' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/1329599135058845224'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/1329599135058845224'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2011/09/tulikotoka-mwanzo-wa-safari-ya-mwisho.html' title='TULIKOTOKA: MWANZO WA SAFARI YA MWISHO YA CCM'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-832753142695782492</id><published>2011-09-23T09:11:00.000-07:00</published><updated>2011-09-23T09:15:39.329-07:00</updated><title type='text'>CHADEMA Ishinde kwa Kushindwa!</title><content type='html'>22 Sept 2011&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matukio ya hivi karibuni ambayo yamefanikiwa kupata nafasi ya juu katika vyombo vya habari kuhusiana na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) yamenijengea mtazamo kuwa ili CHADEMA kushinda katika safari ndefu iliyonayo kama mtawala mbadala kinapaswa kushindwa sasa.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Kitendo cha hivi karibu ambapo wafuasi na viongozi wa CHADEMA wakiwa pamoja na wabunge wawili wa chama hicho, Bwana Sylivester Kasulumbayi na Bi Susan Kiwanga kumtusi, kumkwida, kumteka na hata kumdhalilisha mkuu wa wilaya ya Igunga Bi Fatuma Kimario ni muendelezo wa dalili mbaya ya nini kinaendelea ndani ya chama hicho, ni wapi kinaelekea kama kundi la maslahi ya kisiasa na wapi kinaipeleka Tanzania yetu kama taifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo itakuwa kosa kuangalia kitendo hiki ambacho mimi nakiita kitendo cha kihuni ingawa wapo wanaothubutu kukiita kitendo cha kishujaa na ukombozi, kama tukio linalosimama pekee. Huu ni muendelezo wa mambo mengi ambayo yamekuwa yakijitokeza ndani na nje ya chama hiki kwa muda mrefu sasa ambayo yamefanya baadhi ya watu ambao hapo kabla walithubutu kuamini kuwa chama hiki kinapaswa kuwa mbadala makini wa utawala wa nchi yetu kukitazama kwa jicho la tahadhari zaidi ya matumaini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nadhani sihitaji kuyataja matukio hayo ambayo mengi yamekuwa yakipata nafasi ya kipekee katika vyombo vya habari na mengine yakiwa yanafunikwa haramu ipite. Hapa ningependa kulipitia tukio hili la karibuni kuangalia linaelewekaje na nini athari yake kwa CHADEMA na taifa kwa ujumla endapo wapiga kura wa Igunga ama wataweza au hawataweza kumpa ushindi mgombea wake katika uchaguzi wa tarehe 2 Oktoba 2011.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa miaka kadhaa sasa na tangia kuanzishwa kwa chama hiki, kimekuwa kikiandamwa na tuhuma za ukabila na udini. Yaani chama kinachoweka mbele maslahi ya kabila, eneo na dini fulani. Kabila likiwa wachaga, eneo likiwa la ukanda wa kaskazini wa Tanzania na udini ikiwa wakristo.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Kwa kiasi fulani CHADEMA wamekuwa wakijitahidi kushughulikia tatizo hili ama kwa kukanusha ama kuchukua hatua mbalimbali za tahadhari kujivua tuhuma hizo. Hatua hizo ni pamoja na kuhakikisha mabadiliko ya mara kwa mara ya uongozi wa juu wa chama hicho ikiwemo nafasi ya Mwenyekiti.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Hatua ambayo ilikuwa kwa kiasi fulani ikionyesha dalili za mafaniko hadi mwaka 2009 zilipolazimika kutuwama ambapo kwa mara ya kwanza kilipata mwenyekiti wa kwanza wa zaidi ya muhula mmoja tofauti na ilivyokuwa hapo awali kwa Mwanzilishi Mzee Mtei (Mkristo na mchaga) na baadaye Mzee Makani (Muislamu na Msukuma).&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Katika uchaguzi wa mwaka 2009, Mwenyekiti wa sasa Freeman Mbowe (Mkristo na Mchaga) kwa kutumia mbinu kadhaa alifanikiwa kuhalalishwa kuwa kiongozi wa chama hicho kwa kipindi cha pili mfululizo na hivyo kukiuka busara ya mabadiliko ya mara kwa mara ambayo yamekuwa yakihakikisha mwamko mpya(rejuvenation) wa kichama kila baada ya miaka michache.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mabadiliko ya mara kwa mara ya uongozi wa juu yaliweza kutoa nafasi kwa chama kupanuka na kuondoa kiwingu kuwa chama hiki ni chama cha watanzania wa kabila la Uchaga na wengine ni wasindikizaji tu tofauti na wenzao wa CUF.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Uamuzi huu ulitibua nafasi ya chama hicho kuthibitishia kwa vitendo upotofu wa tuhuma za maadui zake na zaidi umma wa watanzania kuwa sio chama cha kikabila. CHADEMA ikashindwa kujiondoa katika tuhuma hizo na zaidi kujivika rasmi gamba la ukabila na udini mbele ya macho ya walio maadui na hata baadhi ya marafiki wakiwemo wanachama na wafuasi wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama vile hilo halitoshi, tukielekea katika uchaguzi wa rais na wabunge wa mwaka 2010 ambao CHADEMA ilionyesha muamko mkubwa katika medani za siasa nchini, CHADEMA ama kwa kudhamiria, kutokudhamiria au kwa kulazimika, wakafanya kosa jingine ambalo badala ya kuwanasua katika kiwingu cha ukabila na udini wakajikuta wanajisimika ndani ya wingu la Udini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni ukweli ulio wazi kuwa kwa wa miaka kadhaa, wanamikakati wa CHADEMA wamekuwa wakitamani uungwaji mkono wa Kanisa la Katoliki ambao hadi miaka ya karibuni ulikuwa kama ngome muhimu ya kisiasa kwa CCM. Kwa CHADEMA kupata angalao chembe tu ya uungwaji mkono huo wa kanisa la katoliki katika chama chao ambacho wakati waislamu wamekuwa wakikiona kama chama cha waksrito zaidi, wakatoliki wamekuwa wakikiona kama chama cha Walutheri zaidi ilikuwa ni neema ya moto.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Katika uchaguzi wa mwaka 2010, kwa kiasi fulani CHADEMA ilifanikiwa kupata uungwaji mkono wa kanisa la katoliki kama mfumo imara wa kijamii na kisiasa katika nchi yetu. Hili lilikuja ama kutokana na kanisa hilo kama watanzania wengine kuchukizwa na maovu na usaliti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) au kutokana na dalili za uwezekano wa ushindi wa uhakika wa mgombea Urais wa CHADEMA ambaye ni kiongozi wa kiroho na aliyekuwa mtumishi wa ngazi za juu wa chombo nyeti cha kanisa hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kitendo cha viongozi wa kanisa la Katoliki kuanzisha na kuendeleza mpambano mkali wa majukwaani na katika alteri za kanisa kuwashutumu viongozi wa chama tawala cha CCM na serikali yake inayoongozwa na Rais na Mwenyekiti Muislamu, kabla na hata wakati wa uchaguzi huo kilijenga mtazamo wa kuwa kanisa hilo na hivyo wafuasi wake walipaswa kuiepuka CCM na wagombea wake na hivyo kuashiria kuwa CHADEMA ndio chaguo lao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali hii ilileta mpasuko mkubwa wa kimitazamo katika kuelekea uchaguzi huo na hata baadhi ya wanasiasa, viongozi wa makanisa na misikiti na wapiga debe mbalimbali kuthubutu kuendeleza kampeni za udini. Kampeni zilizolenga ama katika kuhakikisha ushindi wa kutwaa nguvu za dola kwa upande wa CHADEMA na kulinda hatamu ya nguvu hizo kwa upande wa CCM.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Wakati hali hii kwa kiasi fulani iliwezesha kuongeza mafanikio ya CHADEMA katika uchaguzi wa ubunge na hata kura za urais, hali hii ilifanikiwa kusimika rasmi gamba la Udini dhidi ya CHADEMA. Kwa lunga nyingine uchaguzi wa mwaka 2010 kwa upande mmoja ulibariki CHADEMA kama chama cha ushindi kuelekea mwaka 2015 na wakati huohuo kukivika gamba la udini chama hicho ambalo ni kikwazo kwa kutimilika kwa baraka hiyo ya ushindi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni katika muktadha huu wa nyota ya ubarikio wa ushindi kwa upande mmoja na gamba la dalili za laana kwa upande mwengine pamoja na matukio kadhaa tangia baada ya uchaguzi wa mwaka 2010 ndio nalazimika kujenga mtazamo kuwa CHADEMA itashinda mbele kwa kushindwa hivi sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nasema hivyo kwa kuwa naamini kama ambavyo CCM walivyokumbwa na janga la kusarandiwa, kuvamiwa na baadaye kutekwa na mafisadi, CHADEMA ya sasa sio tu imekuwa kimbilio la wajanjawajanja wanaoamini kuwa katika mtaji wa chuki kuu inayokikumba CCM miongoni mwa watanzania wanaohisi kuwa wamesalitiwa lakini pia wanaoamini kuwa ushindi wao katika duru za siasa na uchumi unahakikishwa zaidi katika CHADEMA.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;CHADEMA inageuka kutoka kuwa ngome ya mapambano ya demokrasia na upingaji wa maovu dhidi ya wananchi na taifa lao na kuelekea kuwa ngome ya mafanikio ya urahisi na uhakika kisiasa na kiuchumi.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Hali hii inakifanya CHADEMA kama chama kushindwa kupata nafasi ya kujichunguza na kujitambua na pia kuwa na wanaCHADEMA wakiwemo baadhi ya viongozi wake ambao wako tayari zaidi kujidanganya na kukimbilia kukumbatia siasa hovyohovyo na za hatari kwao binafsi na kwa taifa.Siasa ambazo  wanaamini ndizo zinazowavutia zaidi watanzania waliochoka na CCM na kamwe haziwezi kuwageuka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kitendo cha viongozi wa chama kuthubutu kumteka na kumburuza kiongozi wa serikali kinafanya wengi wajiulize maswali kama kweli chama hiki ndicho kinapaswa kuwa chama tawala mbadala. Lakini zaidi kitendo cha viongozi wa chama ambacho kinakabiliwa na tuhuma ya udini kumdhalilisha Mwanamama wa Kiislamu kwa kumvua hijabu yake kinaonyesha jinsi gani chama hicho kilivyoingiliwa na watu ambao kwa idiadi yawezekana wakawa mtaji wa kisiasa lakini kwa kimantiki ni mzigo hatari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbaya zaidi badala ya kuangalia ni jinsi gani wanaweza kulisawazisha kosa hilo kubwa kisiasa, wanatokea viongozi wakuu wa chama hicho na kutoa matamsha kama vile mwanamama yule alijitakia kukumbwa na udhalilishaji huo na hata wengine kujaribu kufananisha kitendo hicho cha kihuni na juhudi za viongozi adhimu kama Mwalimu Julius Nyerere na Mzee Madiba Mandela. Kama ambavyo mbunge wa CHADEMA Bwana Tundu Lissu alivyoripotiwa katika magazeti akisema.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kuwa wakati CHADEMA kama chama kinaonyesha kukua kwa kupata wafuasi, washabiki na hata wanachama lukuki, ukuaji huu sio ukuaji wa kuaminika. &lt;br /&gt;Ni ukuaji unaotokana na ubaya wa CCM zaidi ya uzuri wa CHADEMA.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Ni ukuaji ambao unaoetegemea kufaidika na makosa ya CCM na wengine zaidi ya ukuaji wa kufaidika na mikakati madhubuti yenye kujengwa katika misingi imara itakayohimili dharuba na tufani za kisiasa.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Ni ukuaji unaopalia makaa moto wa kujimaliza kuliko ule wa kupanda mbegu za matunda ya kudumu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukweli ni kuwa wakati ushindi wa CHADEMA katika uchaguzi wa Igunga utapelekea viongozi wa aina hii wa CHADEMA na wafuasi wake wengi wenye mitazamo kama ya viongozi hao kuona kuwa siasa za aina hiyo zinalipa na hazina athari kwao, kushindwa katika uchaguzi huu kwaweza kuwa nafasi adimu kwa viongozi wa chama hiki kupata ushujaa wa kukaa chini kujiangalia na kuwa na uthubutu wa kujisahihisha kabla ya ama kukutana na tufani ya kisiasa huko mbeleni au kulifikisha taifa pabaya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wenzao wa CCM pamoja na makosa mengi wamekuwa wakiyafanya, kimbuka kidogo cha mwaka 2010 kimewaamsha, kujiangalia na kukubali kujisahihisha kwa njia ya kujivua gamba la ufisadi. CHADEMA kwa upande wake wanapaswa kutikiswa na kaupepo cha kisiasa huko Igunga ili kukubali kujiangalia na kuanza mikakati thabiti ya kujivua magamba ya ukabila na udini ambayo ni hatari zaidi kwake na kwa jamii na taifa letu kwa ujumla zaidi ya lile la ufisadi la CCM.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Lakini zaidi kushindwa kwa CHADEMA sasa kutawezesha uongozi wake na zaidi washabiki wao kuwashinikiza kujisahihisha na kuanza kufikiri na kutenda katika taathira ya hulka ya Serikali Mbadala (Government in waiting) inayosubiri kuongoza taifa hilihili ambalo matendo yao ya sasa yanaelekea kuliharibu.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Kushindwa kwa CHADEMA sasa ni kushinda kwa CHADEMA huko mbeleni.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-832753142695782492?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/832753142695782492/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=832753142695782492' title='2 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/832753142695782492'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/832753142695782492'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2011/09/chadema-ishinde-kwa-kushindwa.html' title='CHADEMA Ishinde kwa Kushindwa!'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>2</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-758264606113745549</id><published>2011-08-31T23:44:00.000-07:00</published><updated>2011-08-31T23:50:59.653-07:00</updated><title type='text'>Nashindwa kuelewa!</title><content type='html'>@1st Sept 2011&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nashindwa kuelewa kama serikali ya CCM hapo mwanzoni ilikuwa na nia ya kuanzisha mahakama ya Kadhi hadi pale viongozi na asasi za "kanisa" walipokuja juu dhidi yake na kupelekea kutikiswa kwa mtaji wake katika soko la kura, iweje leo tujidanganye kuwa uamuzi wa serikali haukushawishiwa ama kushuritishwa na kanisa!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini pia wakati naamini katika busara za kukubali hoja hii kwa maslahi ya utanzania wetu, nashindwa kuelewa  hii hoja ya kuwa kodi ya mtanzania haiwezi kutumika kuendesha mahakama ya Kadhi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Iweje isiwe sawa kutoa kodi hizo kwa asasi za dini wakati tayari tumekuwa na tunaendelea kufanya hilo kwa kusaidia mabilioni ya kodi hizo kwa asasi na mashirika ya kidini?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimewahi kusikia kuwa mara baada ya Rais kushinda uchaguzi ambao inaaminika kuwa uliathiriwa na msimamo hasi wa "kanisa" dhidi ya serikali na CCM, serikali imeahidi ama kutoa zaidi ya shilingi bilioni 50 kwa mashirika na asasi kadhaa za "kanisa".&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nashindwa pia kuelewa ni vipi kodi ya mtanzania haipo kwa ajili ya maslahi ya watanzania wakati waislamu ni sehemu ya watanzania?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na pia ni utanzania gani tunaoujenga kwa kudai kuwa ni haramu kwa kodi ya David kutumika kwa maslahi ya Omar?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naamini kuwa msimamo huu unaweza kuwa hafueni ama ushindi kwa mtizamo wa watanzania wa upande mmoja lakini kuongeza malalamiko na hisia hasi upande mwengine. Lakini pia ni muhimu kutambua kuwa wakati wale wa upande mmoja wanadhani kuwa hotuba hii ya Rais imeonyesha uthabiti ambao wengi tunapenda kuuona unaongoza asasi hii nyeti ya Uongozi, wapo wa upande mwengine ambao watachukulia hotuba hii kama ulegelege wa kukubali kushindwa na nguvu za upande mwengine na sio kwa busara za kulinda utaifa wetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukweli ni kuwa mzizi wa tatizo hili ni ujanjaujanja uliotumika kuliingiza suala hili la mahakama ya Kadhi katika ilani ya CCM ambayo ililenga kuidhibiti CUF katika soko la kura.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na sasa nahofia msimamo wa sasa wa serikali ya CCM ni kujaribu kuidhibiti CHADEMA katika soko la kura la 2015.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi pia kuwa ubinafsi na ujanjaujanja wa baadhi ya wanasiasa, wasomi na zaidi viongozi wa dini ulifanikiwa katika kubomoa hoja hii ya mahakama ya kadhi na kuijengea mazingira ya uadui kati yetu badala ya kuijenga kama chachu ya upendo kati yetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii imetokana na hulka ya ushindani na propaganda hasi iliyogubika mjadala mzima wa mahakama ya Kadhi kama ilivyokuwa ukiendelea bungeni, katika vyombo vya habari, katika kampeni, misikitini na makanisani, vijiweni na hata majumbani mwetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati waislamu waliongea kwa mtazamo wa haki yao na hisia za kubaguliwa na mfumo, wakristo walijikita zaidi "ubaya" na nia mbaya ya Mahakama ya Kadhi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wengi wao walikwepa kuongelea yaliyomo katika mchakato mswada wa sheria ya kuendesha mhakama hiyo na sehemu ya katiba katika suala hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mtazamo wangu hutuba hii ni kipenga cha kuanzisha rasmu mjadala huu na sio kuhitimishwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwisho naamini kuwa hii ni sehemu ya changamoto ambazo kama taifa linaloendela tumekuwa na tunapaswa kupitia ili kukomaa kidemokrasia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Muhimu ni kuendeleza utamaduni wa shauku ya kutaka kujua mambo kwa undani wake zaidi ya propaganda za viongozi wawe wa kisiasa ama kijamii na wajenga maoni wetu, kuvumiliana na pengine kuaminiana kwamba wote tuna nianjema katika kujenga tanzanianjema.&lt;br /&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-758264606113745549?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/758264606113745549/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=758264606113745549' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/758264606113745549'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/758264606113745549'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2011/08/nashindwa-kuelewa.html' title='Nashindwa kuelewa!'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-7864991499296320979</id><published>2011-08-30T22:56:00.000-07:00</published><updated>2011-08-30T22:58:21.057-07:00</updated><title type='text'>Africas silent anger!</title><content type='html'>August 2011&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Reports of Libya rebels massacre of black skinned Libyans and emigrants from sub sahara Africa makes my blood boils with anger.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;However this is not news to me as I saw it from the beginning that religious fanatism and racism is fundamentally centered within the NATO supported rebels.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;They hated to be led by a Bedouin Ghadafi, they hated his African agenda as it was obvious during the massacre of black Africans some years ago around Benghazi and bengazis dominated eastern tripoli.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Unfortunately there those misguided Activists have guts to question why most of African government stand of not rushing to legitimize these racist fanatic myopic opportunists western nurtured and aided venture....aghhhh&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Thinking Africans wont embrace rebels due to so called Ghadafi bankrolling history is as closed minded as those thinking that #libya is only oil issue.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;If it's the issue of bankrolling it is the African leaders silence on the utterly abuse of their little trust to international community safeguarding their masters paycheck that should be noticed.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Actually most if those who were really bankrolled like Senegal, Gambia, Malawi and others were the first to betray him.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;It's time for those who think they know us better than ourselves to understand that though we are fucked up as a continent we still cling to principles over opportunism when it comes to what is Africa and our grand aspirations!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;I wish those #libya rebels cheerleaders would notice the silence anger that is boiling inside African population and how it gonna blow!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-7864991499296320979?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/7864991499296320979/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=7864991499296320979' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/7864991499296320979'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/7864991499296320979'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2011/08/africas-silent-anger.html' title='Africas silent anger!'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-3037787033214572224</id><published>2011-07-29T07:02:00.000-07:00</published><updated>2011-07-29T07:04:53.122-07:00</updated><title type='text'>Ya Bungeni ni matunda ya soko la kura...</title><content type='html'>Ya Bungeni ni matunda ya soko la kura...&lt;br /&gt;29 June 2011&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni hatari, si salama na wala sio busara kuacha hatima ya taifa letu iamuliwe kwa mujibu wa maslahi ya soko la kura. Soko ambalo kwa muda mrefu tumekuwa tunalidumaza kifikira. Soko ambalo badala ya kuwa mkombozi wa mtanzania limegeuzwa kuwa janga la utaifa wetu. Soko lililogeuzwa kuwa mazalia  uozo wa kisiasa. Soko ambalo kamwe halitaweza kutuondoa katika lindi la maadui umasikini, ujinga, maradhi, ufisadi na ubaguzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bunge letu la sasa ni matunda ya mfumo na utamaduni wa kisiasa unaojengek​a wenye kuweka mbele maslahi ya soko la kura na kusahau ama kudharau wajibu wa uongozi na kamwe sio kupanuka kwa demokrasia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati wanasiasa wetu wanaamini kuwa siasa za kukosa busara na staha dhidi ya "Watawala" zinashabikiwa na vijana wengi hivyo ni mtaji muafaka wa kura, wamesahau uongozi ni dhamana na una majukumu yake!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kimsingi baadhi yao wanaamini kuwa hizo ndio siasa zinazovutia wapiga kura vijana. Hawajali wajibu wao kama viongozi. Wanasahau ni Tanzania wanayoijenga sasa ndiyo wayakayopaswa kuitawala wakishika dola.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini zaidi ufinyu wa ustadi katika siasa za kujenga zenye kuambatana na uerevu wa masuala ya kitaifa na kidunia katika uga wa siasa unapelekea baadhi ya wanasiasa wetu kuamini katika siasa za ujanjaujanja ili kuficha mapungufu yao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naweza kusema hili ni zao historia ndefu ya nchi yetu kujikita katika utoaji wa bora elimu na pia tatizo la ukosefu wa watu wenye ujuzi, uwezo na umahiri wa masuala mbalimbali ya kimaendeleo katika platform za siasa kama bunge letu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini pia ukosefu wa hulka ya uthubutu miongoni mwa watanzania wenye elimu bora, misingi thabiti na umahiri wa masuala ya uongozi na siasa kuingia katika taaluma ya siasa na kukimbilia maeneo salama kimaisha na kimaslahi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande mwengine soko hili la kura limefanikiwa kutupa viongozi tunaowaona na wakaendelea kupata  ushabiki na hata ufuasi miongoni mwetu hasa sisi vijana kutokana na miaka mingi ya matumizi mabaya ya imani ya watanzania. Imani ambayo watanzania waliwapa viongozi wao pamoja na asasi za utawala. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kutokana na tabia za baadhi ya viongozi wetu kutumia vibaya imani na ridhaa ya watanzania hata kufikia kuwadhihaki na kuwabeza huku wakishindwa kutatatua hata ya matatizo ya msingi ya wananchi hao nako kumewezesha wanasiasa wajanjawajanja kuchakachua soko la kura. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uchakachuaji ambao badala ya kuwapa nafasi watanzania kuwa na upeo mkubwa wa kuchagua viongozi bora unawafanya wawe wahanga wa kuchagua viongozi wahuni zaidi, walafi zaidi, wazembe zaidi na wabinafsi zaidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ili kuepukana na hatari hii ni wajibu wetu sote kuwa mstari wa mbele kujenga upya misingi ya siasa safi na uongozi bora. Na hili litafanikiwa endapo sote ambao tumebarikiwa kupata elimu na kujengeka kifikira kukataa kuwa wahanga wa siasa zenye kujali na kuamini katika kasumba za kisiasa badala Ukweli wa mambo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini pia kuwa tayari kuhakikisha kuwa kila mtanzania anapaswa kujua ukweli wa mambo na kumuepusha kuwa mhanga wa siasa za kasumba, hovyohovyo na majitaka. Siasa ambazo huwezesha udumavu wa kifikira na pia kuwa mtaji wa wanasiasa wajanjawajanja, wahuni na hata madhalimu wanaojivika vilemba vya uwanamapinduzi, uzalendo na ukombozi. Wanasiasa ambao wako tayari kuweka rehani mustakbali wa taifa letu kwa maslahi yao ya kisiasa na binafsi.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-3037787033214572224?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/3037787033214572224/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=3037787033214572224' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/3037787033214572224'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/3037787033214572224'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2011/07/ya-bungeni-ni-matunda-ya-soko-la-kura.html' title='Ya Bungeni ni matunda ya soko la kura...'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-8562002529043250176</id><published>2011-07-18T03:30:00.000-07:00</published><updated>2011-07-18T03:33:01.777-07:00</updated><title type='text'>Nelson Mandela Leadership Philosophy and my Zanzibarinjema Dream.</title><content type='html'> Happy Birthday Mzee Madiba. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Though I abhor the western pimping-iconization of #NelsonMandela, I duly admire and salute his unshaken philosophy of forgiveness n rainbow nation.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;To understand the value of Nelson Mandela philosophy Tanzanians need to look Zanzibar timulutous history.   &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Zanzibar timulutous history of never ending sociopolitical cleavages has dwarf all it's economic power potential.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;While we now have a new Gov of National Unity dispensation in #Zanzibar, more needs done to protect and nurture the  spirit of cooperation in making Zanzibarinjema.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;The noble leadership of three genuine and humble brothers, Ally Shein, Seif Sharif and Ali Seif Idi, needs be supported by institutions of forgiveness, trust and hope above all.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;For this to be achieved and sustain above the three personalities and the constitution, a culture of constructive engagement and embracing of the power of diversity is paramount.  &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;More, I sometime think maybe we should dare to establish Kamisheni ya Ukweli, Uwazi na Maelewano!&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-8562002529043250176?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/8562002529043250176/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=8562002529043250176' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/8562002529043250176'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/8562002529043250176'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2011/07/nelson-mandela-leadership-philosophy.html' title='Nelson Mandela Leadership Philosophy and my Zanzibarinjema Dream.'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-6328453322423048986</id><published>2011-07-11T09:42:00.000-07:00</published><updated>2011-07-11T09:43:33.063-07:00</updated><title type='text'>Mtazamo wangu kuhusu majibu ya Zitto dhidi ya makala ya leo katika gazeti la Tanzania Daima</title><content type='html'>Mtazamo wangu kuhusu majibu ya Zitto dhidi ya makala ya leo katika gazeti la Tanzania Daima.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sifa kuu za mbumbumbu wa siasa ni kupenda na kuamini katika siasa chafu, wivu na uadui! Ni wazi kinachofanywa na wahariri wa gazeti hilo linalomilikiwa na mwenyekiti wa chama chake ni mfano halisi wa umbumbumbu wa siasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Shutuma dhidi ya Zitto kwa kulalamika mtandaoni kuhusiana na kitendo hicho cha Tanzania Daima kuandika habari yenye nia mbaya kwake zinaonyesha kuwa kuna watu wangependa kuona Zitto anakufa kisabuni. Mpaka Zitto alipofikia kureact namna hii ni wazi kuna juhudi alizofanya kuleta busara miongoni mwa viongozi wenzake ambao ukweli ni kuwa wengi wao wanaamini ili wafanikiwe wao ni lazima Zitto aangamizwe bila ya kujali kuwa in a way wanaangamiza chama chao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini pia hii tabia ya kutumia busara ya kuepusha taswira ya mgawanyiko ama mgogoro ndani ya Chadema katika kufunika uozo wa ubadhirifu aka ufisadi na siasa chafu zenye kujaa chuki haina tofauti na ile ya wenzao wa CCM ya kutumia Amani na Utulivu katika kufunika uozo wao. Ni wazi athari ya kuamini katika ujanjaujanja huo zinainekana zinavyowazamisha kama chama na taifa kwa ujumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maadui wa kweli wa umoja, amani na utulivu ama ndani ya vyama vyenu ama nchi yetu ni wale wanaonajisi umoja, amani na utulivu huo kwa kuendeleza ubadhirifu aka ufisadi, siasa chafu, wivu na chuki na sio wale wanaothubutu kusimama kuonyesha, kukemea na kujitetea dhidi ya uharamia huu wa kisiasa na hata kimaisha&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini pia yawezekana kwa kuwa wengi hawajui ni mangapi amenyamazia ndio maana baadhi wanasisitiza busara ya kunyamaza. Wakati wanaona kuwa ni busara kwa Zitto kunyamaza wenzake  wanachukulia kama udhaifu na mtaji katika kufanikisha nia yao mbaya iliyojikita katika utamaduni wa kuamini katika siasa chafu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati wengi wanasisitiza Zitto kunyamaza kwa maslahi ya chama chao wenzake busara hiyo hawana na kwa muda mrefu sasa wamekataa kuitambua. Busara ya kunyamaza huku wenzako wakikumaliza inageuka ujinga pale inapohusu wasio amini katika busara hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa ujumla ni vizuri maadui wake wanajianika ili watu watambue nia zao chafu na mipango yao haramu!&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-6328453322423048986?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/6328453322423048986/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=6328453322423048986' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/6328453322423048986'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/6328453322423048986'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2011/07/mtazamo-wangu-kuhusu-majibu-ya-zitto.html' title='Mtazamo wangu kuhusu majibu ya Zitto dhidi ya makala ya leo katika gazeti la Tanzania Daima'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-3452648234165513712</id><published>2011-05-18T03:37:00.000-07:00</published><updated>2011-05-18T03:38:34.445-07:00</updated><title type='text'>Mtizamo wangu kuhusu matukio ya hivi karibuni na mitazamo kuhusu kesi ya Balozi Mahalu</title><content type='html'>Wednesday 18th May 2011&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naweza kusema kuwa siasa za ujanjanja na hovyohovyo zimefanikiwa kuifikisha nchi kwenye state of paralysis, from state capacity to political thinking even among the self anointed critical citizens....&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimejaribu kuisoma sijui ni ripoti ama makala iliyotumwa katika jukwaa la Jamiiforums.com hivi leo, kuona ni wapi ama ni vipi Mkapa amemkaanga Kikwete zaidi ya kujikaanga mwenyewe sioni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nikiangalaia kwa karibu nakubaliana na Mbopo kuwa huu ni muendelezo wa siasa za ujanjaujanja ambazo sasa zinaelekea kujikita katika mahakama zetu na kugeuza kuwa kama yale majukwaa rasmi na yasiyo rasmi kisiasa ambayo inaelekea kwa baadhi ya wanasiasa kama Mabere Marando, hayajatosheleza kufisadisha siasa za nchi yetu kwa manufaa ya muda mfupi na yale binafsi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watanzania wote tumegeuzwa kuwa mashabiki wa ama upande wa Kikwete ama upande wa “Wengine” bila ya kujali jukumu letu la kuweka mbele umakini zaidi ya ushabiki katika kufuatilia, kuchambua na kuzungumzia maswala muhimu ya kuikomboa nchi yetu kama ambavyo tunapenda kujinadi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siamini kama ushahidi huu wa kuwa serikali ilikuwa na taarifa na kwamba eti taratibu zote zilifuatwa zingeliweza kuwa ushahidi wa maonevu dhidi ya mshitakiwa katika macho ya washabiki wa upande mwengine ambao unadai kuwa huu ni uonevu na ulipaji kisasi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wote hapa tunajua kuwa utawala wa Mheshimiwa Mkapa ulikuwaje, inashangaza kuona kuwa kuna watu wanadhani kuwa Waziri wa wakati ule alikuwa na uwezo wa kukataa kile ambacho bosi wake Rais anataka ama amekubali kifanyike.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini pia inashangaza kuona kuwa usemi wa kuwa ununuzi huo ulifuata taratibu na ulikuwa na baraka zote za serikali unaweza kusafisha uwezekano wa wizi ama rushwa wakati wote tunajua kuwa hata EPA ilikuwa na baraka na utaratibu uliofuatwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Halafu huu mchezo wa kukimbilia kuwa kesi kama hizi ni uthibitisho dhana, madai ama shutuma  kuwa Rais ana hulka ya kisasi ni ujinga na upumbavu. Haiwezekani watu tupige kelele Rais achukuwe hatua dhidi ya ufisadi na mafisadi halafu anapochukuwa hatua dhidi ya wale ambao hawamo katika listi zetu za kuwachukia ama kuwahukumu kuwa ndio mafisadi basi Rais ndio ageuzwe mkosaji. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mtazamo wangu, fikira kama hizi ndio zinazowavunja nguvu na kuwafanya baadhi ya viongozi wetu kuamua ama kujiunga na ufisadi ama kuunyamazia huku wakilinda na kuboresha maslahi yao kwani wanakuja amini kuwa hao wanaopaswa kuwapigania ni mabingwa wa kutoa shukurani za punda kwa kuwapiga mateke pale wanapojitahidi kuwatetea na kuwalinda. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Zaidi naamini umefika wakati na ni muhimu kwa Uongozi wa Mahakama zetu kuchukua hatua kuzuia madhubutu kuhakikisha kuwa mahakama zake hazirasimishwi kuwa majukwaa ya siasa za ujanjaujanja na hovyohovyo kama ambavyo imekuwa ikijionyesha katika miaka ya hivi karibuni. Kama kweli hii habari imetolewa na upande wa utetezi unaongozwa na Wakili Marando ambaye hivi karibuni amekuwa wazi akitumia habari ama sehemu yake katika shughuli za mahakama kufanyia siasa, ni lazima hatua kali zichukuliwe kabla hali hii haijaota mizizi. Inatosha kuona jinsi mahakama zetu zimegeuzwa kuwa kisima cha rushwa na uonevu mwengine, kuruhusu siasa za majukwaani kuota mizizi katika mahakama zetu ni kucheza na hatima ya nchi yetu.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-3452648234165513712?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/3452648234165513712/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=3452648234165513712' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/3452648234165513712'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/3452648234165513712'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2011/05/mtizamo-wangu-kuhusu-matukio-ya-hivi.html' title='Mtizamo wangu kuhusu matukio ya hivi karibuni na mitazamo kuhusu kesi ya Balozi Mahalu'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-400469612766878931</id><published>2011-04-08T00:34:00.000-07:00</published><updated>2011-04-08T00:36:11.900-07:00</updated><title type='text'>Maoni yangu kuhusu mjadala wa mchakato wa katiba mpya</title><content type='html'>******Maoni yangu kuhusu mjadala wa mchakato wa katiba mpya&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nakubaliana na suala la kuwa na muswada wa Kiswahili ingawa sidhani kama hilo liwe jambo la kuathiri mchakato huu muhimu kama ambavyo baadhi ya watu wanavyojaribu kuchochea na wengine kushabikia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pia nakubaliana na suala la muda wa mchakato na ukomo wa hatua moja hadi nyingine kuwekwa bayana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vilevile nakubaliana na maoni kuhusu suala la kutajwa kwa wazi constitution making bodies na nguvu zake na Kupunguza nguvu za maamuzi mikononi mwa Rais.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pia suala la hadidu za rejea kuwekwa na bunge lakini naunga mkono suala la uteuzi kubaki mikononi mwa Rais huku bunge likaachiwa jukumu la kuwapitisha na pia kuchagua uongozi wake ingawa nafasi ya Katibu kubaki kuwa jukumu la serikali iwe Rais ama waziri mhisika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Suala la sheria dhidi ya watakaozuia shughuli za kamati ni muhimu kuwepo ukichukulia dalili mbaya zinazoanza kujionyesha na utamaduni wa kutoheshimu wala kuvumilia mawazo mbadala unaojijenga katika jamii. Si CCM itakayoamua lakini ni mahakama zetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Napinga kabisa maoni ya kuwa mijadala ya maoni kufanyika majomboni chini ya uongozi wa wabunge. Wabunge wetu wengi hawana ujuzi wa kuongoza mijadala ya maoni tofauti, wengi hawana heshima katika jamii zao, wamejawa na chuki za kiitikadi na pia hawana nidhamu ya ukweli.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maoni yangu ni kuwa mijadala ianze katika ngazi za kata ambako itasimamiwa na watendaji wa kata wakisimamiwa na wawakilishi wa kamati, asasi za kiraia na vyama vya siasa(mmoja mmoja). Hapa watakusanya maoni yote kama yalivyo na kusimamia uchaguzi wa wawakilishi wao (idadi iwe watano- mwanaume, mwanamke, kijana, mwanamama, kiongozi wa kijamii) watakaokwenda katika mjadala wa wilaya ambao nao utachakusanya maoni kama yalivyo na kuchagua wawakilishi wa mkutano wa mjadala wa kitaifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maoni yatakayotoka katika ngazi ya wilaya yatakuwa streamlined katika masuala na wingi wake halafu yapelekwe katika mjadala wa kitaifa ambako watashiriki wawakilishi wawili AMA watatu kutoka katika kila wilaya ambao watachukua asilimia 50 hadi 60 ya mkutano.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pia kutakuwa na wawakilishi wa makundi maalumu, asasi za kiraia, viongozi ama makundi ya kijamii, wafanyakazi, wakulima, wafanyabiashara, wataalamu na pia wawakilishi wa vyama vya siasa (mmoja kutoka kila chama chenye usajili na uwiano wa kura za uchaguzi uliopita (popular votes) kwa vile vilivyopo bungeni)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maoni hayo ndiyo yatumike kutengeneza rasimu ya katiba mpya itakayopelekwa na kujadiliwa katika national constitutional assembly or convention kabla ya kupelekwa bungeni kama mswada halafu kupelekwa katika kura ya maoni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nawakilisha&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-400469612766878931?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/400469612766878931/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=400469612766878931' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/400469612766878931'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/400469612766878931'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2011/04/maoni-yangu-kuhusu-mjadala-wa-mchakato.html' title='Maoni yangu kuhusu mjadala wa mchakato wa katiba mpya'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-384075715671495282</id><published>2011-02-03T04:06:00.000-08:00</published><updated>2011-02-03T04:10:30.098-08:00</updated><title type='text'>Siasa zetu, Nguvu za Maaskofu na Mahusiano ya jamii zetu</title><content type='html'>January 2011&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimekuwa nikisita sana kutoa maoni yangu katika mjadala huu kutokana na kutambua kuwa wengi wetu tumekuwa tukiongozwa na mihemuko na ushabiki zaidi kuliko uhalisia wa mambo katika kuendeleza majadiliano ama malumano yetu. Lakini leo naomba nijitoe muhanga kusema kile ambacho naamini kinapaswa kusemwa kabla ya kujikuta kuwa tumefikia mahala pabaya zaidi kusipokuwa na kurudi nyuma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kweli kabisa viongozi wa dini, wawe Mashehe, Maulamaa, Maaskofu, Mapadre na Wachungaji wana haki na wajibu wa kukemea maovu yote bila ya kuchagua wakiwa kama wanadamu na pia raia wa nchi yetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kweli kabisa kuwa katika historia ya nchi yetu, wakati wote viongozi wa dini wamekuwa wakijihusisha na masuala ya kisiasa kwa njia moja ama nyingine, iwe kushutumu ama kupigia debe kundi kundi ama suala moja na lingine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kweli kabisa viongozi wa kijamii wana umuhimu mkubwa katika kusaidiana na wae wa siasa katika kuendeleza jamii kwenye neema zaidi na kuepusha kwenye majanga yawe ya kisiasa, kijamii ama kiuchumi.&lt;br /&gt;Ni kweli kabisa kuwa Maaskofu haswa wale wa kanisa la katoliki wana nguvu kubwa ya ushawishi katika jamii yetu kuanzia katika masuala ya kijamii na hata kisiasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo ni muhimu sana kutambua kuwa haki na wajibu huu ni lazima utambue UHALISIA wa mazingira tuliyonayo kama jamii. Ni wajibu wa viongozi kuangalia hali halisi haswa ya mahusiano ya kijamii ili kuiga faida na hasara za kutekeleza haki na wajibu wao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tanzania yetu ni Tanzania tunayoamini katika umoja na amani. Hii ni nyenzo muhimu katika kufanikisha dira ya maendeleo ya nchi yetu. Watanzania kama jamii ama taifa tunaamini kuwa tunapendana na kuheshimiana. Lakini hilo halina maana kuwa watanzania wote tunaaminiana, kupendana ama kuheshimiana kama tunavyopenda kuamini na kujigamba mbele ya wengine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni ukweli ambao wengi tunajaribu kuukataa kuwa watanzania hatuaminiani. Na kutokuaminiana huko kupo katika misingi ya kisiasa, kimapato, kiasili, kikabila na hata kidini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka ya zamani ilikuwa sio kitu cha kawaida kusikia mtu akisema hawezi kumuamini mchaga. Lakini sasa hilo ni neno la kawaida kusemwa tena bila ya kificho wala haya. Miaka ya zamani ilikuwa sio kawaida kusikia muislamu akisema hamuamini mkristo ama mkristo kusema kuwa hamuamini muislamu, lakini sasa hilo ni neno la kawaida kusemwa tena bila hata kificho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yapo mengi yanayodaiwa kuwa chanzo cha hali hii ya kutokuaminiana tuliyonayo sasa. Wapo wanaoamini ni kutokana na umaskini, wapo wanaoamini ni kutokana na ujinga, wapo wanaoamini ni kutokana na siasa za ushindani usio na kifani, wapo wanaoamini kuwa ni kutokana na historia, wapo wanaoamini ni kutokana na siasa za kidunia hasa siasa za marekani na ulaya katika kupambana na kile kinachotabulika kama ugaidi wa kiislamu na wapo wanaoamini yote kwa pamoja ama sababu nyingine tofauti.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Zote zaweza kuwa ni sababu lakini cha muhimu ni kuwa uhalisia unaonyesha kuwa watanzania hatuaminiani. Na mbaya zaidi ni kuwa kutokuaminiana katika misingi ya kikabila na kidini kumekuwa kunakuwa ama kukuzwa zaidi kuliko kushughulikia kwa nia ya kupunguzwa kama sio kuondolewa kabisa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika moja ya hotuba zake, Mwalimu Nyerere aliwahi kusisitiza kuwa ingawa nchi yetu inajengwa katika misingi ya kutokuwa na ukabila, udini ama ubaguzi wa aina yeyote ile, si kweli kuwa watanzania sio wabaguzi. Aliendelea kudai kuwa utakuta wengie tunajigamba kuwa tunachukia udini ama ukabila lakini tukiminya kidogo tunatoka mapovu ya udini na ukabila. Na ndio maana UTANZANIA wetu ukajengwa kwa misingi ya kupiga vita ubaguzi wa aina yoyote ile kwa sababu uo na ni hatari kwa taifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mtizamo huu unasisitiza ule mtizamo ambao yawezekana hakuandikwa katika sheria zetu lakini ulikuwepo miongoni mwa fikira za utanzania wetu kuwa si BUSARA kuchanganya dini na siasa. Hii ni busara ambayo inatambua haki na wajibu wa viongozi wa dini zetu kushiriki katika kupiga vita maovu ya aina zote lakini pia inatambua umuhimu wa kuepuka athari za kufanya hivyo kutokana na hali halisi ya jamii yetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wote tunakumbuka ni jinsi gani viongozi wa kisiasa na kidini walivyokuwa mstari wa mbele kusisitiza BUSARA hii katika miaka ya tisini ambako kulikuwa na vuguvugu kubwa la viongozi wa dini ya kiislamu kutoa matamko ya kisiasa. Wengine ambao leo hii tunajaribu kuhalalisha hilo ndio tuliokuwa mstari wa mbele kulaani vitendo vya mashehe hao wakati ule.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapo ambao wanatumia matamshi ama uungwaji mkono wa wazi wa Askofu Kilaini katika ugombea wa Rais Kikwete mwaka 2005. Lakini wanaacha kusema ni jinsi gani viongozi wenzake wengineo ambao walilaani kitendo chake hicho na kumpelekea kupunguziwa madaraka yake kama ilivyo sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Moja ambalo wengi wanashindwa kung'amua ni kutambua mchango mkubwa wa kujenga maelewano na kupunguza kutoakuaminiana kulikowahi kufanywa na kiongozi huyo miaka ile. Wengi tunashindwa kufikiria tamko lake lile katika upana wake na ni jinsi gani tamko kama lile kutoka kwa kiongozi mkubwa wa kanisa la katoliki kumpigia debe mgomba urais muislamu linavyoweza kujenga na sio kubomoa kama endapo lingekuwa ni tofauti na lile.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wengi hawajui ama wameshasahau nini kilichowapata baadhi ya mashehe ambao wamekuwa mstari wa mbele kusifia uongozi wa Mwalimu Nyerere ambaye kwa baadhi ya waislamu yeye anawakilisha chanzo kikuu cha madhila yote ambayo wanaamini wanayapata kutokana tu kuwa wao waislamu. Lakini wengine tunatambua umuhimu wa mitazamo chanya ya baadhi ya viongozi wa kiislamu kwa Baba wa Tafa sio tu kwa kuendeleza misingi aliyotuachia lakini hata kupunguza hali ya kutokuaminiana miongoni mwa wanajamii wa dini zetu mbili kubwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati wengi wa waislamu wakitambua mapungufu mengi yaliyopo katika serikali ya Rais Kikwete na chama chake ni ukweli usiofichika kuwa kuna mtazamo unaolingana miongoni mwa waislamu walio wengi kuhusiana na matamshi ama makaripio yasiyoisha kutoka kwa viongozi wa dini ya kikristo ambayo wanaamini yanamlenga zaidi Rais Kikwete kuliko utashi wa kupiga vita ufisadi, ombwe la uongozi ama haki na demokrasia. Mtizamo huo ni ule wa kutokuamini nia ya dhati ya makaripio hayo.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Ni ukweli ambao wengi tunapaswa kuutambua kuwa mtizamo kama huo hapo mwanzo ulikuwa miongoni mwa wale ambao wengi tungependa kuwatambua kama SIASA KALI/ EXTREMISTS ambao wapo katika pando zote za dini zetu, hivi sasa ni mtazamo wa wengi ama MAINSTREAM feelings. Huo ni ukweli ambao wanaoshabikia hali iliyojijenga katika miaka karibia minne iliyopita wanapaswa kutambua na kupima kama ni busara viongozi wa dini wawe waislamu ama wakristo wanapaswa kuendelea kuachwa ama hata kushabikiwa pale wanapotoa matamshi yenye kuonekana kama yana malengo ya kisiasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yawezekana kabisa hali hii ya viongozi wa kidini kuwa mstari wa mbele kutoa matamko ya kisiasa yakawa yanaendana kabisa na matakwa na nia njema kabisa miongoni mwa watanzania kuona kuwa taifa letu linaepushwa na wingi zito za madhila ya ufisadi linalotanda, lakini pia kama raia makini ni muhimu kupima kama msaada huo unazidi umuhimu wa BUSARA ya viongozi wa kidini kutofanya hivyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kuna watu wa mtazamo kuwa chanzo cha hali ya kutokuaminiana kati ya watanzania ama makundi ya kidini nchini ni viongozi wetu wa dini. Mtazamo wangu ni kuwa katika suala la kutokuaminiana viongozi wa dini wana dhambi ya kuchochea na kutofanya juhudi za kutosha kuondoa hali hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mzizi wa hali hii ni jamii zetu kuanzia ngazi za familia. Wengi wetu tunakuzwa katika hali ya kuaminishwa kuwa dini zetu ni nzuri na za kweli sio kwa mafanikio yake bali kwa kulinganisha na "ubaya" wa dini zingine. Hali hii hutoka katika familia hadi katika mfumo mzima wa kijamii ukiwemo mfumo wa elimu yetu. Na hata tunapokuwa wakubwa hali hii tunakutana nayo mitaani na vijiweni. Inapofika katika ngazi ya makazini na nafasi za kiuchumi na kisiasa ndio hali inakuwa mbaya zaidi. Tatizo linakuwa zaidi pale viongozi wetu wa kidini wanapoamua kuchagua makundi ya kisiasa kama nyenzo za kulinda, kutetea ama kuhakisha maslahi yao binafsi na pia makundi yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa unapokuta tunakuwa mfumo hovyo wa kisiasa unao hodhiwa na wanasiasa wajanjawajanja na wenye tamaa isiyo na kifani, ndipo mchanyato huo unapokuwa mkubwa na kupelekea hali hii ya kutukuaminiana kugeuka kuwa hali ya kuchukiana kama ambavyo inajijenga sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naamini kuwa wanasiasa na wanaharakati kama watakuwa tayari kuwajibika zaidi na kwa umakini zaidi wanaweza kabisa kufanikisha kile ambacho viongozi wa kidini wanachojaribu kukifanikisha ama kuzuia. Ni wazi kuwa kukaa pembeni kwa viongozi wa kidini kutotumia haki yao ama kutotekeleza wajibu wao wa kukemea maovu kwa style ya makaripio ya wazi ama matamshi ya majukwaani, kutaweza kujenga zaidi kuliko kubomoa kama mbavyo hali inavyoelekea hivi sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanasiasa, wanaharakati na raia makini wana wajibu wa kutimiza wajibu wao ipasavyo ili kuhakikisha kuwa viongozi wetu wa kidini wanatilia maanani uhalisia wa mazingira ya kisiasa na kijamii tuliyonayo kama taifa ambayo ukweli yanataka yanataka subira zaidi, busara zaidi na uvumilivu wa hali ya juu kuliko hali ilivyo sasa.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-384075715671495282?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/384075715671495282/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=384075715671495282' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/384075715671495282'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/384075715671495282'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2011/02/siasa-zetu-nguvu-za-maaskofu-na.html' title='Siasa zetu, Nguvu za Maaskofu na Mahusiano ya jamii zetu'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-7948699664114851368</id><published>2010-08-09T08:27:00.000-07:00</published><updated>2010-08-09T08:29:36.653-07:00</updated><title type='text'>Tanzania: Beyond sectarian interests</title><content type='html'>Tanzania: Beyond sectarian interests&lt;br /&gt;A PAPER BY PROF. HAROUB OTHMAN&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;By Haroub Othman &lt;br /&gt;No-one knows whether the 1964 union between Zanzibar and Tanganyika was dictated by cold war considerations first, with pan-African ideals of unity playing second fiddle to ideology and personal survival, writes Haroub Othman. But what is clear, Othman argues, is that despite Tanzania’s controversial history, the union brought peace and stability to the region, in contrast with the secessionism and violence seen elsewhere. While corrective measures – supported by the people – are required to ensure that it is fit for purpose, the union is a better option than breaking into a federal structure with Kenya and Uganda, says Othman.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Since the 1920s the countries of East Africa, namely Kenya, Tanganyika, Uganda and Zanzibar, had developed common services and joint institutions. Matters such as posts and telecommunications, harbours, railways and currency were run jointly. There was also a body to coordinate the development of Kiswahili. This, no doubt, was easy in view of the fact that all the four countries were neighbours and under one colonial power. The white settlers in Kenya had at one time pressed the British government for a federation of the East African countries on the lines of that of Central Africa. But people in Tanganyika and Uganda feared that if that was to happen it would throw their countries into the hands of white supremacists in Kenya, in the same way that the peoples of Central Africa found themselves under the white supremacists of Southern Rhodesia at the time of the Central African Federation. And so this idea was opposed at the time. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;But as the countries were approaching independence and because of the close cooperation among the nationalist organisations, the idea of federation re-emerged. Nyerere, in a statement made in Addis Ababa when Tanganyika’s independence was imminent, said that he was prepared to delay his country’s independence if the four countries of East Africa could come to independence at the same time and form a federation. But with independence each country retreated into its own national shell, and what was agreed was the formation of the East African Common Services Organisation that later in December 1967 was transformed into the East African Community. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;When, therefore on 26 April, 1964, the People’s Republic of Zanzibar and the Republic of Tanganyika announced that they had merged to form a union, the international community felt that Zanzibar and Tanganyika had succeeded where the four East African countries together had failed. But was it the ideals of Pan-Africanism that brought Zanzibar and Tanganyika together? Was the union the result of an African initiative or was it propelled by cold war rivalry? The circumstances in which the union was formed raised a lot of questions, many of which are still unanswered, and some have been at the centre of continuing debates and controversies in Tanzania in the last twenty years. Were the fears of ZNP (Zanzibar Nationalist Party) that Zanzibar would be ‘taken over’ by Tanganyika had been proven true? In later years, the union was to haunt the Zanzibar politicians for a long time, with each of them playing the ‘union card’ either for legitimacy on the mainland or for support at home. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nyerere stated that he casually proposed the idea of the union to Karume when the latter visited him to discuss the fate of John Okello. According to Nyerere, Karume immediately agreed to the idea and suggested that Nyerere should be the president of such a union. In a New Year message to the nation on 2 January 1965, Nyerere implied that even if the ASP (Afro-Shirazi Party) had come into power through constitutional means and not as a result of a revolution, the union would still have taken place. But Amrit Wilson’s research has revealed that there was a very strong Western pressure, especially from the United States, for the Zanzibar revolution to be contained because it was felt that it held the threat of the spread of communism in the East African region. The Untied States, Britain and the then West Germany, which Tanganyika was heavily dependent on at the time, viewed the revolutionary government in Zanzibar as either a surrogate of the communist powers or dancing to their tune. The international press had already started to characterise Zanzibar as the ‘Cuba of Africa’, though to be fair to Duggan, he had referred to Zanzibar as ‘Tanganyika’s Cuba’ far back in July 1963 when he had interviewed Nyerere in Washington during the latter’s state visit to the US. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;In a cable message to US embassies in Dar es Salaam, Nairobi and Kampala, the US Secretary of State Dean Rusk instructed his diplomats to urge Nyerere, Kenyatta and Obote to explain to Karume the dangers involved in his dependence on Babu and: &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;‘The danger Babu represents… to the security of Zanzibar and East Africa generally… they should recognise here that the big problem is that Karume himself has great confidence in and dependence on Babu… also that Nyerere has said that Karume needs Babu who, despite his background, can and must be worked with. Kenyatta and Joseph Murumbi on the other hand appear to regard Babu as undesirable and the chief threat to Karume. Would it be useful to raise with Nyerere, despite his previous objection, the idea of a Zanzibar-Tanganyika Federation as a possible way of strengthening Karume and reducing Babu’s influence? Such action at this time may also help Nyerere’s own position.’ &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;In an interview with Amrit Wilson in 1986, Frank Carlucci, the US consul in Zanzibar at the time of the union who was later thrown out of Zanzibar because of CIA (Central Intelligence Agency) activities (and who later rose to become the director of CIA and US secretary of state for defence), confessed that there was United States’ pressure on Nyerere. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Susan Crouch in her book Western Responses to Tanzanian Socialism 1967-1983 reveals that: &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;‘To this end the American Central Intelligence Agency was active in trying to create the conditions for union, fanning antagonisms among Zanzibar’s revolutionary leaders, and creating a fear of Zanzibar as a communist threat among East African leaders.’ &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Was the union then, as is indicated in US state department papers, dictated by cold war considerations first and the questions of pan-African ideals of unity were secondary to ideological factors and questions of personal survival? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;It has also been suggested that Karume wanted a union with Tanganyika as a means of warding off his marxist and left wing colleagues. What seems to be the case is that after the electoral defeat of July 1963, Karume’s leadership within the ASP parliamentary group was shaky. There was a schism in it, with Karume being challenged by Othman Shariff, and some of the party’s MPs calling for a government of national unity that would bring together in government all the political parties in parliament. After the revolution, Umma Party radical elements in the government (Babu, Khamis Abdalla Ameir, Ali Sultan Issa, Ali Mahfoudh, Salim Rashid, Badawi Qullatein, etc) were forging links with the ASP leftists (Abdallah Kassim Hanga. Abdulazizi Ali Twala, Hassan Nassor Moyo, etc.), and this might have scared Karume and other moderate elements within the regime. At the same time, the radical way in which the revolution was surging ahead might have alarmed the regime in Dar es Salaam. It should not be forgotten that within days of the revolution in Zanzibar, an army mutiny took place in Tanganyika (later repeated in Kenya and Uganda); and even though we know now that there was no link between the revolution and those mutinies, it was difficult to see it that way at the time. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;As a result of the army mutiny in Dar es Salaam, Tabora and Nachingwea, there was virtually no government in Tanganyika for three days, anarchy prevailed, and Nyerere was forced to request British military intervention to bring the country back to normalcy.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;The West, particularly the Untied States, perceived developments in Zanzibar in the context of East-West rivalry, and given the leftist credentials of the Umma Party and some of the ASP leaders that were prominent in the revolutionary council, it was assumed that a Cuba-type situation was evolving. The best way of averting it, short of direct military intervention a la Playa Giron (though this was thought of and preparations made), was to try an ‘African initiative’. And it worked. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;QUESTIONS OF LEGITIMACY &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Many questions continued to be raised regarding the legal basis of the union: Whether the two presidents on their own had the powers to sign such a union agreement; why the Zanzibar’s attorney-general, as the principal legal advisor to the government, was not consulted; why there was no referendum; and whether in joining such a union, Zanzibar was not in fact ‘swallowed’ and ‘annexed’ by Tanganyika. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Discussions on the union were conducted very secretively. From the archival materials and the statements of those who were in the ‘corridors of power’ at the time, it would appear that not many people in the Tanganyika government or the Zanzibar Revolutionary Council knew what was happening. Apart from Nyerere and Karume, the only other people who might have been privy to those discussions were Rashidi Kawawa, Oscar Kambona, Job Lusinde, Abdallah Kassim Hanga, Abdul-Aziz Ali Twala and Salim Rashidi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;When these discussions were at an advanced stage, Nyerere is said to have called in his attorney-general at the time, British expert Roland Brown, and asked him to draft a union agreement without anybody knowing. In the case of Zanzibar, the attorney-general, Wolf Dourado, is said to have been sent on a one-week ‘leave’ and instead a Ugandan lawyer, Dan Nabudere (according to his own account which was corroborated by Babu), was brought in to advise Karume on the draft submitted by Tanganyika. Both Brown and Nabudere were present in the Karume-Nyerere discussions. One can speculate that one reason why Dourado was not involved was because he was ‘inherited’ from the previous ZNP/ZPPP (Zanzibar Nationalist Party-Zanzibar and Pemba People's Party) regime and the revolutionary government was hesitant to involve him in such a sensitive matter. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Under both the 1962 Republic of Tanganyika constitution and the Zanzibar presidential decree No.5 quoted above, the two presidents had the powers to enter into international agreements on behalf of their governments. What is also important is that the union agreement was ratified by both the Tanganyika parliament and the Zanzibar Revolutionary Council. Contrary to what some writers have said, the Nyalali Commission was satisfied that the Revolutionary Council met to ratify the Articles of Union. Both Abdulrahman Babu and Khamis Abdallah Ameir, the two former Umma party leaders who were in the Revolutionary Council at the time, have confirmed that the matter was discussed in the council, and while there were reservations on the part of some members, these were ‘quashed’ by Abdallah Kassim Hanga who made an emotional intervention to support the union. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Once the Articles of Union had been ratified by the two legislative bodies in Tanganyika and Zanzibar, there was no further requirement in law to make them enforceable. The question of referendum would not have arisen because under the Commonwealth legal tradition, in which the two countries were brought up, the notion of a referendum was unknown. The referendum was introduced as a legal requirement under British law in the 1970s during the heated debate in the United Kingdom on the question of its entry into the European Economic Community. To have also expected the Zanzibar revolutionary government to call a referendum on the union, four months after it came into power through unconstitutional means, was like expecting the French revolutionaries of 1789 to have invited King Louis XVI for dinner after they had overthrown him. Should ASP have conducted a referendum to ask Zanzibaris whether or not to stage a revolution? In law, therefore, the Union Agreement, as both Prof Issa Shivji and Dr Kabudi have pointed out, is valid. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;ARTICLES OF UNION: 1 + 1 = 3 &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;The Union Agreement, signed by Karume and Nyerere in Zanzibar on 22 April 1964, is known as the Articles of Union. When this agreement was announced the following day, many people inside the two countries, and outside too, were taken by surprise. The strong feeling was that the West had won in their intention to containing the Zanzibar revolution; in fact there were military preparations by both Britain and the United States in case there was a violent reaction in Zanzibar against the union. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;What the Tanganyika leadership wanted at the time was to play down the whole event. In a cable message of 23 April 1964 to the US secretary of state, the US ambassador in Dar es Salaam, William Leonhart, informed: &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;‘Mbwambo, chief protocol, has just telephoned a personal request… that, to the maximum extent, any US public statements on Tangovernment –Zanzibar union be avoided. Situation over the next few days in Zanzibar could be very critical and both the Soviet and Chinese reaction is undetermined.’ &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;In an address later to the National Assembly requesting the ratification of the Articles of Union, Nyerere insisted that the move was inspired by the ideals for an African unity. ‘Unity in our continent does not have to come via Moscow or Washington’, he insisted. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;The Articles of Union have been given different interpretations and characterised as federal, quasi-federal, an interim arrangement towards one government, etc. Some have seen the union as similar to the relationship between the United Kingdom and Northern Ireland. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Those who were close to the scene at the time also differ as to what type of relationship it is. The US ambassador in Dar es Salaam, in a cable message to his government on 22 April 1964, the day the Articles of Union were signed by Karume and Nyerere, stated: &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;‘Like the relationship between Northern Ireland and Britain, the union of Zanzibar and Tanganyika gave the island limited regional administrative autonomy… but ensured overall power… was held by the centre at Dar es Salaam’. But Frank Calucci, reporting from Zanzibar the next day, said that Karume was ‘still under the impression that he is agreeing to a federation of two autonomous states, not a centralised union envisaged under the present articles’. Attwood, the U.S. Ambassador in Kenya at the time, says he was informed by Dustan Omari, Nyerere’s permanent secretary then, ‘that the major power would rest in the centre… but that Zanzibar would retain its own internal governmental affairs’. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;While I have difficulty in accepting some of the assertions of some of the writers on the character of the union for reasons that I will advance later, I would only want to agree with the notion that the Articles of Union are the Grundnorm, the fundamental law of the United Republic, on which the Constitutions of Tanzania and Zanzibar, and other laws, have to be based and from which they derive their legitimacy. Like any supreme law in any other legal system, no other law or constitutional act can be in conflict with it. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Articles of Union provide for matters that would be under the union arrangement. From the original 11 items in 1964, the list has now expanded to 23. Some people question the validity of such an expansion, though one must admit that there was nothing that was added into the list unconstitutionally. The Articles of Union also provide for the existence of two governments: One for the whole United Republic for all union matters and for non-union matters in Tanganyika, which, under the 1977 Union Constitution is referred to as Tanzania mainland, and one for Zanzibar in all matters that are non-Union. According to Nyerere, Karume wanted a total union, but he (Nyerere) cautioned against it, saying that such a move might be construed by Zanzibaris and others as meaning that Zanzibar had been swallowed up, annexed, incorporated into or taken over by Tanganyika. He insisted that Zanzibar’s identity must be maintained. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;There is no way one can construe the ‘Article of Union’ as a basis for a federal set-up. Nor can they be seen as an interim arrangement towards a one government. They intended to create a single state with two authorities, but with one of those authorities having a limited geographical jurisdiction. The intention was to retain the identity of the smaller unit. By this event, Tanganyika has not been lost; in fact it has been enlarged. Even if it is accepted that the union was a Western conspiracy against the Zanzibar revolution, the effect of the intention was to deny Zanzibar the capacity to be an international actor, not to interfere with what was happening inside the country. To be able to change the internal course of events would have entailed changing the regime. What might have confounded some of the law experts looking at the relationship between Zanzibar and mainland Tanzania was the fact that no such example existed in the Anglo-Saxon legal system. The closest they could think of then was that of the United Kingdom and Northern Ireland. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;CONSOLIDATING THE UNION: POPULAR APPROVAL &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;At the time of the Union Zanzibar and Tanganyika were ruled by different political parties, ASP and TANU respectively. The Articles of Union did not require the formation of a single political party for the whole United Republic. Thus in the period 1964-1977 each party operated within its own geographical area, though at the approach of every general election, the two parties held a joint congress where they nominated a join presidential candidate for the elections. Only in 1977, after a national survey of members of both parties, did the two parties merge to form the Chama cha Mapinduzi (CCM) with authority over the whole country. But why did Zanzibaris agree to such a merger? Nyerere had always expressed surprise when recalling the radiant faces he saw and the jovial mood of the Zanzibaris the day CCM was proclaimed at the Amaan stadium in Zanzibar. The fact is that Zanzibaris were celebrating not only the birth of CCM but also the demise of ASP. By that time the general feeling in the islands was that the ASP had outlived its usefulness. The revolution which it had championed had stooped so low as to devour its own sons: Most of the leaders were busy amassing wealth; prison and death were the only options open to political dissent; and political thuggery was a virtue. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;One matter that was added in 1984 to the list of union items was that of national security. This happened at the time when Ali Hassan Mwinyi was president and Seif Shariff Hamad the chief minister of Zanzibar in 1984-85, commonly known as the Third Phase government. Not having much confidence in the security personnel they inherited, who might have had personal allegiance to Jumbe and Seif Bakari, the new administration sought the extension of the National Security Act of the mainland to Zanzibar. In that case it was possible to transfer the security personnel in Zanzibar to the mainland and vice versa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;So from the above one can see the following: First, Zanzibaris wanted a merger of the parties, and for the united party to have authority all over the country, in the hope that it would rescue them from a regime that was no longer able to inspire confidence and instil enthusiasm; and second, a ‘consolidation’ of the union in this regard was necessary for one faction of the leadership to ward off any possible challenge by the other. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;The long-term effect of the parties’ merger was to have matters that were entirely within Zanzibar’s jurisdiction, and that were not union matters, decided by a pan-territorial political party where Zanzibari representation was not decisive. This became clear in 1984 when Aboud Jumbe was forced to resign as Zanzibar president: It was the party’s NEC which appointed Ali Hassan Mwinyi as an interim president and later nominated him for election as the president of Zanzibar. Since NEC’s Zanzibari membership is no more than a third of the total, this means therefore that a Zanzibar president could be chosen by a forum, which is predominantly non-Zanzibari. And this was further evidenced with the nomination by CCM’s NEC of the present president of Zanzibar. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;A number of other measures were taken to consolidate the union, particularly in the constitutional realm. A permanent constitution was put in place in 1977 instead of an interim one that had been in existence since 1964. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;ZANZIBAR’S IDENTITY IN THE UNION &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;In the Articles of Union, Zanzibar is allowed to retain its autonomy and pursue its own policies in all matters other than those stipulated as Union matters. In this case, the power to decide is left to the Zanzibar organs such as the house of representatives, the revolutionary council and the president of Zanzibar and chairman of the revolutionary council. The union constitution stipulates that constitutional amendments require the approval of two-thirds of Zanzibaris sitting in the union parliament and the same proportion of mainlanders. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;In order to avoid a clash in the legislative functions of the two sides of the union, it has been provided that if the house of representatives enacts any law which should be under the jurisdiction of the union parliament that law will be null and void, and also if the union parliament enacts a law on any matter under the jurisdiction of the house of representatives that law will be null and void.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;The constitution also provides for effective Zanzibari representation in the union parliament. It also guarantees a separate judiciary system for Zanzibar which has jurisdiction over Zanzibar alone. Even though the court of appeal of the United Republic is a union organ, it has no power to decide on a case involving a dispute between the union government and the Zanzibar revolutionary government. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;However one might view the circumstances that made Zanzibar merge with Tanganyika in 1964, the fact of the matter is that Zanzibar was not annexed or forcefully incorporated. It agreed on the union out of its own free will and as a result of decisions made by its own organs. The argument that within the union Tanganyika has lost its identity has no basis. If anything it has enlarged its territory. It is Zanzibar’s autonomy and identity that must be maintained lest, as Nyerere himself has pointed out several times, an impression is created that the larger and more populous Tanganyika has swallowed Zanzibar. Such a situation is not new even in the most centralised states. In China, despite the fact that the country has a centralised authority and no federal traces of any kind, yet because of certain historical, political or cultural reasons, certain areas are conferred autonomy, and are constitutionally given the status of autonomous regions. As will be pointed out later there are entities in present-day Europe that enjoy full autonomy within one state. To entertain the thought that the Articles of Union are a temporary arrangement, and that ultimately the intention should be to create one government is to manifest ‘big brother chauvinism’ &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;DEBATES ON THE UNION: A POLLUTED ATMOSPHERE &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;In 1983/84 and 1990/92 extensive political and constitutional debates took place in the country that deeply probed the question of the union. The debates of 1983/84 resulted in major amendments to the 1977 union constitution and the formulation of a new Zanzibar constitution in 1984. But they also resulted in the forced resignation of Aboud Jumbe from all his state and party positions, the sacking of a Zanzibar chief minister and the serious warning given by the ruling party to a number of prominent Zanzibar figures. The debates of the 1990/92 period resulted in the Nyalali Commission making major recommendations on the structure of the Union. In between the two periods also another Zanzibar chief minister was sacked, and several leading Zanzibar politicians were dismissed form the ruling party. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;As stated above, the question of Zanzibar being ‘sold’ to the mainland was an issue in pre-revolutionary Zanzibar. And if one remembers that the political parties were almost evenly divided, then one can assume that almost half of the Zanzibar population was already biased against the mainland even before the union. The post-revolution politics in the islands did not help matters much. Karume went into a union to save himself from his marxist and left-wing colleagues; and since Jumbe was not considered to be the ‘heir apparent’ before Karume’s assassination in 1972, he was not thought of as the natural successor when he took over. It has been speculated that the revolutionary council had Colonel Seif Bakari in mind, but Nyerere advised that since Karume was killed by an army officer, Seif Bakari taking over might be construed as a military coup. Jumbe, feeling that he had not much support within the revolutionary council, depended very much on Nyerere’s and mainland’s support. It is no wonder then that it was during his presidency that much of the consolidation of the union took place, with the most items added to the union list. It is significant too that the merger of the parties took place then. But this dependency on the mainland was costing him much popular support at home. Either as a way of outflanking his opponents or because of genuine problems he found in the union (after all he was for a long time a minister for union affairs before he became president of Zanzibar), he first raised the question of restructuring the union in a speech seven years before the 1983/84 debates. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Other politicians in Zanzibar too have used the mainland as a trump card either to crush their opponents or to climb the political ladder. Seif Shariff Hamad, Khatib Hassan, Shaaban Mloo and others accused Jumbe in 1984 of planning to break up the union, and thus forced Jumbe to resign from his political posts then. They in turn faced the same accusation from their opponents in 1988 and were dismissed from the party. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;The issues that were raised in both the 1983/84 and 1990/92 debates centred on the following: &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;1. Whether the Articles of Union of 1964 provided for a federation, that is three governments (one of Tanganyika, the other of Zanzibar, and a third a federal one) or only two governments as presently existing; &lt;br /&gt;2. As the union government is also the government for the mainland in non-union matters, does this not give the impression that mainland is the union? &lt;br /&gt;3. Does Zanzibar get a fair share in the distribution of benefits coming form the union? &lt;br /&gt;4. Is Zanzibar well represented in the diplomatic service? &lt;br /&gt;5. Does it get a fair share of foreign aid coming to Tanzania? &lt;br /&gt;6. Since the people of Zanzibar were not consulted at the time of the formation of the union, should there not be a referendum now to ascertain whether the people wanted the union or not? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Most of these questions, as can be seen, were coming from Zanzibar, and what surprised many people at the time of the 1983/84 debate, was that they were being aired in the state-owned-and-controlled official mass media. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;No such strong feelings were voiced on the mainland during the debates. Many people who made submissions to the Nyalali Commission said hardly anything about the system of governments that the union should have. It was only after the opening up of the political system and the establishment of more political parties that one began hearing very strong views coming form the mainland on the question of the Union; some of those going even further than anybody in Zanzibar had ever contemplated. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;THE NYALALI COMMISSION: AGREED TO DISAGREE &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;One of the major recommendations of the Nyalali Commission was for the replacement of the present union set-up with a federal one. This was one of the areas that bought about a very heated debate within the commission and which necessitated members of the commission having to vote. Later those who were opposed to the federal idea had to append their own dissenting opinion to the main report to explain their position. But the division in the commission on this issue almost came to a mainland/Zanzibar division. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Of the 11 members from Zanzibar, seven wanted the present union set-up, with some major changes, to remain; three wanted a federal and one was undecided. Of the same number from the Mainland, nine wanted a federal set-up and two wanted the present arrangement to continue. What is important is that both sides agreed that there were problems within the union. Even though at the time the complaints form the mainland were not so loud compared to Zanzibar, it would have been wise if those complaints were addressed and resolved. The majority of members of the commission felt that in a federal set-up, both Tanganyika and Zanzibar would retain their identity, federal areas would be clearly defined and the responsibilities of each would be understood, and the federal entity would be distinct from the national ones. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Those holding the minority opinion, on the other hand, were of the view that there was nothing in the Articles of Union to suggest that their framers had a federal set-up in mind; that a federation would be a step backward and might be a prelude to the dissolution of the union; that corrective measures could be taken, if there is political will, which would define union matters, list union institutions and apportion the responsibility of each side on those matters. Examples were provided from the two Scandinavian countries of Denmark and Finland where entities (Faroe Islands, Aaland Islands and Greenland) have full autonomy in a number of areas that they exercise within a non-federal state. The dissenting opinion in the Nyalali Report pointed out: &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;‘Greenland and Faroe Islands, both of which are part of Denmark, have full autonomy in many matters. For example, a parliament that is not subject to interference form the central government of Denmark, and all political and economic matters agreed upon and even in international relations. The islands of Faroe have their own flag hoisted in all government buildings and on ships registered in Faroe islands. Also Faroe Islands authority issues passports; &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Denmark had agreed to join the European Economic Community. So did Greenland. But later, Greenland withdrew from the Community. Therefore, all EEC agreements and conditionality accepted in Denmark did not apply in Greenland. Similarly, the Islands of Faroe are not a member of the EU. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;In regard to Finland, the islands of Aaland have their own parliament and government. The islands of Aaland also have their own ‘identity’ for persons born in the islands and who have not lived abroad consecutively for five years or more. The islands have their own flag, issue their own stamps and its citizens are not subject to military service. The islands of Aaland are a demilitarised zone. The Central Bank of Finland must consult the government of Aaland before it takes measures that might harm the economy of Aaland. This, despite the fact that they share a common currency; &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;The islands of Aaland, as is the case for Greenland and Faroe, are, on their own right, represented in the Nordic Council that consists of Denmark, Finland, Sweden, Norway and Iceland.’ &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;WHITHER THE UNION? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;As pointed out above, there have been historical links between Zanzibar and Tanganyika long before the coming of the colonialists in East Africa; and colonialism did not in fact stop such interactions from continuing. During the struggle for national independence, the two main political parties in the two countries cooperated – though there is nothing to suggest that the two parties were thinking of merging into a union of this kind after they came into power. What they had in mind was to form a federation with Kenya and Uganda. Until the elections of July 1963, ASP still thought that it would win power through the electoral process; and it would appear that their main supporters, TANU (Tanganyika African National Union), thought likewise. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Now the union is a fact. Despite a lot of problems, it has brought stability and peace in the region. It is difficult to speculate what would have happened to the Zanzibar revolution without the union: Whether Zanzibar would have advanced faster or whether a counter-revolutionary force would have taken over and embellished a dictatorship worse than anything the islands have actually experienced especially during the first phase government. What is clear though is that the union has brought the two peoples much closer together. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;I do not believe that the unity of the two peoples can be strengthened by restructuring the present set-up into a federation. I see movement from the present set-up to a federation as a step towards the dismemberment of the union; and I do not think that that is to the short or long term benefit of the people of Tanzania. The present problems can be resolved if there is a strong political will on the part of our political class and if the people are told the truth about those problems. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Only when corrective measures are taken, would it be possible to sustain and strengthen the union. Otherwise if the difficulties inherent in the Articles of Union and the problems arising from implementation are only emphasised and not resolved, the tendency would be towards the withering away of the union. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;In this era of multi-parties and openness, it is even more important that matters are discussed and solutions founded on popular will. Of all the political parties that have been established since the abolition of the one-party system, only one, the Democratic Party led by Reverend Mtikila, has come out strongly against the union and called for its dissolution. Others are prevaricating between ‘referendum’, ‘federation’ and modifications within the present set-up. The CCM and its governments which seemed earlier on to strongly accept the dissenting opinion in the Nyalali Report, now seems to be torn apart, with a strong group calling for a federal set-up. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;The national language, the ethics of equality and human dignity, and the Union of Tanganyika and Zanzibar are what overcame the ethnic hatred, religious bigotry, regional parochialism and national differences and forged national cohesion and unity. It is these that have made Tanzania an example in a continent beset with secessionism, ethnic violence and religious pogroms. One hopes that there is capacity, honesty and patriotism within Tanzania that will look beyond the sectarian interests. The alternative is too horrendous to contemplate. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;*A full version of this paper was published in 1993 by the Danish Centre for Development Research. It also appeared in the book Zanzibar and the Union Question, edited by Prof Chris Peter and Professor Haroub Othman and published by the Zanzibar Legal Services Centre. &lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-7948699664114851368?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/7948699664114851368/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=7948699664114851368' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/7948699664114851368'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/7948699664114851368'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2010/08/tanzania-beyond-sectarian-interests.html' title='Tanzania: Beyond sectarian interests'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-4181787435749142339</id><published>2010-05-12T23:33:00.000-07:00</published><updated>2010-05-13T23:49:29.706-07:00</updated><title type='text'>Mwalimu Nyerere anapogeuzwa mtaji wa ufisadi endelevu</title><content type='html'>Kama kuna mhimili pekee wa utaifa wetu ambao hadi sasa umeweza kuhimili mikiki mikiki lukuki yenye nia ya kuubomoa na kuufutilia mbali katika historia ya nchi yetu basi ni jina la Mwalimu Nyerere. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka kumi baada ya Mwalimu kuondoka duniani bado jina la Mwalimu limekuwa kama nguzo kuu ambayo watanzania kwa pamoja wamekuwa wakiendelea kutegemea kama turufu pekee ya kulinda, kutetea na zaidi kuhalalisha maoni, matakwa, mitizamo na hata matumaini yao. Jina la Mwalimu Nyerere limeendelea kuwa turufu pekee ya watu mbalimbali katika ulingo wa kisiasa, kiuchumi na hata kijamii kuhalalisha maoni, mitizamo na hata maslahi yao. Jina la Mwalimu Nyerere limeendelea kuwa lulu ya wengi hata kufikia wengine kudai kuwa na hati miliki ya matumizi yake na kuwanyima wengine haki hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati nchi yetu ilipokuwa ikilazimika kufuata mkumbo wa kuanzisha mfumo wa demokrasia ya vyama vingi, Mwalimu Nyerere aliweza kujitokeza kuwa sehemu muhimu ya mabadiliko hayo. Mengi yemesemwa kuhusu nini alisema na alikuwa na maana gani. Mojawapo ni lile la kuwa upinzani imara utatoka ndani ya CCM. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Imekuwa ni kawaida siku hizi kusikia watanzania wengi wakilalama, kusema na hata kupayuka kuwa ili nchi yetu iwe na demokrasia imara basi ni sharti CCM imeguke na kutimiza kile wanachodai utabiri wa Mwalimu Nyerere.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwanzoni haya yalikuwa yakizungumzwa sana miongoni mwa wachache waliopo katika vyama vya upinzani. Baadae hali hii ikaanza kujitokeza zaidi miongoni mwa watanzania waliochoshwa na “maovu” ya CCM lakini hawako tayari kujiunga ama kuunga mkono na vyama vya upinzani vilivyopo wakiamini kuwa huo sio upinzani wa kuaminika na utakaoweza kutoa mbadala makini wautakao wao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika miaka ya hivi karibuni kinachoitwa utabiri wa Mwalimu Nyerere umekuwa zaidi ukizungumziwa sana na wana CCM wakiwemo viongozi waandamizi, viongozi wastaafu na hata wanachama wa kawaida.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kufuatia mparaganyiko mkubwa uliojitokeza kuanzia mkutano wa halmashauri kuu ya CCM wa mwaka 2002 na kuhalalishwa rasmi wakati wa uchaguzi wa wagombea wa CCM katika uchaguzi wa mwaka 2005 ambao matunda yake yakaanza kujitokeza rasmi na kwa uwazi zaidi ndani ya bunge hili la sasa na kusambaa pande zote za nchi. Kile kinachoitwa “Utabiri wa Mwalimu” kimegeuzwa kuwa mtaji mkubwa wa kisiasa miongoni mwa wanaCCM na hata katika vyama vingine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutokana na kugubikwa na utamaduni wa siasa chafu zenye kuendekeza rushwa na ufisadi, ubinafsi, migongano ya kimaslahi, chuki, uadui, majungu, kutokuaminiana na kukosa dira ndani ya chama hicho, watanzania wengi wamejikuta wakilazimika kukaa mkao wa kula kusubiri kutimia kwa utabiri wa Mwalimu wa kuwa upinzani imara utatokana na kumeguka kwa CCM. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwao wao ni kuwa matatizo yanayolikumba taifa letu yanatokana na sababu mbili. Moja ni migogoro ya ndani ya chama ambayo kwa maoni yao inasababishwa na baadhi ya wanachama wenye hulka ya kuthamini rushwa na ufisadi zaidi ya “maslahi ya chama na taifa” na Pili ni kukosekana kwa upinzani imara utakaoweza kukishurutisha chama cha CCM kurudi katika mstari ulionyooka na kukifanya kuwa imara kama inavyotakiwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kuwa wakati Mwalimu akitoa hicho tunachokiita utabiri wa kumeguka kwa CCM na kupatikana kwa upinzani imara nchini, alikuwa akifikiria ni jinsi gani chama chake alichokipenda na kukitumikia kwa uaminifu mkubwa kinaweza kurudi katika mstaari mnyoofu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo wengi wetu tunashindwa kuangalia mazingira na mantiki halisi yaliyompelekea Mwalimu kuamini kuwa upinzani imara utatoka ndani ya CCM. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwalimu aliamini kuwa kutokana na misingi imara aliyoiwekeza katika CCM ni wazi kuwa kitaendelea kuwa chama imara kama kitapata upinzani imara utakaowalazimu wanaCCM kujiangalia na kujisafisha ili kuendelea kutawala. Kwa hali iliyokuwepo wakati ule Mwalimu alipotoa matamshi yale ni wazi aliona mkanganyiko wa kimisingi na kiitikadi ambao ulikuwa ukichipua ndani ya chama hicho. Ni wazi kuwa Mwalimu aliposema upinzani imara alimananisha kuwa upinzani ambao utakuwa unatofautiana na CCM kimisingi, kisera na kiitikadi na sio magomvi na ushindani wa nani anafaidika zaidi na ufisadi na nani anazuiliwa kufaidika zaidi na ufisadi huo kama hali ilivyo sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mimi naamini kuwa Mwalimu hakuwa mzembe wa kimawazo wa kuamini kuwa upinzani imara utatoka CCM bila ya kutambua sehemu ya tofauti za kimisingi na kiitikadi ambazo zingelipelekea baadhi ya wanaCCM kujitoa na kuanzisha chama chao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwalimu aliongelea mgawanyiko wa CCM kwa mantiki ya kuwa kwa kuwa kulikuwa na baadhi ya wanaCCM wakiwemo viongozi wakuu wakiamini kuwa misingi, sera na itikadi ya Ujamaa na Kujitegemea imepitwa na wakati  na wangependa kuona CCM na Tanzania zinafuata misingi ya ubepari. Ni wazi hali hiyo ingepelekea chama hicho kugawanyika katika misingi hiyo na hivyo kuleta upinzani imara wenye kufuata tofauti za kimisingi, kisera na kiitikadi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tukumbuke kuwa ni wakati huohuo ndipo Mwalimu aliwahi kutamka kuwa kati ya vyama vilivyokuwepo aliamini kuwa CHADEMA ambacho kilikuwa kikijinasabisha na sera na itikadi za KIBEPARI kwa waziwazi bila ya kificho kama ilivyo kwa CCM ndicho kitaweza kuwa imara hapo mbeleni. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni vizuri tukajiuliza, Mwalimu akiwa kama mjamaa aliyekubuhu ni kwa nini hakusema kuwa NCCR ingeliweza kuwa chama makini wakati wao walikuwa wakijinasabisha na ujamaa wa mrengo wa kati lakini akasema ni CHADEMA. Iweje Mwalimu adhani kuwa CHADEMA kilichoanzishwa na mtu ambaye alimtaka ajiuzulu uwaziri wa fedha kutokana na kuonyesha nia ya kukumbatia ubepari kiwe cha kutolea mfano wa upinzani makini na sio NCCR iliyokuwa bado ikithamini chembechembe za ujamaa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vilevile tusisahau ukweli kuwa wakati hadi siku zake za mwisho Mwalimu aliendelea kuamini katika ujamaa lakini pia alishangaa rafiki yake mwaminifu Mzee Kawawa aliposema atakuwa na CCM hadi mwisho wa maisha yake. Ni wazi Mwalimu alishangaa ujasiri wa Mzee Kawawa kusema kuwa atakuwa mwanachama muaminifu wa CCM  hata kama kitaamua kukumbatia ubepari kama dalili zilivyokuwa zikianza kujionyesha wakati ule.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa Mwalimu suala la misingi na itikadi ndilo lilikuwa suala la yeye kuendelea kuwepo CCM ama kuachana nacho. Hivyohivyo alikuwa akiamini katika suala la kumeguka kwa CCM kutokana na tofauti za kimisingi na kiitikadi na kutokea kwa upinzani imara hapa nchini na si vinginevyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa ndipo ninakuja kuona kuna upotoshaji mkubwa sana wa kile kinachoitwa utabiri wa Mwalimu kuhusu upinzani imara nchini. Ninaamini kuwa upotoshaji huu unafanyika ama kwa kutokujua ama kwa makusudi kabisa ili kuendelea kumtumia Mwalimu Nyerere kuhalalisha maslahi na mikakati ya kuendeleza mfumo fisadi unaoendelea kushamiri nchini mwetu.Hawa wapo tayari kuwaaminisha Watanzania kuwa endapo wao watatoka CCM na kuanzisha ama kujiunga na chama kingine basi chama hicho ndicho kitakuwa upinzani makini. Hawa wasingependa watanzania kuwauliza na hata wao wenyewe kujiuliza maswali magumu ya kama kweli kumeguka kwa CCM kutokana na hali na sababu za hivi sasa ndio kunatosheleza kuleta upinzani imara katika mntiki ya ule alioutabiri Mwalimu Nyerere.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inatia wasiwasi zaidi kuona kuwa hivi sasa wakati tunaelekea katika uchaguzi mkuu wapo baadhi ya wanaCCM na hata wasio wana CCM wamekuwa mstari wa mbele kuendeleza upotoshaji huu kuwa mpasuko utakaotokea hapo ndio utakaoleta upinzani imara nchini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbaya zaidi inasikitisha kuona kuwa miongoni mwa vyama vya upinzania wapo ambao badala ya kutilia mkazo suala la kujenga upinzani imara wameamua kuendelea kukaa mkao wa kula kusubiri kile wakiitacho mmeguko wa CCM ili nao wafaidike na makapi ya chama tawala kufanikisha ndoto zao za kurithi mfumo fisadi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inatisha kuona ni jinsi gani kwa muda wa miezi michache sana tayari kuna zaidi ya watanzania elfu kumi ambao wanadhani tayari wamepokea mwito wa utabiri wa mwalimu wa kujenga upinzani imara kutokana na mmeguko wa CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siamini kuwa Mwalimu Nyerere alikuwa ameshindwa kufikiri kiasi cha kudhani kuwa bila ya kujali sababu na mitizamo ya hao Kimisingi, Kiitikadi na Kisera basi hao watakaotoka CCM wataweza kujenga upinzani imara aliokuwa akiufikiria yeye.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sidhani kama Mwalimu alikuwa amechoka kuifikiria Tanzania yake hadi kuamini kuwa tofauti zinazoonekana sasa zinazohusishwa na suala la rushwa na ufisadi ama ushindani wa kimakundi wenye taswira ya uhodhi wa madaraka ndani ya CCM, zinatosheleza kupelekea kupatikana kwa upinzani imara nchini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naamini kuwa wapo wengi wanaotambua kuwa utabiri wa Mwalimu Nyerere kuhusu upinzani imara ulikuwa na maana ya kuwa utatokana na kumeguka kwa CCM kwa tofauti za misingi, itikadi na sera na sio tofauti hizi tunazoziona sasa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naamini kuwa Mwalimu Nyerere aliona upinzani imara utakaotokana kuvunjika kwa CCM kutokana na kukua tofauti za kimisingi, kiitikadi na kisera ambazo zitasimamiwa kidete na kupelekea ama wahafidhina waumini wa Ujamaa kuondoka katika chama hicho na kuwaachia wajanjawajanja waumini wa Ubepari au waumini wa ukombozi wa Kibepari kuondoka katika chama hicho na kuwaacha waumini wa Imani za Kijamaa kuendeleza kile ambacho yeye alikianzisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kuwa kutokana na hali inavyokwenda sasa uwezekano ni mkubwa wa CCM kumeguka katika misingi ya wale walio mstari wa mbele katika vita ya ufisadi. Yaani wale ambao wanaona kuwa ufisadi sio tatizo kubwa ndani ya chama chao na wale ambao wanaodhani kuwa ufisadi ni mzigo mkubwa ambao chama kinapaswa kujivua ili kuweza kuendelea kulinda uhalali wa kuwa chama tawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yawezekana kuwa hili litaweza kupunguza ukiritimba wa CCM katika utawala. Lakini sidhani na wala siamini kuwa Mwalimu aliufikiria mgawanyiko wa aina hiyo ndio upinzani imara kama ambavyo wengi wanavyopotosha. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Upinzani ambao utatokana na kumeguka kwa CCM kutokana na ushindani wa kimakundi ambao umeegemea zaidi katika masuala (kama vile ufisadi na ushindani wa uhodhi wa nguvu za kiushawishi ndani ya chama) na sio kuegemea katika misingi, itikadi na sera, ni upinzani unaojengwa kwa nguzo legelege. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kuwa upinzani wa aina hiyo hautaweza kuwa imara kwani ni rahisi kujikuta yale ambayo wameyaacha huko walikotoka ili kuanzisha ama kuhamia chama kingine yataibuka tena huko walikoenda lakini zaidi hauwezi kuwa wenye kuweza kuleta suluhu la matatizo ya kitaifa yanayotukuma hivi sasa na hata huko mbeleni. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Upinzani imara ambao utakuwa na manufaa ya kwa watanzania ni ule utakaotokana na tofauti za kimisingi, kiitikadi na kisera na sio tofauti hizi za kiujanjaujanja tunazoziona sasa.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-4181787435749142339?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/4181787435749142339/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=4181787435749142339' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/4181787435749142339'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/4181787435749142339'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2010/05/mwalimu-nyerere-anapogeuzwa-mtaji-wa.html' title='Mwalimu Nyerere anapogeuzwa mtaji wa ufisadi endelevu'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-481762000284876144</id><published>2009-08-31T16:37:00.000-07:00</published><updated>2009-09-01T06:47:03.420-07:00</updated><title type='text'>WAMEBAKA NA KUDUMAZA KADEMOKRASIA KETU</title><content type='html'>August@2009&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati watanzania walio wengi wanaamka na kuonyesha utayari wa kuchukua jukumu la kuleta mabadiliko ya kweli ambayo yataliwezesha taifa letu kusonga mbele katika harakati za kujenga mfumo wa kidemokrasia nchini, ndugu zetu wa CHADEMA wameamua kubaka na kudumaza mfanikio madogo yaliyoweza kupatikana hadi hivi sasa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kifupi tukio la kumshinikiza ama kumshawishi kama ambavyo wanapenda watu wajue, kiongozi wao mahiri Zitto Kabwe kuacha kushindana kidemokrasia na Mwenyekiti wa sasa Freeman Mbowe katika kugombea nafasi ya mwenyekiti kinatafsirika kwa maneno machache sana. CHADEMA wamebaka na kudumaza harakati za demokrasia nchini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama kuna chama ambacho watanzania hasa vijana walikuwa na matumaini makubwa ya kuwaondoa katika madhila ya ukiritimba wa miaka mingi ulioshiwa na tija wa CCM, basi chama hicho kilikuwa ni CHADEMA. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Natumia neno kilikuwa na matumaini kwa kuwa naamini kuwa kwa hali ilivyo sasa ni vigumu na kama sio kitu kisichowezekana kwa watanzania kuendelea na imani waliyoanza kuijenga kwa chama hicho kuwa kingeliweza kuwakomboa kutoka kwa maovu ya CCM ambayo yanaonekana kukosa dawa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;CHADEMA wamefanya yale ambayo hata mahasimu wao CCM hawakutegemea kuyaona. Wameweza kutupa baharini nafasi ya kipekee ya kuhakikisha ushindi wa kutosha kwa chama hicho katika chaguzi zinazokuja na kuamua kujichimbia kaburi la kisiasa. Yaani wameamua kujiunga na historia ya vyama ambavyo vilikuwa tishio kwa CCM, kuanzia enzi za NCCR Mageuzi hadi CUF ambavyo kwa sasa vimebaki historia tu kama vyama mbadala vya CCM. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa nisingependa kuzungumzia ni nini CHADEMA ingeweza kufaidika ama kuathirika endapo wangelimchagua Zitto Kabwe kama mwenyekiti wao mpya. Ninachojaribu kuchambua ni faida gani CHADEMA kama chama na wapenda demokraisia nchini wangeliweza kupata na hasara gani ambazo uamuzi wa kumshawishi ama kumshinikiza Zitto kujitoa katika kinyang’anyiro hicho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukweli ni kuwa kitendo cha mwanachama mwenye ushawishi mkubwa kama alivyo Zitto Kabwe kuthubutu kusimama kushindana na Mwenyekiti aliyeko madarakani kilifungua nafasi kubwa sana kwa CHADEMA. Kitendo hicho kimeweza kuonyesha kwa vitendo kuwa chama chao ni kweli chama cha demokrasia na maendeleo na maneno hayo sio kauli mbiu tu. &lt;br /&gt;Wapo watu wengi, vijana kwa wazee ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakivutiwa na CHADEMA. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na kama ilivyo utamaduni wa watanzania, wengi wao bado walikuwa wanasubiri uhakikisho kuwa CHADEMA ni mbadala makini wa CCM ili wajiunge katika harakati za kuleta mabadiliko makubwa kisiasa. Wengi wao kuingia kwa Zitto katika kinyang’anyiro hicho ilikuwa ni ishara kuwa CHADEMA inaweza kuaminiwa kwa yale wanayoyasema kwani wanaonyesha kuyatenda.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiangalia kwa undani utaghamua kuwa kule kuingia tu katika kinyang’anyiro hicho kwa Zitto Kabwe kulikuwa ni mtaji mkubwa kwa CHADEMA na zaidi kwa maendeleo ya demokrasia nchini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kitendo cha Zitto Kabwe ambaye amekuwa kama kioo cha mafanikio ya wanasiasa vijana wenye uthubutu wa kusimama kupambana na mfumo kandamizi uliokuwa ukiwatisha kuthubutu kujiunga na vyama vya upinzani kuthubutu kuingia katika kinyang’anyiro hicho kulikuwa ni mwaliko wa wazi kwa maelfu ya vijana kujiunga na CHADEMA.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama CHADEMA wangeweza kuendelea na kufanya uchaguzi wao na mwishoni mshindwa akamkumbatia mshindi basi ni wazi hilo lingejenga imani kubwa kwa chama hicho miongoni mwa wapenda mabadiliko makini ambao hadi sasa wanashindwa kuamini vyama vyetu vya kisiasa na wanasiasa kwa ujumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa watanzania ambao tungependa kuona kunakuwa na mfumo ambao unawezesha nchi yetu kuwa na demokrasia ya kweli yenye kujenga umakini wa kisiasa katika kuchagua viongozi wetu na kufanya maamuzi makubwa na madogo ya kikatiba, kisheria, kisera, kifalsafa na kiutawala. Kuna umuhimu mkubwa wa kuwa na chama ambacho kitaweza kwanza kuondoa ukiritimba wa CCM katika vyombo vya maamuzi na baadae kutupa chaguo mbadala pale itakapowezekana kubadilisha chama tawala. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;CHADEMA ilishaanza kujenga muono huo miongoni mwa watanzania walio wengi. Zitto Kabwe ni mmoja wa watu ndani ya CHADEMA ambao wameweza kujenga hisia miongoni mwa jamii kuwa kama wangendelea vizuri ni muonekano wa kidemokrasia na maendeleo, basi wangeweza kujenga imani miongoni watanzania hao. Yaani CHADEMA walikuwa ndio wanaelekea katika kufanikiwa kujenga imani kuwa lipo chaguo mbadala la CCM katika nchi yetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukweli ni kwamba baada ya kuyafanya waliyoyafanya, ni wazi kama ilivyo vigumu kwa viongozi wa CCM kuzungumzia vita dhidi ya ufasadi mbele ya watanzania, kwa CHADEMA itakuwa ni vigumu kwa viongozi wao kusimama kuongelea umuhimu wa demokrasia na kupiga vita ukandamizaji nchini na kuaminika ama hata kueleweka.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Ni wazi CHADEMA wamejifunga uhalali hata wa kuongelea UFISADI ambayo imekuwa ajenda yao muhimu katika miaka ya kariuni. Kwani hapa wameonyesha ufisadi wa hali ya juu dhidi ya misingi ya kidemkrasia ambayo ina nafasi kubwa katika kufikia maamuzi ya kisiasa miongoni wa wapenda mabadiliko katika nchi yetu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kitendo walichokifanya, tena kwa kumkandamiza Zitto Kabwe ambaye ni alama ya uthubutu na umakini miongoni mwa vijana ambao ndio mtaji mkuu katika chaguzi zinazokuja, CHADEMA wamewaondolea hata nafasi waliyokuwa nao baadhi ya vijana wao katika kushinda kwenye chaguzi zijazo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kutokana na hali iliyotokea kuanzia sasa itakuwa vigumu sana kwa vijana wa CHADEMA ambao walikuwa nyota zinazotegemewa kubadili sura ya siasa katika uchaguzi ujao kuweza kuwashinda vijana wenzao wa CCM. Hii inatokana na ukweli kuwa hata wao o wamejijengea taswira ya ama kuunga mkono, kubariki ama kunyamazia nguvu za wazee ndani ya chama chao zikifisadisha misingi ya kidemorasia ambayo wao walipaswa vijana hao walipaswa kusimama kidete kuitetea na kuipigania. Ni wazi kuwa kuanzia sasa itakuwa vigumu kwa vijana wa CCM kusimama mbele ya vijana wenzao katika chaguzi zijazo na kuwashawishi kuwa wao ndio chaguo la mabadiliko ya kweli.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Zaidi, sababu ya kumshikiza Zitto kuacha kushindana na Mwenyekiti wao aliyekuwepo madarakani ili kuepusha mpasuko ndani ya chama ni sababu inayoleta maswali zaidi ya majibu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa chama ambacho kinasema kinapigania demokrasia na maendeleo nchi kuamini kuwa kuwaacha viongozi wawili kushinda katika uchaguzi ni tishio la umoja wa chama ni sawa na kukubaliana na fikiria mgando zilizomo miongoni mwa wahafidhina ndani ya CCM kuwa kuruhusu ushindani wa haki na huru kati ya vyama vya siasa nchini ni kuhatarisha amani na maelewano ya nchi yetu.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Pia, kusema kuwa Mbowe akipata mshindani mkali kutaleta mtafaruku ndani ya chama kunatoa sura ya ama wazee kumuogopa Mbowe ama kukiri kuwa CHADEMA hawawezi kufanya siasa za kiungwana na zisizo na chuki ambazo zingeleta mgawanyiko. Ni wazi fikira kama hizo sio tu zitazuia wengi wengine kujiunga na chama hicho lakini pia si ajabu tukasikia kuendelea kwa mlolongo wa wanachama na viongozi wa chama hicho kuondoka na kwenda kujiunga na jinamizi walilolizoea yaani CCM. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndio maana baada ya kuona hili nimekuwa nikijiuliza sana ukweli wa sababu za viongozi na wanachama kadhaa wa CHADEMA ama kuhama, kusimamishwa ama kufukuzwa uanachama katika miaka ya karibuni. Nimekuwa nikijiuliza kama ni kweli hawa walikuwa vidudu mtu vinavyohatarisha ustawi wa chama ama kuna tatizo la kiuongozi ndani ya chama hiki. Kutokana na maamuzi yaliyofanyika hivi karibuni nachelea kuamini kuwa wapo walio ondoka CHADEMA baada ya kushindwa kuvumilia kuvunjika moyo katika nia yao ya kujenga mabadiliko ya ndani ili kuweza kushawishi mabadiliko ya nje.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Na katika hili, ni wazi muathirika si Zitto, si Mbowe na wala sio CHADEMA tu bali ni mustakali mzima wa mapambano ya kujenga demokrasia nchini.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Kitendo cha kuonyesha taswira ya kuwa kuna uwezekano wa kiongozi wa CHADEMA kuwa tayari kutumia mbinu zozote zile, halali na haramu, makini na hovyohovyo, salama na hatari ili kulinda nafasi yake kileleni, kinaonyesha kuwa ile ndoto ya vyama vya upinzani kuungana ili kukishinda chama dola cha CCM zinaendelea kubaki hivyo, yaani ni ndoto tu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mantiki hiyo, ni wazi kuwa kitendo hiki kinahalalisha propaganda ya CCM na dola kuwa viongozi wa vyama vya upinzani wamegubikwa na ubinafsi na hawana nia ya kuwakomboa watanzania kama wasemavyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na hapa napenda kuwashauri wana CHADEMA kuacha kutumia ujanja wa CCM kama sababu ya yaliyotokea na yanayoendelea kuwakumba. Kufanya hivyo ni sawa na kuwaunga mkono watwala wetu wa sasa ambao daima hawachoki kuwalaumu wazungu ama wakoloni kwa umasikini na madhila waliyowezesha katika nchi yetu kutokana na makosa yao wenyewe. Ilichofanya CHADEMA ni kujianika mbele ya mashamulizi ya CCM na maadui wengi. Na itakuwa ajabu sana kama madui hao wataacha nafasi hii kuwashambulia na hata kuwamaliza kabisa wakati huu nyeti wa kuelekea katika chaguzi za kitaifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Zaidi, kitendo walichokifanya CHADEMA kinawapa nafasi na nguvu zaidi maadui wa demokrasia kuendelea kudhihaki harakati za demokrasia nchini. Wapo ambao wamekuwa wakipita mitaani kusema kuwa wanaopiga kelele kutaka demokrasia hawana nia ya kweli ya kuleta demokrasia ya kweli bali ni mbinu tu ya kuweza kujipatia madaraka na baadae kufanya yaleyale ambayo wanayalalamikia wakati wasipokuwa madarakani. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatua ya kumshikinikiza Zitto Kabwe kutotumia haki yake ya kidemokrasia ya kuomba ridhaa ya kuongoza chama chake kwa wanachama wenzake kinahalalisha mitazamo ya maadui wa demokrsia kama hao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi, uamuzi wa wazee wa CHADEMA kumshinikiza Zitto Kabwe kujitoa katika kinyang’anyiro cha kugombea nafasi ya uenyekiti wa chama chake kwa kuhofia uwepo wa siasa chafu zitakazoweza kugawanya chama chao ulichofanikiwa ni kuhalalisha matumizi ya siasa chafu na hovyohovyo na hivyo kudumaza kabisa ndoto na juhudi za watanzania wanaopenda kuona mfumo wa demokrasia makini unatawala nchini mwetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya kufuatilia kwa karibu mwenendo wa siasa zetu wakati wa uchaguzi uliopita (2005) na baadae kupata taarifa za ufisadi mkubwa uliokuwa na na bado unaendelea katika nchi yetu mara baada utawala Mwalimu Nyerere, nilikuja katika hitimisho kuwa CCM na wadau wake wamelibaka taifa letu, na sasa nachelea kuhitimisha kuwa CHADEMA wamebaka kademkorasia ketu ambako katika miaka ya hivi karibuni tulianza kujenga imani na matarajio nako.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-481762000284876144?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/481762000284876144/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=481762000284876144' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/481762000284876144'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/481762000284876144'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2009/08/wamebaka-na-kudumaza-kademokrsia-ketu.html' title='WAMEBAKA NA KUDUMAZA KADEMOKRASIA KETU'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-2813169440071155307</id><published>2009-07-25T08:49:00.000-07:00</published><updated>2009-07-25T08:51:44.626-07:00</updated><category scheme='http://www.blogger.com/atom/ns#' term='MY STILL LIFE....'/><title type='text'></title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://3.bp.blogspot.com/_eC7gpTgHV-Q/Smsp77o2zuI/AAAAAAAAAFc/X03XLHMj0jo/s1600-h/5081_222677835270_795910270_7597830_1864545_n.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;width: 320px; height: 213px;" src="http://3.bp.blogspot.com/_eC7gpTgHV-Q/Smsp77o2zuI/AAAAAAAAAFc/X03XLHMj0jo/s320/5081_222677835270_795910270_7597830_1864545_n.jpg" border="0" alt=""id="BLOGGER_PHOTO_ID_5362425890912784098" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-2813169440071155307?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/2813169440071155307/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=2813169440071155307' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/2813169440071155307'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/2813169440071155307'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2009/07/blog-post_25.html' title=''/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://3.bp.blogspot.com/_eC7gpTgHV-Q/Smsp77o2zuI/AAAAAAAAAFc/X03XLHMj0jo/s72-c/5081_222677835270_795910270_7597830_1864545_n.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-2751509014906180920</id><published>2009-07-02T14:07:00.000-07:00</published><updated>2009-07-02T14:14:05.974-07:00</updated><title type='text'>My uncle, my hero, my guardian, my role model, my Prof..</title><content type='html'>My uncle, my hero, my guardian, my role model, my Prof..&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;The family is at lost,&lt;br /&gt;Tanzania is at lost,&lt;br /&gt;ZANZIBAR is at lost, &lt;br /&gt;Africa is at lost,&lt;br /&gt;Palestine is at lost,&lt;br /&gt;The left is at lost,&lt;br /&gt;U should not leave us now Prof Othman...&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Not now when we need ur wisdom,&lt;br /&gt;Not now when we need ur patience,&lt;br /&gt;Not now when we need ur ideals,&lt;br /&gt;Not now when we need ur values,&lt;br /&gt;Not now when we need ur integrity,&lt;br /&gt;Not now when we need u most...&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yes u have given us the most,&lt;br /&gt;Yes u have stand for us during the worst,&lt;br /&gt;Yes u have taught the greatest&lt;br /&gt;Yes u have inspired the best, &lt;br /&gt;Yes u have done ur share,&lt;br /&gt;But u shouldn't leave us the earliest.....&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ur the best, &lt;br /&gt;Ur the greatest, &lt;br /&gt;Ur the LEFT,&lt;br /&gt;Ur the THA PANAFRICANIST,&lt;br /&gt;Ur the teacher, ur the wisdom, ur the hope, ur the role model, ur THA comrade, ur the friend in the struggle...&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;28th June 2009&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-2751509014906180920?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/2751509014906180920/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=2751509014906180920' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/2751509014906180920'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/2751509014906180920'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2009/07/my-uncle-my-hero-my-guardian-my-role.html' title='My uncle, my hero, my guardian, my role model, my Prof..'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-2026562469123487483</id><published>2008-07-28T07:35:00.000-07:00</published><updated>2008-12-10T17:48:38.011-08:00</updated><title type='text'>TANZANIA BORA HAITAJENGWA KWA STAILI YA BANDIKABANDUA</title><content type='html'>Ilyas, O.S @ August 2008&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika miaka ya hivi karibuni nchi yetu imekuwa ikipita katika mitihani migumu inayotishia hatima yake kama taifa na hatima ya watanzania kwa ujumla. Mitihani ambayo kwa hali moja inatusaidia kupevuka kama taifa na kwa hali nyingine inatishia mustakabali wetu kama taifa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali hii imefuata baada ya miaka kadhaa ya mtindo wa bandika bandua katika kushughulikia changamoto mbalimbali zinazolikumba taifa letu. Mtindo ambao kwa mantiki ya hali ilivyo sasa na dalili zinazonyesha huko tuendako, inatubidi kuachana nao haraka kabla hatujachelewa zaidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Changamoto tulizonazo ni lukuki ambazo ni wazi uzito wake utatuelemea. Hizi ni pamoja na tatizo la ufisadi, kuporomoka kwa maadili ya uongozi, kukua kwa hisia na kuongezeka kwa matendo ya kibaguzi miongoni mwetu, kustawi kwa matumizi ya siasa chafu, kupanuka kwa tofauti za kipato na kuongozeka kwa dalili za kuvunjika kwa muungano wetu. Kwa ujumla Tanzania ya sasa ina kila dalili mbaya ambayo hutokea katika jamii na matifa mbalimbali duniani zikiashiria kuvunjika kwa jamii hiyo ama tifa hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata  hivyo ni bahati mbaya kuwa mabadiliko yanayoendelea yamekuwa ni yale ya mtindo wa bandikabandua ambao unalenga zaidi katika kuendeleza uhalali wa tabaka tawala ambalo limejihodhisha nguvu zote za mabadiliko ya kisasa na kiuchumi badala ya kushughulikia mizizi ya changamoto hizo. Tumegubikwa na ujanjaujanja wa kushughulikia matokeo ya matatizo badala kuwa na uthubutu wa kushughulikia sababu ama mizizi ya matatizo hayo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali ya ufisadi unaokomaa, kuporomoka kwa maadili ya uongozi, kukua kwa hisia na kuongezeka kwa matendo ya kibaguzi miongoni mwetu, kustawi kwa matumizi ya siasa chafu, kupanuka kwa tofauti za kipato na kuongozeka kwa dalili za kuvunjika kwa muungano wetu hayo yote ni matokeo ya matatizo na sio tatizo lenyewe. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Viongozi wetu ni lazima wakubali kuwa wakati umefika kuacha kupendelea hatua za kufunika kombe mwanawazimu apite. Viongozi wetu wanapaswa kukubali kuwa suluhu la matatizo au changamoto tunazokumbana nazo ni kuzungumzia, kukubaliana na kutekeleza makubaliano ya jinsi gani ya kuikoa Tanzania yetu na jinsi gani ya kuijenga kwa pamoja Tanzania iliyo bora kwa wote. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kuwa wakati umefika kwa viongozi wetu kuonyesha njia kwa watanzania kukaa kwa pamoja kujadili na kukubaliana njia mwafaka na ya muda mrefu ya kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazotukabili. Na viongozi wetu wakishindwa kupata uthubutu wa kuongoza katika hili basi wajue wazi kuwa si kitambo sana watanzania watajitwalia mikononi mwao jukumu hilo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yapo mengi ambayo watanzania tunapaswa kuwa tayari kuyaongea na kukubaliana kwa ukweli na uwazi bila ya kuogopa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Watanzania tunahitaji kupata nafasi ya kuongelea masuala kama aina ya mfumo uchumi tupaswao kufuata, Mfumo wa kisiasa, mfumo wa muungano wetu wa Tanganyika na Zanzibar, Muungano wa Afrika Mashariki, sifa na maadili ya viongozi, utawala na sheria, haki na wajibu wa kijamii na jinsi gani tunaweza kuwa na mfumo wa uwezeshaji wa makundi maalumu ya kijamii bila ya kusababisha kutokuaminiana miongoni mwetu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunapaswa kukaa pamoja na kuongelea kuhusu mfumo wa elimu, mahusiano kati ya vyama vya kisiasa na dola, mfumo wa uchaguzi na uwakilishi, nafasi ya vyama vya kiraia katika jamii yetu na suala zima la mila na tamaduni za kitaifa nayo ni muhimu yaka angaliwa upya kwa pamoja. Vilevile masuala ya uraia na siasa, suala heshima na maelewano ya kijamii na nafasi za viongozi wa kijamii katika uongozi wa nchi yetu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kuwa hali ilivyo sasa ni ushahidi tosha kuwa wakati umefika sasa wa kuamua ni upi kati ya mfumo wa kibepari ama kijamaa tupaswao kuufuata na kwa faida ipi na njia zipi. Ni wazi kuwa bila ya uoga wowote tunapaswa kuliongelea suala la muungano ambalo kwa miaka sasa limekuwa kama donda liogopwalo kutibiwa ama hata kuguswa. Tunapaswa kulijadili sasa kuliko kuchelewa zaidi hadi kufika mahala chembe ya busara na uongozi thabiti iliyosalia, ikakosekana kabisa na kuacha chuki na dharau kuchukua mkondo kama dalili zinavyo onyesha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kuwa tunapaswa kujadili suala la maadili katika jamii yetu kwa mapana yake na si hili la muono wa karibu wa siasa na biashara. Suala la maadili ni suala muhimu pia si tu kwa viongozi ambao wanapaswa kuwa kioo cha jamii lakini pia wananchi kwa ujumla. Hivi sasa jamii yetu inageuka jamii ya kichokoraa ambapo kila mtu akishindana na mwenzie kuvunja sheria za nchi na jamii kwa ujumla. Maadili sio suala la watoto na vijana wetu tu kama tulivyozoe. Ni suala la wazee, wazazi, viongozi wakuu na wadogo, matajiri na masikini, wenyeji na wageni, na watawala na watawaliwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mfumo wa kisiasa nao unahitaji kufumwa upya ili kuwezesha demokrasia ya kweli kuweza kukomaa na kusaidia kujenga Tanzania yenye neema. Kamwe hili halitwezekana kama tutaendela na stili ya bandikabandua ambayo inalenga kulinda maslahi na nafsai za kundi fulani tu bila ya kujali mapungufu yanayotokana na staili hiyo ambayo yanamsabibishia mtanzania kuendelea kuishi katika maisha ya unyonge yasiyo na tija ya kimaendeleo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uamuzi wa kufanya mjadala huu wa kisiasa unapaswa kufikiwa sasa ili kuweza kutumia nafasi hii tuliyojikuta tunayo bila ya kuchelewa. Ni muhimu kufanikisha mjadala huo mapema ili kupelekea kutungwa kwa katiba mpya kabla ya mwaka 2010 itakayowezesha kuwa na uchaguzi ambao umefanyika chini ya mfumo mpya ulioshirikisha na kukubalika na watanzania wote. Tukawa na katiba ambayo itapata uhalali wa kila mtanzania aliye na haki ya kupiga kura. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Umuhimu wa kufanya hivyo unatokana na kuwa watanzania sasa zaidi ya wakati mwengine wowote wana shauku kubwa ya kuijenga nchi yao kwa uthabiti zaidi kama ari mpya inavyosomeka na wengi&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini vilevile ni muhimu kuamua sasa kwani siasa ni fani inayosifika kwa kubadili mwenendo wakati wowote ule. Kama uamuzi huo hautachukuliwa sasa na kutumia mazingira ya kisiasa na kijamii tuliyonayo sasa basi inaweza ikatokea hapo baadae hali ikawa mbaya zaidi na kulazimisha mabadiliko hayo yatokee baada ya kupitia njia mbadala ambayo itakuwa janga kubwa kwa taifa letu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tusingoje tufikie hali ya siasa za magomvi na chuki kama zilizowafikisha ndugu zetu wa Burundi, Sudan, Zaire (Kongo DRC), Siera Leone, Liberia walipofikia ndio tufikirie hilo. Na wala tusisubiri hali ya kutatanisha iliyojengwa katika upande mmoja wa muungano wetu yaani visiwa vya Unguja na Pemba ndipo tufikirie kufanya hilo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Badala ya kuendelea kupoteza muda, fedha, na hata maisha ya watanzania, viongozi wetu wanaotaka kukumbukwa kwa mapendo na sio chuki dhidi yao na vizazi vyao hapo baadae, wanapaswa kuwa na uthubutu wa kushinikiza na kuanzisha mjadala wa kitaifa kuhus hatima ya nchi yetu sasa bila ya kuechelewa zaidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mjadala bora na wa kujenga, daima hufanyika pale wahusika wanapokuwa katika hali ya mapendo, maelewano na heshima miongoni mwao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapo wanaodhani kuwa kuanzisha mjadala kama huu ni kufungulia matatizo ambayo yanaweza kushindikana kudhibitiwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapo wanaogopa kufungulia mabadiliko kwa kuwa wanaamini hali iliyopo sasa ni hali ya kupita tu na wataweza kubadili mwelekeo na ukawa unaoridhisha kwa upande wao. &lt;br /&gt;Hawa wote kwa kweli wamesahau kusoma nyakati. Mwenendo uliopo sasa hautabadilika bila ya kuwa tayari kuchukua uamuzi thabiti wa kuanzisha mjadala wa kitaifa kuhusu masuala yote muhimu yanayotusibu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Badala ya leo kuwa na mjadala wa kuwa na KADHI, kesho mjadala wa kuhamia Dodoma, kesho kushokutwa mjadala wa URAIA, mtondogoo mjadala wa Uongozi na Biashara, ni muhimu tukawa makini zaidi na kuanzisha mjadala wa kitaifa wa pamoja ambako haya yote na mengineyo yatajadiliwa kwa mpangilio madhumubuti na utakaopunguza mzigo kwa walipa kodi wa nchi yetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni mjadala wa kitaifa tu na sio maamuzi ya bandikabandua yanayolenga kulinda mfumo fisadi tulionao ndio yataweza kujenga Tanzania iliyo na neema kwa wote kama kauli mbiu ya chama tawala CCM. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni mjadala wa pamoja na sio ule wa wakubwa wachache tu utawezesha kuongeza utashi wa watanzania kulitumikia taifa lao kwa nguvu na uminifu zaidi. Ni utashi binafsi wa watanzania ndio utakaorudisha nidhamu binafsi na uzalendo miongoni mwa watanzania. Na bila ya kurudisha haya tutaendelea longolongo hadi kukuche lakini Tanzania bora kamwe haitawezekana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tanzania bora kwa wote itajengwa kwa kushirikisha watanzania wote bila ya ubaguzi wa aina yoyote na kamwe haitajengwa kwa mtindo wa mabadiliko ya bandikabandua kama tunaoendeleza sasa.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-2026562469123487483?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/2026562469123487483/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=2026562469123487483' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/2026562469123487483'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/2026562469123487483'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2008/07/tanzania-bora-haitajengwa-kwa-staili-ya.html' title='&lt;span style=&quot;font-weight:bold;&quot;&gt;TANZANIA BORA HAITAJENGWA KWA STAILI YA BANDIKABANDUA&lt;/span&gt;'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-2357519851055103401</id><published>2008-07-25T11:55:00.000-07:00</published><updated>2008-07-25T11:57:50.026-07:00</updated><title type='text'>CCM iende, Tanzania ibaki…</title><content type='html'>&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na Ilyas, O.S @ July 2008&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tangia serikali ya CCM kuamua kwa shingo upande kuanzisha mfumo wa siasa za vyama vingi hapa nchini kumekuwa na taharuki kubwa ndani ya chama hiki katika kuchagua kati ya maslahi ya nchi na maslahi ya chama. Hali hii imejengwa kutokana na sababu mbalimbali ndani na nje ya chama hicho. Moja ya sababu kuu ni kubadilika kwa falsafa na mantiki ya kisiasa ya chama hicho kutoka katika kumuendeleza mtanzania hadi &lt;br /&gt;kulinda na kuendeleza maslahi na nafasi ya tabaka tawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kuwa CCM ililazimika kukubali mfumo wa vyama vingi sio kwa sababu waliamini ni njia muafaka ya kulinda amani na umoja wa kitaifa. Ni wazi kuwa waiamua kufanya hivyo baada ya kung’amua kuwa bila ya kufanya hivyo wakati wakati ule basi mbeleni wangelazimika kufanya hivyo kwa matakwa na shurutisho za umma. Hali ambayo ni wazi isingewapa nafasi waliyonayo sasa ambapo bado wameweza kuhodhi nguvu za kuzuia mabadiliko ya kweli ambayo hayahakikishi usalama wa nafasi ya tabaka tawala. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali hii ya kubadilika kwa mantiki ya kisiasa ya CCM kutoka kujenga na kuendeleza taifa hadi kulinda nafasi ya tabaka tawala naweza kusema ndio mzizi mkuu wa matatizo lukuki tunayokumbana nayo hivi sasa. CCM wamekuwa wakijali zaidi kulinda mfumo wa kisiasa na kiuchumi tulionao ili kuepusha uwezekano wa kutokea mabadiliko ambayo yatadhoofisha nafasi ya kiutawala hata kama uhalali wao utatetereka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matatizo hayo ni pamoja na yale mapya ya ufisadi, uongozi mbovu, ubaguzi wa kidini, kikabila, kimapato, kirangi na hata kimaeneo na mengine ya tangia zamani kama lile la la hali na hatma ya muungano wetu. Hivi sasa wapo wanaochukulia haya kama ndio matatizo haswa na kuamua kutumia muda mwingi kufikiria, kuongea na hata kulalama mfululizo kama vile kuna uwezekano wa kuyashinda majanga haya bila ya kuyafikiria kwa mapana yake. Wapo wafanyao kosa hili bila ya kujua lakini wapo ambao wanajua wazi kuwa hali ya kufikiri hivyo ni tatizo kwani kunawezesha kuendelea kwa mfumo tulionao sasa ambao wao ni wafaidika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Suala la ufisadi ndilo limekuwa agenda kuu ya watanzania hivi sasa kiasi cha kufikia mahala ambapo ndio imekuwa kama taswira ya CCM miongoni mwa watanzania walio wengi, wana CCM na wasio wanaCCM. Bahati mbaya agenda hii ya UFISADI badala ya kutufanya watanzania tufikirie zaidi na zaidi inaelekea kuwa imeanza kutudumaza kifikira. Agenda ya UFISADI imekuwa kama kiongeza mwendo muhimu cha kufisadisha mustakabali wa Tanzania yetu badala ya kulitetea na kulilinda taifa letu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapo wengi wanaoshangaa ni jinsi gani CCM imeshindwa kulishughulikia suala hili katika njia ambayo sio tu ingeweza kuliokoa taifa letu lakini pia kuokoa nafasi ya chama hicho katika utawala wa nchi. Wengi wanaamini kuwa CCM chini ya uongozi wa Jakaya Kikwete kwa kutumia nafasi yake kama mwenyekiti wake lakini zaidi rais wa dola la Tanzania, inaweza kabisa kuchukua hatua madhubuti kuondokana na janga hili. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo ni wazi kuwa wanaoamini hilo wanashindwa kutambua jambo moja muhimu. Kwamba Chama Cha Mapinduzi hakijabadili tu falsafa yake kutoka katika ujamaa na kujitegemea kuelekea kusikojulikana, lakini pia kimebadili hata mantiki ya kisiasa kutoka kujenga na kuendeleza taifa hadi sasa kuwa ni kulinda nafasi ya tabaka tawala. Tabaka linalojumuisha walio wanachama na wasio wanachama wa chama hiki. CCM ya sasa sio ile ya zamani inayoamini hakuna maisha yenye umuhimu kama Tanzania. CCM ya sasa inaamini kuwa maslahi ya tabaka tawala ambalo limehodhiwa na kuneemeshwa na UFISADI yana umuhimu zaidi ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kwa mantiki hii ndio sasa tunaona sio tu tumekuwa na ongwa la uongozi linalosababisha kushindwa kwa kuchukuliwa hatua dhidi ya wale wanaosadikiwa kuwa ni MAFISADI lakini pia sasa kuhatarisha hata muungano wetu ambao wapo walio apa kiapo cha kuulinda kwa hali yoyote ile.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi karibuni kumekuwa na watu wakisema waziwazi na wengine ndani ya vikao vikuu vya CCM kuwa na tuachane na muungano. Wengi wao ni wale ambao agenda ya ufisadi imewakaba kooni hivyo wangelipenda kutumia kila njia kuondoa fokasi ya watanzania kutoka huko. Kwao wao ni bora muungano uende lakini madhambi yao yasahaulike, kwao wa ni bora Tanzania iende na CCM ibaki. Kwao wao Tanzania si chochote si lolote na CCM ndio kila kitu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inasikitisha na inatisha kuona kuwa hata wale walioapa mbele ya mungu na watanzania kuwa wataulinda muungano kwa nguvu zote ndio wanafikia kusema maneno kama acha muungano uende. Kwa maana nyingine wanasema acha Tanzania iende kwani ukikubali kuvunjika kwa muungano hakuna Tanzania. Inawezekana kutokana na mfumo wa muungano tulionao wapo wanaodhani kuwa tukirudisha Tanganyika bado tutabaki na Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inasikitisha sana kuwa watanzania tumefikishwa mahala kama hapa ambapo tupo tayari kuvunja nchi yetu ili mradi maslahi ya wachache yaendelee kulindwa. Inatisha mno kuona kuwa wafanyao haya ni wale ambao walibahatika kulelewa kwa misingi madhubuti ya muungano wetu. Yaani wale wa kizazi ambacho Mwalimu Nyerere alijitahidi kwa nguvu zake zote kukijenga katika fikira za utanzania zaidi ya yote. Hawa ndio wamekuwa wa kwanza kuusaliti muungano wetu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Cha ajabu ni kuwa haohao wanaodiriki kusema wacha muungano uvunjike ndio kwa miaka wamekuwa mstari wa mbele kuwaita wale wanaojaribu kushauri njia muafaka za kushughulikia changamoto za muungano kuwa ni maadui wa muungano. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika hali kama hii ni wazi watanzania tunapaswa kujiuliza masuala kadhaa magumu yatakayotapatia majibu muhimu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi kama hawa wanafanya hivi itakuwaje kizazi chetu cha vijana wa sasa ambacho kimenyimwa malezi ya kitanzania na kukuzwa katika fikira za ubinafsi na ufisadi kitafanyaje ? &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jee, kukubali usaliti huu unaoendelea sasa wa kuthamini maslahi ya CCM zaidi ya TANZANIA yetu ndio kutatuwezesha kutatua matatizo na changamoto tulizonazo sasa?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi ni kipi muhimu kati ya CCM na maslahi ya tabaka tawala ama Tanzania na maslahi ya watanzania ?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati umefika wa watanzania kuamka na kuwaeleza wazi na kwa nguvu zote ndugu zetu hawa kuwa ni bora CCM iende lakini Tanzania ibaki. Uoga wao wa kuthubutu kuchukua maamuzi magumu ambayo yaweza kuhatarisha usalama wa maslahi yao lakini ukalinda na kundeleza ujenzi wa taifa letu hauna uhalali wa kuifikisha Tanzania yetu tulipoifikisha. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati umefika kwa viongozi wetu ambao wangependa tuendelee kuwatofautisha wao na mafisadi mashuhuri tunaowanyoshea vidole sasa, kuthubutu kusimama kidete na kusema, ni bora CCM iende lakini Tanzania ibaki.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-2357519851055103401?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/2357519851055103401/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=2357519851055103401' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/2357519851055103401'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/2357519851055103401'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2008/07/ccm-iende-tanzania-ibaki.html' title='CCM iende, Tanzania ibaki…'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-8198749489736785405</id><published>2007-08-02T11:13:00.000-07:00</published><updated>2008-12-10T16:58:00.455-08:00</updated><title type='text'>Tulimsaliti na tunaendelea kumsaliti Amina wetu….</title><content type='html'>I really thank u, from my heart, kuna vitu vingi ulinisaidia, kuna miongozo fulani, courage fulani na mambo mengine mengi, nimeona nikushukuru tu leo, asante na naappriciate as I said before, IT COMES FROM MY INSIDE, DEEPLY IN MY HEART, THANKS ONCE AGAIN, WISH U LUCKY, BE BLA$$ED. Amina chifupa mpakanjia.&lt;br /&gt;Sender: +25577306944&lt;br /&gt;Sent: 10:44:37&lt;br /&gt;04/21/2007&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimepigwa na butwaa, nimeishiwa na nguvu, sijui nifanyeje….najiuliza, hivi wapi ningelifanya zaidi na kwanini sikufanya mapema?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapo juu ni ujumbe alionitumia mtu ambaye karibia mwaka mmoja sasa nilimwita dada na yeye akaniita kaka. Ni Amina binti wa Chifupa. Huyu ni Amina niliye bahatika kumjua kwa kipindi cha karibia mwaka mmoja sasa. Katu sio Amina niliyekuwa nikijidai namjua miaka mitano kabla. Ni ujumbe ambao dada yangu amina alinitumia zaidi ya mara mbili katika usiku wa manane majira ya ughaibuni. Ni ujumbe ambao nilidharau kuujibu kwa siku mbili zaidi hadi Amina alipoamua kunipigia simu kunikumbusha kuhusu ujumbe huo. Sikujua kuwa ni ujumbe wa kwaheri ya milele.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nakumbuka siku moja nikiwa mahala fulani naelekea nyumbani Tanzania nilimpigia simu rafiki yangu Zitto. Hii ilikuwa ni siku ambayo Rais Kikwete alihutubia Bunge letu kwa mara ya kwanza kama rais wa nne wa jamhuri yetu tukufu. Alitumia muda mwingi kunielezea ni jinsi gani alivyovutiwa na maudhui ya hotuba hiyo kitu ambacho kwa ninavyomjua rafiki yangu Zitto kilinishtua kiasi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katikati ya mazungumzo Zitto aliingiza suala la Amina. Akaniambia kuwa kwa muda mfupi aliofanya naye kazi anadhani kuwa Amina sio mtupu kama jamii inavyomtafsiri. Mimi nikamshauri kuwa jaribu kuwa naye karibu kumjua zaidi na kama kuna sehemu za kumsaidia basi asisite kufanya hilo kwa manufaa ya nchi yetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mimi binafsi nilikuja kufunguliwa macho kutambua hazina iliyojificha ndani ya Amina siku alipopanda juu ya madhabahu ya kielemu katika ukumbi wa Nkurumah pale Chuo kikuu cha Dar Es Salaam. Hii ilikuwa ni miezi ya mwanzo ya mwaka 2006. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbele yangu nilishuhudia Amina tofauti kabisa na yule ambaye jamii ikiongozwa na wana udaku walivyokuwa wakimtafsiri. Mbele yangu nilimuona kijana mdogo aliyejawa na ushujaa, upendo wa dhati kwa nchi yake na zaidi mwenye kipaji cha hali ya juu cha siasa. Mbele yangu nilimwona kijana ambaye sio tu amejawa na uthubutu wa kujaribu lakini pia aliyekuwa na ndoto ya kufanikisha mambo makubwa katika maisha yake.&lt;br /&gt;Mara baada ya Amina na wakina dada wengine mashujaa waliokuwepo pale kumaliza kutoa ushuhuda wao kuhusu nafasi ya mwanamke katika siasa za nchi yetu, nililazimika kusimama ili nami nitoe ushuhuda wangu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilianza kwa kumuomba radhi dada Amina. Bila ya kusita nilimtaka radhi kutokana na mimi kuwa mmoja wa wale watanzania waliokubali kuamini kashfa, uzandiki, na zaidi unyanyapaa ambao baadhi wanajamii walikuwa wakimfanyia.Baada ya hilo nikamuahidi urafiki naye ili tuweze kubadilishana mawazo na ujuzi ambao niliamini kwa upande wake ungeweza kumwongezea pale alipopungukiwa na mimi kuongeza pale nilopopungukiwa na vilevile kutimiza lengo langu la kusaidia vijana wenzangu haswa kina dada kama Amina kufanikiwa ndoto zao katika ushiriki wa kujenga taifa letu kwa pamoja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya muda mfupi wa kujuana na zaidi kufaidika na tabia ya ucheshi na upendo mkubwa aliokuwa nao Amina, nikajikuta naongeza rafiki mwingine wa karibu katika maisha yangu ambaye kwa kweli alifikia kuwa mdogo wangu mpendwa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mdogo wangu ambaye leo nasikitika kuwa sikufanya vya kutosha kwake yeye kunishukuru kama alivyofanya katika ujumbe huo hapo juu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mdogo wangu ambaye namshukuru mwenyezi mungu kwa kunipa nafasi ya kumtaka radhi kutokana na makosa niliyofanya hapo mwanzoni ya kumtafsiri vibaya. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mdogo ambaye amenifundisha umuhimu wa kutowatafsiri na kuwahukumu watu ambao tunadhani tunawajua kumbe ukweli ni kuwa hatuwajui. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mdogo ambaye alinifundisha kumpokea mtu kama alivyo na sio kama tunavyotaka sisi awe. &lt;br /&gt;Mdogo ambaye kwa muda mfupi sana amenifunza mengi kuhusu dunia hii kuzidi hata niliyojifunza katika zaidi ya miaka ishirini niliyokaa darasani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Muda uliruhusu machache kushauriana. Lakini katika muda huo kiduchu Amina alitokea kuwa mwalimu na mwanafunzi mzuri kwangu na mwenye kuthamini mawazo yangu kama ambavyo alivyokuwa akithamini na kutetea mawazo yake kwa uthabiti mkubwa. Amina hakuwa mtu wa kuburuzwa na wala kutishwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ushahidi unaonyesha kuwa kadiri alivyokuwa akitishwa ndivyo alizidi kuwa na ushujaa wa kusimama na kuongea yale ambayo aliamini kuwa yanapaswa kusemwa bila ya kujali kama wale aliokuwa akiwasemea wanamshukuru ama kumdhihaki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siku moja nilikuwa nikipata nasaha za mzee mmoja ambaye alimjua mzazi wangu wakati akiwa hai. Mwishoni mwa mazungumzo aliniasa kitu kimoja. Mzee huyu aliniasa kuwa katika dunia yetu Mawalii huja kwa sura nyingi na mara nyingi huja katika sura ambayo wengi hawakutegemea na hivyo kushindwa kutambua bahati waliyoletewa na mwenyezi mungu hadi pale atakapotoweka. Waseme watakayosema lakini kwangu nathubutu kuamini kuwa Amina alikuwa ni walii aliyeletwa duniani kupima ubinadamu wetu na kutuelimisha mengi.Walii aliyekuja na ujumbe wa kuthubutu kupambana na moudhi yaliyoigubika jamii yetu bila ya woga.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika maisha yake tangia akiwa kigori hadi alipokabidhiwa majukumu makubwa ya kutetea maslahi ya vijana wenzake katika chama tawala, Amina amekumbwa na mengi. Kama ni mitihani basi ni wazi Amina alipata mitihani mikubwa sana. Mtihani mmojawapo ulikuwa ni ule wa wanajamii aliokuwa akiwapenda na kujitolea muhanga kuwatetea kujenga mazoea ya kumdharau, kumdhihaki, kumkejeli, kumbeza na zaidi kutomwamini katika katika uthabiti wake wa kutetea maslahi yao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wengi walikuwa wakimwona Amina kama mtu aliyekuwa amelewa na mafanikio. Wapo waliodhani kuwa Amina alikuwa akifurahia sana aina maisha aliyokuwa anakumbana nayo kila kukicha. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Masikini hawakujua kuwa ndani ya lile tabasamu murua lilojaa bashasha kulikuwa na mateso makubwa akilini na rohoni. Inasikitisha kuwa hata wale aliokuwa akiwaona kama kimbilio lake ndio kabisa hawakuweza kumpa nafasi ya kupunguza yaliyo rohoni. &lt;br /&gt;Naamini kuwa kamwe sina haki ya kuwasema wanafamilia wake lakini nathubutu kuwasema wanajamii wengine wote. Hawa wakiwemo wanasiasa wenzake haswa wale wenziwe katika chama chake, waandishi wa habari, wanaharakati wa kijamii na hata wenzangu na mimi wasio na chao ambao Amina daima alikuwa akipenda kujinasabisha nao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa miaka mingi hawa wote nikiwemo na mimi tumekuwa tukimsaliti Amina kila kukicha. Wengi wetu tumekuwa tukimdharau, kumsimanga na hata kutengeneza na kushabikia maneno ya uzandiki ambayo yalikuwa yakitafuna furaha ya Amina kila uchao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati aliposimama kuwaongelea mamilioni ya watoto wa shule wanaotembea maili kadhaa bila ya viatu na wala uhakika wa kutia kitu tumboni siku nzima wawapo shuleni na hata wanaporudi nyumbani, tulimdhahaki na kumwambia anaongelea upuuzi. Eti amezidi umediocre. Aliposimama kuongelea maswahibu yanayowakuta watoto wa shule haswa katika wilaya za jiji la Dar es Salaam tulimwambia anataka kujijenga ili apate ubunge katika moja ya jimbo la jiji hilo. Waliodai kuwa ni jimbo lao hawakuacha kumtumia maonyo makalimakali. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata alipothubutu kusimama kuongelea manyang’au wanaojineemesha kwa kuwabebesha na kuwauzia maelfu wa vijana wenzetu sumu inayowamaliza kila siku, yaani madawa ya kulevya, tukamdhihaki kuwa ni mtoto mdogo hajui afanyalo. Wapo waliofikia kudai kuwa amefanya hivyo kumkomoa mumewe. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukweli ni kuwa hakuna aliyetaka kuamini kuwa ndani ya sura ile iliyojaa bashasha kuna uchungu wa dhati juu ya maslahi ya kijana mtanzania wa kawaida anayeathirika na hayo. Kijana wa kawaida ambaye tofauti na waheshimiwa wengine wengi katu Amina hakuacha kujinasabisha nao. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mara dada yetu alipozimika kila mtu akaibuka kutafuta mchawi. Mara hili mara lile. &lt;br /&gt;Kama kawaida ya wanadamu hakuna mwenye ubavu wa kuthubutu kujiangalia yeye binafsi ni vipi amechangia Dada yetu Amina kutuacha katika mazingira ambayo amefariki. Hakuna anayetka kung’amua ukweli kuwa wote kwa pamoja tulimsaliti Amina wetu. Wakati akituhitaji sisi tulikuwa tukimbeza na kumdharau. Wakati akihitaji mapendo yetu sisi tulimkejeli na kumzodoa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yote hayo aliyoyakusanya moyoni miaka nenda miaka rudi yakamalizwa kwa pigo la mwisho. Pigo ambalo lilimpelekea kuamini kuwa hata yule ambaye wazazi wake walitoa idhini ya kuwa mlinzi wa roho yake na mwili wake hapa duniani naye hakuweza kuwa naye pale alipokuwa akihitaji zaidi mapendao na uelewa zaidi. Na zaidi alipotaka kuyatoa yaliyokuwa yakimmaliza rohoni wapo waliothamini maslahi yao zaidi ya roho yake. Wote kwa pamoja tukaendela kumsaliti Amina wetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inasikitisha zaidi kuona kuwa hata katika kifo chake tunaendelea kumsaliti Amina. Badala ya kujiuliza ni vipi tutaendeleza moto aliouwasha kuokoa vijana wenzetu na jamii yetu kwa ujumla, tunaendela kushabikia uzandiki, unafiki na udaku dhidi ya dada yetu Amina. Jamani tusitafute mchawi. Wengine walimalizia tu lakini sote tulimsaliti Amina wetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kweli natamani wote tungelimjua Amina wa kweli. Yule Amina niliyebahatika kumjua karibia mwaka mmoja tu kabla hajatuaga, Amina mwenye ucheshi wa haja. Amina mwenye nidhamu hata kwa wale aliokuwa akijua wanamdhihaki na kumdharau. Amina mwenye upendo wa kweli kwa watu wote, Amina asiyeogopa kusema na kufanya yale yote aliyoamini ni ya haki na yanapaswa kusemwa ama kutendwa. Amina mwenye uthubutu ambao wengi wetu tumeukosa. Amina nyota tuliyoizima hata kabla haijang'ara. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwenzenu natamani ningelifanya zaidi na zaidi kuonyesha urafiki wa kweli kwako dada yangu mpendwa Amina. Siamini kuwa eti nami sikuweza kuwa karibu nawe wakati ukihitaji zaidi urafiki wangu hata kwa uchanga wake. Amina dada yangu umetutoka lakini namshukuru mungu uliniaga kwa maneno ya upendo ingawa akati ule  sikujua hilo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema tu ndiye ajuaye kuondoka kwako kuna funzo gani kwetu. Watasema yote lakini jua kuwa tupo tuliobahatika kukuamini na kukuthamini kwa dhati hata kama muumba hakutupa muda mrefu wa kufanya mengi. Nasema tumebahatika kwani ni nadra kwa dunia yetu hii kupata bahati ya kuitwa rafiki na walii kama wewe. Cheche ulizowasha kamwe hazitaenda bure. Bendera tutaipeperusha hadi mwisho sio kwa maneno bali kwa vitendo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msalimie kaka Chachage. Mwambie akusomee hadithi ya makuwadi wa soko huria. Mwambie ndoto yake ya ukombozi wa mlalahoi wa Tanzania yetu baada ya miaka kadhaa ya unyang’au wa soko huria inaelekea kutotimizika hivi karibuni. Mwambie kuwa yule mswahili mlalahai mwenzio Jakaya anahitaji makarama zaidi kutoka kwake huko alipo ili aweze kutimiza yale matumaini aliyokuwa nayo kwake kabla hajatuaga na kutuacha wapweke pale mlimani. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Namalizia kwa kunukuu ujumbe wa taarifa ya kifo chako kutoka kwa rafiki yetu kipenzi Zitto: AMINA AMETUTOKA….&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-8198749489736785405?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/8198749489736785405/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=8198749489736785405' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/8198749489736785405'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/8198749489736785405'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2007/08/tulimsaliti-na-tunaendela-kumsaliti.html' title='Tulimsaliti na tunaendelea kumsaliti Amina wetu….'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-4882931056477692557</id><published>2007-08-02T10:49:00.000-07:00</published><updated>2008-12-10T16:52:34.172-08:00</updated><title type='text'>WAANDISHI WETU NA UKUWADI WA UNYANG'AU</title><content type='html'>@14th July 2006, Published by Tanzania Daima Newspaper.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Comrade Chachage aliwaita makuwadi wa soko huria, mimi nawaita makuwadi wa unyang’au. Makala hii niliandika miezi mingi iliyopita lakini mengi yalinisababisha kutoiwakilisha kwa wapendwa watanzania. Kutangulia kwa kaka yangu na mwalimu wangu wa fikra changanuzi, kumenipa nguvu za kuwasilisha hoja yangu kwa watanzania, wanyonyaji kwa wanyoge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Neno manyang’au lina tafsiri mbalimbali katika macho ya watanzania. Kwangu mimi unyang’au ni ile hali ya kufikiri na kutenda mambo ambayo yanaathiri mustakabali mzima wa mwananchi wa kawaida. Manyang’au ni wale wote wanaotenda mambo mbalimbali kwa maslahi ya uchu wao pekee bila ya kujali madhara makubwa ya matendo hayo kwa jamii. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hawa ni wale walio katika nafasi zote na haswa za juu za kutoa  maamuzi serikalini, kwenye vyama vya kisiasa na katika makundi mengine ya kijamii. Hapa nchini mwetu  utawakuta katika kila pembe ya maisha yetu. Wapo wenye nguvu kisheria kuwemo katika kundi hilo na wapo walioweza kujipenyeza humo kwa kutumia mbinu mbalimbali kama vile uwezo wa kiuchumi na nafasi zao katika makundi ya kijamii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Manyang’au wapo wakubwa na wadogo. Wapo wa kutoka nje na wapo wengi tunaotoka nao katika nchi yetu hii hii iliyojaa harufu na ladha ya umasikini wa kutupwa. &lt;br /&gt;Unyang’au ni mfumo rasmi katika jamii yetu ukiwa na baraka za kisheria kama zile za takrima na nyinginezo nyingi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Makuwadi wa unyang’au ni wengi na wapo katika sekta zote za kisiasa, kiuchumi na kijamii katika nchi yetu. Wapo wanaojiita wafanyabiashara, wapo wanaojiita makada, wapo wanaojiita wasomi, wapo wanaojiita watumishi wa serikali na wengine wengi.&lt;br /&gt;Wapo ambao wanafaidika kweli na unyang’au huo na wapo wale wanaodhani kuwa wanafaidika lakini kumbe wakipatacho ni makombo tu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapo wanaojiona kuwa wanakundi halali katika mfumo wa kinyang’au na wapo waliomo humo kwa kujipendekeza na kuifaragua. Wapo waliomo humo kwa kupenda na wapo waliojikuta humo bila ya wao kujijua. Wakiulizwa wanadai ni kulazimika kutokana na mazingira yaliyopo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hawa wote wamekuwa tayari kuuza uwezo na ujuzi wao kifikira na kikazi kutetea, kusadifu na kulinda mfumo unaohalalisha unyang’au katika jamii yetu. Wengi wamekuwa wakifanya hivyo kwa kudhani kuwa wanaenda na wakati ambao unashurutisha kila mmoja wao kuwa na “mahusiano mazuri” na manyang’au wa nchi yetu na wale kutoka nje ya mipaka yetu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwao wao, ili kuwa na kile wakionacho ni mafanikio kimaisha, ni lazima wajitumikishe kwa manyng’au wa nchi hii ambao wengi wao wana nguvu za ushawishi katika dola la nchi yetu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Moja ya sifa ya pamoja ya ndugu zangu hao walio amua kukuwadia unyang’au ni kutoacha kulalamika kuhusu masahibu ya unyang’au katika jamii lakini kwa upande mwingine wanageuka kuwa ndio wasadifu na walinzi mahiri wa mfumo sababishi.Hapo mbeleni tutawachambua wote kwa makundi yao, katika makala hii ningependa kuongelea makuwadi waliomo katika sekta ya uandishi wa habari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Fani ya uandishi ya habari ni moja ya nguzo muhimu za kiutawala ambazo jamii yoyote inayothamini umuhimu wa mfumo wa demokrasia inapaswa kuipa kipaumbela na umuhimu wa hali ya juu. Bahati mbaya katika Tanzania yetu fani hii imegeuka kuwa adui mkubwa wa demokrasia ya kweli na hata kutishia hatima ya mchakato mzima wa kuanzisha na kuboresha misingi ya kidemokrasia katika jamii yetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa miaka mingi sasa, wachunguzi wa mambo ya siasa na jamii wamekuwa wakijadili nafasi ya fani ya uandishi wa habari katika nchi yetu. Wengi wamekuwa wakihoji uwezo wa wahusika wa fani hii. Wengi wamekuwa wakijaribu kuchambua uwezo wa kitaaluma wa wengi wa waandishi wetu ambao wameonekana kana kwamba huwa wakifanya kazi hiyo bila ya kuwa na sifa za kitaalamu zinazohitajika katika fani hiyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kweli ukiangalia historia ya nchi yetu na zaidi sera za serikali yetu kuhusiana na suala zima la elimu na sio katika fani ya uandishi wa habari tu, utang’amua kuwa mfumo mbovu wakutojali elimu bora ni moja ya sababu kuu ya tatizo hilo. Hata hivyo ukosefu wa nia thabiti, utashi wa kutetea haki zao na hata uzalendo wa kweli, ndugu zangu waandishi wa habari ambao mimi huwaita wahandisi wa habari, wamegeuka kuwa makuwadi wa unyang’au unaoendelea kuligubika taifa letu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndugu zangu hawa ama kwa kupenda au kulazimika kimazingira wamegeuka kuwa watetezi na waficha maovu ya manyang’au wa nje na wa ndani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndugu zangu hawa wameamua kuwa wasadifu wa manyang’au wa nchi yetu na mfumo wao.  Kazi yao kubwa imekuwa ni kuhalalisha na kuusimika mfumo wa kinyang’au uliojengeka katika nchi yetu katika fikira za watanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Waandishi wetu wamekuwa tayari kuwapaka rangi za kuvutia baadhi ya manyang’au wa nchi hii, wakubwa wao kwa wadogo, na kuwavika sura ya utakatifu mbele ya watanzania walio wengi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati vyama vya upinzani vikiwa vimenyang’anywa nguvu za kutekeleza ipasavyo jukumu kukosoa na kuwaeleza wananchi ubaya ama uwongo wakubwa wa mfumo wetu wa kinyang’au, ndugu zangu waandishi wameamua kuwaacha watanzania katika msitu wa giza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanahabari wetu wanapaswa kujua kuwa ushabiki wa ajabu wanao uonyesha kwa watawala wetu ambao miongoni mwao wamelewa utamaduni wa kuwadhulumu watanzania haki zao za msingi, unalipeleka taifa letu katika mustakabali wa kutisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kuwa kama ndugu zetu wanahabari hawatazinduka na kuanza kutekeleza kwa dhati wajibu wao kwa wananchi, kuna hatari ya wajanjawajanja miongoni mwetu kutulazimisha kurudi rasmi katika enzi za siasa za chama kimoja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati wa uchaguzi na mchakato mzima ndani ya vyama kuelekea katika uchaguzi huo, tulishuhudia jinsi kujitokeza wazi kwa hali hii ya ukuwadi miongoni mwa ndugu zangu. &lt;br /&gt;Mwanzoni wengi wetu tulidhani kuwa hilo lilikuwa ni zoezi muda mfupi la wachache kujipenyeza katika timu ya ushindi na wengine kutimiza wajibu wao kutoka kwa wafadhili wao waliogeuka kuwa waajiri mbadala wao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini kwa hali inavyoendelea hivi sasa, inaelekea uozo uliopo ambao tayari umeshatanda katika nyanja zote za fani hii ya uandishi. Hii ni kuanzia wamililiki, waajiri, wahariri, waandishi wa kawaida na hata wasomaji umesababisha donda ndugu ambalo linaweza likashindwa kutibika.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapo waliofikia hata kubeza na kudhihaki juhudi za wachache waliokubali kuchukua jukumu la kuendeleza mapambano ya kutukomboa katika mfumo butu wa utawala wa chama kimoja. Tabia hii ya kuwakuwadia manyang’au kwa kutumia wino ni kuwageuza watanzania kuwa kama bendera inayofuata upepo ambayo haina uwezo wa kuhoji maamuzi yanayobariki unyang’au katika jamii yetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kukuwadia unyang’au wa aina yoyote na mahala popote ni kujidanganya nafsi zetu. Sumu ya unyang’au kamwe haiachi kumdhuru kila mtu katika jamii husika na hata ile ya mbali. Hata kama madhara yake hayataonekana kwa mhusika binafsi wakati wa uhai wake, ni lazima itamsibu huko aendako kupitia kwa vizazi vyake. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo, ni wajibu wa ndugu zangu waandishi wa habari kuwa wa mwanzo kujinasua katika laana ya unyang’au kwa kuacha kuwakuwadia makuwadi wetu, wa ndani na nje na kuwaonya wengine wa aina yao katika sekta zengine.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-4882931056477692557?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/4882931056477692557/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=4882931056477692557' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/4882931056477692557'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/4882931056477692557'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2007/08/waandishi-wetu-na-ukuwadi-wa-unyangau.html' title='WAANDISHI WETU NA UKUWADI WA UNYANG&apos;AU'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-3623841977806449936</id><published>2007-08-02T10:44:00.000-07:00</published><updated>2008-12-10T17:03:36.142-08:00</updated><title type='text'>MWANZO WA SAFARI YA MWISHO YA CCM</title><content type='html'>@2005..Published by by a local Tanzania Newspaper&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni ukweli usiopingika kuwa matokeo ya uchaguzi wa mgombea wa nafasi ya urais katika Chama Cha Mapinduzi yameweza kuliepusha kundi hili kisiasa katika hatari ya kugawanyika kwa kasi kama ilivyokuwa ikionekana awali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naongelea dhana ya kugawanyika kwa kasi tu, kwa kuwa nina uhakika kuwa mwenendo mzima wa siasa za uchaguzi huo na mambo kadhaa yaliyojitokeza katika siku za mwisho za shughuli hizo ndani ya chama hicho, zimeleta mgawanyiko mkubwa na wa hatari zaidi utakaodumu daima.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata kama kwa njia za ajabu mno ndugu hawa wameweza kumchagua mtu ambaye kwa maoni yao wana uhakika wa kuendelea kutawala watazania kwa miongo kadhaa ijayo. &lt;br /&gt;Ni wazi kuwa CCM ya sasa si ile tena iliyokuwa ikiwavutia watu kwa utulivu wake, uongozi wa kufuata maadili ya utanzania, falsafa zake zenye kujali utu, kupinga ubaguzi na mengineyo mengi mazuri yaliyokuwa yakitofautisha chama hiki na makundi mengine ya kisiasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chama cha mapinduzi kama ilivyo kwa vyama vingine vikubwa tawala barani afrika, kimepitia mabadiliko mbalimbali hadi kufikia sasa.Mabadiliko hayo yameanzia kutoka kuwa chama cha ukombozi, kikaja kuwa chama cha kujenga utaifa na baadaye kuwa chama cha kuimarisha uchumi na kuboresha maisha ya watanzania kabla ya sasa kugeuka kuwa chama cha kuhakikisha kuendelea kubaki madarakani kwa tabaka tawala.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbadiliko huu umekuja kutokana na nguvu mbalimbali za kimfumo na mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi duniani ambayo yamepelekea washika dau wa chama hiki ambao mwanzo walijitahidi kukabiliana vilivyo, kuamua kufuata mkondo wa mabadiliko ili kuweza kuendelea kuongoza taifa hili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mfano mkubwa wa mabadiliko haya nje ya mipaka yetu ni chama cha Labour cha Uingereza kinachoongozwa na mwanasiasa “kijana” machachari Tony Blair. Chama ambacho wiki iliyopita kilipata pigo kubwa la kisiasa kwa kupoteza viti vingi katika baraza la wanaojiita wawakilishi wa makabwela.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama ilivyokuwa CCM, chama hiki kilianzishwa kama kundi la kutetea wafanyakazi na makabwela wa Taifa hilo la kibwanyenye. Na mama ilivyo kwa vyama vingi vya aina hii duniani, chama cha Labour kama kilivyokuwa CCM hapo awali, kilikuwa ni chama kinachoendeshwa na misingi na falsafa madhubuti za kutetea wanyonge.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Falsafa na misingi ambayo walijiwekea ili kila anayetaka kuchaguliwa kukiongoza chama hicho na hivyo kugombea nafasi ya kuongoza serikali ya Uingereza alipaswa kuonyesha wazi kuwa ni mfuasi makini na mwaminifu wa misingi hiyo kwa kauli thabiti na vitendo.&lt;br /&gt;Mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi duniani yalikipelekea chama hicho kukosa mvuto wa kuaminiwa na wapiga kura wengi na hivyo kuwekwa kando katika kuingoza Uingereza kwa miaka kadhaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali hiyo iliwapelekea kundi dogo la wanasiasa vijana machachari wa chama hicho akiwemo bwana.. Mandelson ambaye aliwahi kuishi Musoma, Tanzania kwa miaka kadhaa akitafiti siasa ya ujama na kujitegemea na utaalamu wa kiuongozi wa baba wa Taifa, kuja na mbinu mpya walioita LABOUR MPYA.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tofauti na Labour ya kihistoria, New Labour kama ilivyo CCM hivi sasa, ililenga matumizi ya siasa za kubabaisha zilizo tofauti na misingi na falsafa asilia ya chama hicho ili kuweza kuwalaghai wapiga kura waliokitupa, kukichagua na kukirudisha madarakani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwao wao ni kuwa mara baada ya kurudi madarakani wangeweza kuzirejesha siasa makini za kihistoria za chama hicho na hivyo kuendeleza misingi na falsafa zake asilia kwa mtindo unaoendana na wakati uliopo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama hapo baadae ilivyokuwa kwa upande wa wahafidhina wa chama cha Republican cha Marekani walipomchagua George W Bush kuwauzia fikira zao za kulinda nafasi ya ubabe wa marekani duniani, Mandelson na wenzake waliamua kumchagua mwanasiasa machachari aliyekuwa akikubalika wakati huo yaani Tony Blair kuongoza mpango huo.&lt;br /&gt;Matokeo yake ni hali inayonekana hivi sasa huko Uingereza. Sio tu chama hicho kimegeuka kuwa cha kinyang’au zaidi kuliko chama cha mahafidhina wa kijadi cha Conservative, hivi sasa kinaelekea kaburini kwa mwendo wa kasi mno. Kitu pekee kinachowezesha wao kuwa madarakani hadi hivi leo sio uhalali wa kidhati kutoka kwa wananchi isipokuwa propaganda za kuwapumbaza wapiga kura. Propaganda zinazolenga kuwaweka mateka Waingereza walio wengi kwa kutumia dhana ya kuwa hakuna mwengine mwenye mvuto kama yeye anayeweza kuwalinda waingereza kwa madhila makubwa zidi kutoka kwa chama cha wahafidhina.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiangalia mlolongo mzima wa historia ya chama cha Labour ni wazi kuwa kuna mambo yanayoshabihiana na hali inayojikita ndani ya chama cha mapinduzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapo zamani hata baada ya kuruhusu siasa za vyama vingi  chama cha mapinduzi kilikuwa ni chama kilichokuwa kinapata wafuasi wengi kutokana na hali ya kuwa wengi wa wananchi hawa walikuwa wakijinasabisha na misingi na falsafa za chama hicho. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata kama wengi walikuwa wakikatishwa tamaa na matendo ya viongozi walio wengi wa chama hicho ambayo ni tofauti na sura yake asili, kuwepo kwa umakini wa kimaamuzi haswa yale makubwa kama vile mtiririko mzima wa kubadilishana madaraka kuliwapa faraja wanachi wengi waliokuwa wanaendelea kukata tamaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hili na lile la kuwepo kwa baadhi ya viongozi wachache ambao tofauti na walio wengi, kauli zao na matendo yao yenye kuonyesha kuendelea kwao kuamini misingi na falsafa asilia za chama hicho, kuliwapa moyo wa matumaini watanzania walio wengi, wanachama na wasio wanachama. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali hii iliweza kuwazuia wanachama waaminifu wa chama hicho vijana kwa wazee, wenye sifa za umakini wa hali ya juu kutokisusa ama kutohama chama hicho kwa muda mrefu sasa. Wengi hawa walikuwa bado wakiamini kuwa ipo siku chama hiki kitapata uongozi imara na makini utakaowezesha kurudisha chama na nchi yetu katika mstari ulionyooka na kuachana na siasa za sera za kukurupuka kwa minajili ya kuwalaghai wapiga kura tu. Ndio maana hata hivi karibuni tulipokuwa tukishuhudia siasa chafu za kupindukia mipaka ya utanzania na ubinadamu kwa ujumla, bado walikuwepo waliukuwa wakiamini kuwa mwishoni busara za uongozi wa chama hicho zingesimama na kurekebisha mambo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata hivyo hilo halikutuokea na waliukuwa wakiaminiwa kwa kazi hiyo ama walinyamaza kimya, walinyamazishwa au waliamua kukubali yaishe na kubariki siasa chafu zenye kukiuka misingi madhubuti ya chama hicho kutawala maamuzi ya vikao vyake vikuu.&lt;br /&gt;Yote yanaweza kufumbiwa macho lakini kitendo cha Mwenyekiti wa chama hicho kuamua kuzuia taarifa ya siri ya sekretarieti ya maadili ya chama hicho iliyokuwa ikielezea vigezo vya kimaadili vya wagombea wote kuzungumziwa na wanakamati kuu ni kosa kubwa la kihistoria.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maelezo kuwa wote wametoa rushwa hivyo wote sawa, kwa kweli ni upuuzi wa hali ya juu ambao kamwe hakuna aliyefikiri kuna siku mwenyekiti wa chama hicho anaweza akaufanya (sasa tunajua ni kwa nini).Hata kama historia na tafiti mbalimbali zinaonyesha wazi kuwa chama hiki kimekuwa kikumbatia rushwa na kiongozi wake kuishia kutoa vitisho vya mdomo tu, lakini inapofika mkuu huyo anahalalisha uchafu huo ambao ni tofauti na nguzo kuu asili za chama hicho ati kwa kuepusha kubomoka kwa chama, ni wazi safari ya mwisho imewadia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lingine ni lile la kuruhusu wanakamati kuu ambao wengine ni viongozi waandamizi bila ya aibu kutumia siasa ya ubaguzi ndani ya vikao vikuu kama hivyo. Pale wahuni kadhaa walipokuwa wakitumia siasa haramu na chafu kama hizo kwenye vyombo mbalimbali vya habari, halali na haramu, baadhi ya watanzania makini ambao ndio walikuwa ngome ya mwisho wa chama hiki waliweza kuelewa na kuvumilia.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Lakini pale anapokuja mtu mkubwa kama Waziri mwandamizi akasimama akipinga kuchaguliwa kwa fulani kwa kuwa amezaliwa akiwa na mchanganyo wa kabila au rangi fulani, na wakubwa hao wakapigia makofi, kunyamaza au mwenyekiti akahalalisha jambo hilo kama ni demokrasia, kwa kweli hiyo ni ishara mbaya mno.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vilevile ni dalili mbaya pale wakuu wa chama hicho na haswa wazee wa busara waliokuwa katika makuzi ya siasa asilia za chama hicho na wengine kushiriki katika ujenzi wake wanapokuwa tayari kuweka kando maslahi ya watanzania kwa ujumla na kujali ushindi wa chama tu kama dira yao kuu ya kufanya maamuzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ushindi ambao kwao wao ni muhimu tu kutokana na uhakikisho wa kuwa wao na vizazi vyao vitaendelea kuwa madarakani daima milele hata kama ishara zinaonyesha kupotea kabisa kwa utaifa wetu ambao ndio umekuwa nguzo yetu muhimu kama nchi na jamii staarabu.&lt;br /&gt;Kwa ujumla ingawa wengi wanaamini kuwa chama cha mapinduzi kimeweza kuvuka mtihani mkubwa kwa ushindi, ni wazi kuwa ushindi huo unaendana na kujisimika rasmi kwa siasa mpya zisizojali misingi na falsafa asilia za chama hicho ambazo kwa kweli ndizo zimekuwa nguzo kuu za kuendelea kwa uimara wake wakati wote huu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siasa hizi mpya ambazo zinalenga wingi wa kura tu na sio mipango madhubuti ya muda mrefu yenye kulenga kustawisha jamii kwa mapana na marefu daima haziwezi kuifanya CCM kuendelea kuwa chama cheney mvuto asili ambo hata kama mambo hayaenda sawa wananchi wataendelea kukiamini na kikihamini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siasa hizi zinazofuata mbinu za soko huria ambazo zinalenga kumnadi mtu kama bidhaa nyingine sokoni zinafanya chama hicho kutegemea uhalali wa umaarufu wa mwanasiasa huyo tu na sio mapenzi na imani juu ya chama hicho.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bahati mbaya umaarufu huu unajengwa na matarajio hewa ndani ya mioyo ya wananchi, ambayo ama kwa mapungufu ya kiutendaji ya mwanasiasa huyo au ya kimfumo ni vigumu kuyafanikisha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo basi kukifanya chama hicho kuwa mateka wa mwanasiasa huyo na wajanja wachache waliomzunguka wanye uwezo wa kucheza na akili za wapiga kura kwa muda Fulani tu. &lt;br /&gt;Hawa huwezesha hilo kwa kutumia mbinu mbalimbali za kihadaa ambazo daima huishia ama kuvuruga jamii au kuchokwa na wapiga kura.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapo wanaofikiri kuwa kupatikana kwa mgombea na baadaye kiongozi mwenye mvuto kama aliyechaguliwa hivi karibuni kuwa ni silaha muhimu ya kuhakikisha uimara wa chama hiki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mimi nasema ndio lakini ni kwa muda mfupi tu na hiyo hiyo ndiyo silaha ya kujiangamiza kwa muda mrefu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni dhahirikuwa ushindi uliopatikana Dodoma hivi karibuni ni mwanzo wa safari isiyo rasmi ya mwisho ya chama cha mapinduzi.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-3623841977806449936?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/3623841977806449936/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=3623841977806449936' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/3623841977806449936'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/3623841977806449936'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2007/08/mwanzo-wa-safari-ya-mwisho-ya-ccm.html' title='MWANZO WA SAFARI YA MWISHO YA CCM'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-1630126124685849844</id><published>2007-08-02T10:43:00.000-07:00</published><updated>2009-09-05T12:17:24.119-07:00</updated><title type='text'>NINI FALSAFA YA MAPINDUZI YA CHIMWAGA 2005?</title><content type='html'>@2005..Published by Mtanzania Jumapili soon after CCM nomination process.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya miaka mingi ya Chama Cha Mapinduzi kudorora na kukosa chachandu zinazoendana na jina lake hatimaye katika hali ya kustajabisha kabisa Mapinduzi mengine ya ndani yametokea. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni ukweli usiofichika kuwa moja ya mbinu iliyotumika katika kuhakikisha kuwa mheshimiwa/ndugu Jakaya Kikwete anashinda mchakamchaka wa kuchaguliwa kugombea urais ndani ya Chama Cha Mapinduzi, ni kauli mbiu inayosema ARI MPYA, KASI MPYA NA NGUVU MPYA.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;kini kubwa zaidi ni kuwa kauli mbiu hii ilikuwa na bado inaendelea kuashiria kufanyika kwa mapinduzi makubwa ndani ya CCM. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mapinduzi ambayo kwa kiasi fulani yamefanikiwa ingawa mengi bado yatakiwa kufanyika.&lt;br /&gt;Katika siku za hivi karibuni kumekuwa na kukua kwa mtindo wa vijana wengi wa kizazi kipya kuvaa fulana zenye picha za viongozi mbalimbali duniani ambao wamekuwa wakihusishwa na mapambano mbalimbali ya kimapinduzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miongoni mwao, picha ya Hayati Ernesto Che Guevara ndio imekuwa maarufu zaidi kama ilivyo katika jamii zengine za vijana katika nchi mbalimbali duniani.&lt;br /&gt;Kwa wale wasiomjua Che Guavara, huyu ni mwanamapinduzi mwenye asili ya nchi ya Argentina kule Amerika ya kusini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwanamapinduzi huyo amefanya mengi katika kupigania kuundwa kwa jamii isiyo na matabaka na inayoheshimu thamani ya utu wa kila mtu.&lt;br /&gt;Katika jitihada zake hizo ambazo zilikuwa zikiongozwa na dira ya falsafa ya mapinduzi ya kijamaa, Che Guevara alijitolea muhanga maisha yake kwa kuwa mstari wa mbele katika mapambano ya ukombozi kuondoa tawala mbalimbali  za kibepari uchwara katika pande zote za dunia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni yeye ndiye akiwa begabega kwa bega na kiongozi wa CUBA, Mwanamapinduzi Fidel Castro, mnamo maka 1959, aliongoza majeshi ya walalahoi wa nchi hiyo kuuteka mji wa Havana na kusimika utawala wa kimapinduzi wa kijamaa unaotawala hadi hivi sasa. &lt;br /&gt;Ni Che ndiye aliyeamua kuacha maisha ya anasa ya kuwa waziri muhimu katika seriakali ya CUBA na kuja afrika kusaidiana na wanamapinduzi kadhaa kama Mzee Ben Bella wa FNL ya Algeria. Baadaye alijipenyeza hadi Kigoma, Tanzania alikokwenda kusaidiana na Marehemu Mzee Kabila wa DRC.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Wakati huo Mzee Kabila alikuwa akiongoza kikundi cha wanamapinduzi wanaofuata falsafa za kijamaa waliokuwa wakijaribu kurudisha madarakani mabaki ya utawala wa mwanamapinduzi mwengine, Hayati Patrice Lumbumba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya hapo, Che alienda nchi zengine zilizokuwa zikikabiliwa na unyang’au wa tawala za kibepari ambazo zilikuwa zikiongozwa na viongozi vibaraka wa Marekani, akiwa na mkoba wake uliojaa fikira za kimapinduzi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maisha ya mwanamapinduzi huyu  yaliishia mikononi mwa mawakala wa shirika la ujasusi la marekani CIA waliokuwa wakisaidia kuulinda utawala wa kinyang’au wa René Barrientos huko Bolivia, amerika ya kusini. Inasemekana kuwa picha ya sura ya Che Guevara ndio picha maarufu zaidi ya binadamu yeyote kuchapwa katika vitu mbalimbali duniani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mimi ni moja wa vijana ambaye nimetokea kuvutiwa sana na kuvaa fulana zenye picha za wanamapinduzi hawa akiwe,o Che Guevara na kwa kweli huwa najisikia vizuri sana ninapokuwa katika vazi hilo.Lakini tofauti na mimi ambaye nilianza kuvaa fulana zenye picha za wanamapinduzi hawa mara baada ya kusoma vitabu mbalimbali. &lt;br /&gt;Wengi wa vijana wenzangu nchini wamekuwa wakivaa mavazi ya aina hii bila hata kujua mtu huyo wanayemshabikia ni nani na ni nini alichokuwa anakiamini na kukisimamia katika maisha yake.Wengi hawajui kabisa ni falsafa gani ambayo Che Guevara alikuwa akiamini na jinsi gani alivyokuwa akichukia kwa ukweli kabisa madhila yaliyokuwa yakimsulubu mwanadamu yeyote yule katika pande zote za dunia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hali kama hii imekuwa ikionekana katika kinyang’anyiro cha na nafasi ya kugombea urais ndani na nje ya CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika CCM kwa miaka kadhaa sasa kumekuwa na mabadiliko ya sura katika ngazi za uongozi wa chama hicho kuanzia kata hadi Taifa. Kuna wakati mabadiliko haya yalikuwa na baraka zote za viongozi wa chama hicho haswa wale wazee kama “Komredi” Kingunge Ngombale Mwiru, Mzee Rashid Kawawa, Mzee John Malecela na wengineo.&lt;br /&gt;Kwao wao waliamini kwa dhati kuwa damu mpya inahitajika ili kuhakikisha kuwa chama kinaendelea kuwa na ushawishi mkubwa ndani ya jamii ya watanzania ambayo vijana ndio wawakilishi wakuu.&lt;br /&gt;Bahati mbaya wazee hawa hawakuweka wazi vijana wa aina gani wanaotaka wao waaminiwe na kukabidhiwa dhamana ya kuwaongoza wenzao. Kosa ambalo sasa limewafanya wao kujikuta na mtihani mgumu wa kuamua ni nani haswa anapaswa kuaminiwa kupewa nafsi ya kuwa rais wan chi yetu kwa miaka mitano au kumi ijayo.Mtihani ambao ulihitimishwa kule Dodoma wiki iliyopita ambapo kwa kweli waliweza kuushinda kwa busara za hali ya juu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kweli mimi kama kijana ningelipenda kuona mapinduzi haya yakitokea ndani ya chama hiki ili kukipa nguvu mpya na uhalali wa kutosha kutawala kwa ufanisi zaidi.&lt;br /&gt;Lakini tatizo linakuja pale ambapo ninapoona kuwa dhana ya mapinduzi ndani ya chama ambayo hawa “vijana” wenzangu wanajaribu kuionesha inakuwa imekosa kiungo kikubwa muhimu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kiungo ambacho ni lazima kuwepo ili mapinduzi yeyote yale ya kisiasa au kijamii yawe yana manufaa kwa mwanachi wa kawaida aliyezingukwa na madhila yasiyo na kifani.&lt;br /&gt;Kiungo hiki ni kuwepo kwa falsafa itakayoongoza mapinduzi hayo wakati wa kufanyika na baada ya kufanikiwa kubadili mfumo wa uongozi uliopo katika chama cha mapinduzi.&lt;br /&gt;Siasa za kimapinduzi za mwalimu Nyerere ziliongozwa na fikira za mzee wetu huyu ambaye kwake aliheshimu kila mtu bila ya kujali kipato chake, kabila lake, rangi yake, elimu yake ama utashi wake kisiasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Fikira hizi zikiongozwa na kanuni binafsi za mwenendo wa kimaisha wa kiongozi huyu wetu mpendwa zenye kuendeshwa na maadili bora ya kiuongozi ndizo zilizopelekea kutangazwa kwa Azimio la Arusha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni azimio la Arusha ndilo lilionyesha wazi nafasi ya falsafa ya ujamaa na kujitegemea ambayo ndiyo iliyongoza mapinduzi ya kisiasa, kijamii na kiuchumi ndani na nje ya chama cha TANU na baadaye CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bahati mbaya tofauti na mapinduzi ya wakati huo, mapinduzi tunayoshuhudia sasa kwa kweli yamekosa kabisa kuweka wazi falsafa ambayo inaonyesha kuwa ni mapinduzi yanayolenga masilahi za mtanzania wa kawaida na sio vinginevyo.&lt;br /&gt;Hivi karibuni niliweza kupata habari nyeti ambazo zilikuwa zikionyesha wazi ni wajumbe gani ndani ya halmashauri kuu ya CCM ambao wanatambulika kama wafuasi wa mapinduzi haya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kweli ukiangalia hao wafuasi tuu ni dhahiri kuwa wengi wao si tu wamekosa utashi wa dhati wa kimapinduzi lakini zaidi hata upeo wao wa siasa za kimapinduzi ni mdogo mno.Wengi wao katika maisha yao ya kawaida wameonyesha kuwa makuwadi wakubwa wa siasa za kibepari uchwara zenye kujali maslahi binafsi. Wengi wao kwao ukombozi wa mtanzania wa kawaida utatokea pale tuu wao na washirika wao wachache watakapoweza kupata madaraka zaidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wao ni walokole wa dhana mpya ya utajirisho inayojikita katika nchi yetu. &lt;br /&gt;Dhana ambayo inaelezea kuwa dawa ya umasikini katika nchi yetu ni kuwaacha wao wachache wenye nafasi katika uwanja wa siasa na maharamia wenzao waruka kodi watajirike zaidi bila kujali maslahi ya walio wengi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kweli dhana hii ndio inayoendesha fikira za ndugu zangu hawa waliojivika kilemba cha uwanamapinduzi. Uwanamapinduzi unaodai kulenga ukombozi wa mimi na wewe na yule.&lt;br /&gt;Si bure kwao wao kuyachukulia mapinduzi yao ni ya kirika na kamwe si kifikira.&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Kama ni fikira za umimi na usisi zenye kusadifiwa na falsafa ya ubinafsi ambayo sidhani kama ni falsasfa muafaka ya kuwasaidia watanzania walio wengi ambao kwao wao tatizo si sura bali mfumo mzima wa kisiasa uliowazunguka. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tatizo la wanamapinduzi hawa wa karne mpya ni kuwa wengi wao na zaiid wale walio karibu zaidi na chaguo lao wamekosa utashi wa kujiendeleza kifikra kwa kukosa ustarabu wa kujisomea.Wengi wao hawana tofauti na vijana wenzangu niliowaelezea hapo juu ambao wanavaa fulana na nembo zinazonyesha wanamapinduzi mbalimbali bila hata kujua nini watu hao walikuwa wakisimamia&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hawa ni wanamapinduzi wa CNN, BBC na MNET ambao kwao wao shule pekee ya kimapinduzi ni ile wanayoiona katika vyanzo hivi vya habari vikionyesha kinachoitwa “mapinduzi” mbalimbali yanayotokea katika nchi za Ulaya ya mashariki na kati.Hawajui kwamba mapinduzi haya hayana tofauti na mapinduzi kibwanyenye yaliyotokea Uingereza, Ufaransa, Marekani katika karne kadhaa zilizopita ambayo badala ya kumkomboa mwananchi wa kawaida kutoka katika unyang’au wa kikabaila, yalisimika makabaila wapya katika sura ya ubinafsi wa kibepari.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbaya zaidi ni kuwa tofauti na mapinduzi hayo ya kibwanyenye ambayo yalikuwa na mwongozo wa kifalsafa uliojengwa na ujuzi wa kisayansi, mapinduzi haya ya “vijana wa CCM” yamekosa ufanisi wa kisayansi na kielimu ambo ungeweza kujenga falsafa bora na makini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wengi wa wahubiri wa mapinduzi haya hawana elimu wala uzoefu ya kutosha ya siasa za kidunia ambazo zingeliwawezesha kuwa na dira imara ya kulinda mapinduzi hayo mara baada ya wao kuweza kutwaa madaraka ya dola.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na wale walioweza kubahatika kujua umuhimu wa hilo kutokana na elimu kubwa waliyonayo wengi wao wamechoka kifikira na wameamua kusalimisha silaha zao na kujitwika majoho ya ubinafsi wakisema kubali yaishe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wao (wasomi wachache walio katika kundi hili) wamechoka na dharuba za kimaisha wanazozipata kuotokana na misimamo yao iliyokuwa ikilenga jamii bora zaidi.&lt;br /&gt;Wameamua kujiunga na timu ya ushindi na kusema kubali yaishe, bora hichi kidogo kuliko kuendelea kukosa kabisa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa kifupi wote kwa pamoja wanaamini kuwa ili kurekebisha mambo kwa haraka zaidi ni bora kuja na dhana ya mapinduzi ya kirika yenye kulenga mbadiliko wa kisura katika nyanja za utawala bila ya kujali nafasi ya fikira mbadala katika mapinduzi hayo.&lt;br /&gt;Fikira ambazo zinaonyesha umakini wa kiongozi wa mapinduzi hayo ambaye daima ndiye anayetakiwa kuhodhi mawazo dira ya mapinduzi hayo na yeye mwenyewe kuweza kuyauza kwa walengwa ili kupata uhalali wao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inapotokea kuwa kiongozi wa mapinduzi hayo anakosa au anashindwa kuweka wazi fikira za kiuanamapinduzi zenye kujengwa na kulindwa na fasafa makini ya ukombozi wa kweli, basi hizo ni dalili mbaya za matokea ya mapinduzi haya.Na inapotokea kuwa kiongozi wa mapinduzi hayo anakuwa amezungukwa na manyang’au wenye uchu tu wa madaraka na utajirisho wao binafsi. Waliojaa kashfa za kuwadhulumu wananchi wa kawaida basi hiyo ni dalili ya hatari kubwa zaidi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata kama kiongozi huyo amekuwa akilelewa kifikira tangia ujana wake, mazingira kama yaliyomzunguka kiongozi wa mapinduzi haya yanaonyesha uwezekano tofauti kidogo.&lt;br /&gt;Uwezekano ambao historia za nchi kadhaa zilizowahi kufikwa na hali hiyo zinaonyehsa jinsi gani mapinduzi kama haya yameweza kupelekea kueseka, kuabika, kunyanyasika na kuuawa kwa mamilioni ya hao waliokuwa wakidhani wanapiganiwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini yote haya yanatokea na makosa waliyofanya wazee hawa wa CCM ambao kuanzia miaka ya mwanzo ya tisini wamekuwa wakiruhusu kila mtu kuingia katika ngazi za uongozi za chama hicho. Bila ya kujali utashi wake wa kuwahudumia wananchi na sio kujihudumia yeye binafsi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mbaya zaidi inakuja pale ambapo chama hiki kilipoondoa umuhimu wa elimu ya maadili na ya kifalsafa ambayo hapo mwanzo kila anayejiunga na chama hicho na haswa vijana alipaswa kipitia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Makosa haya yote na lile la chama chenyewe kukosa mwelekeo wa kifalsafa zaidi ya falsafa ya ubinafsi ndivyo vimepelekea chama hiki kujikuta njia panda katika kuamua kama jee mapinduzi ya aina hiyo ni ya muafaka au la.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mungu ibariki Tanzania&lt;br /&gt;Mungu ibariki afrika&lt;br /&gt;Mapambano daima.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-1630126124685849844?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/1630126124685849844/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=1630126124685849844' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/1630126124685849844'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/1630126124685849844'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2007/08/nini-falsafa-ya-mapinduzi-haya.html' title='NINI FALSAFA YA MAPINDUZI YA CHIMWAGA 2005?'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-5864551195441062226</id><published>2007-08-02T10:40:00.000-07:00</published><updated>2009-09-05T12:20:56.848-07:00</updated><title type='text'>MPAMBANO KATI YA SIASA ZA UMAARUFU, UHAFIDHINA NA UMAKINI NDANI YA CCM: NINI HATMA YA MTANZANIA.</title><content type='html'>@2005..Published by RAI&lt;br /&gt;NA ILYAS, O. S&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ilikuwa miaka, ikaja miezi na sasa imebakia wiki moja tu watanzania wachache watukufu katika ulingo wa maamuzi ya nchi wakutane kule Dodoma katika madhabahu makuu ya siasa nchini kuamua ni nani anapewa nafasi ya kugombea ubwana mkubwa wa nchi yetu kwa tiketi ya kile kinachoitwa chama cha mapinduzi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mimi kama mtanzania mwanachama wa chama kinachoitwa TANZANIA kinachofuata imani ya MWAMKO WA UAFRIKA naamini ni wajibu wangu kuchambua na kuelezea yale ninayoyaona yakiendelea na yatakayoendelea wakati na baada ya uchaguzi huu bila ya woga na hata kama nafasi yangu kubadilisha mawazo ya ndugu zangu wa CCM ni finyu mno.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chama cha mapinduzi kama yalivyo makundi mengine yenye nia ya kuwa na uwezo wa kisiasa na kikatiba kushikilia mihimili ya nchi inayotoa na kuelekeza maamuzi ya kisiasa, kiuchumi na kijamii katika dola lolote, daima huwa katika mivutano ya hapa na pale inayoletwa na tofouti mbalimbali miongoni mwa wanakundi hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mivutano hiyo inaweza kuwa ya kifikira, kiutashi, kimuono ama kimaslahi. Mivutano hiyo inaweza kuwa ya siri ndani ya wanakundi pekee, inaweza kuwa inatokana na mawazo ya wanakundi pekee au kama ilivyo sasa kwa CCM ikawa ya wanakundi wakishirikiana, kuhusisha au kuendana na mawazo ya wasio wanakundi kutoka ndani au nje ya mipaka ya nchi yetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa miaka kadhaa sasa kumekuwa na mabadiliko makubwa yakiendelea ndani ya kundi hili linaloitwa Chama cha Mapinduzi. Mabadiliko ambayo yanalenga kulifanya kundi hili kuendana na fikra za baadhi ya wanakundi hilo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanakundi ambao wanadhani kuwa fikra zao ni bora zaidi kwa maslahi ya nchi na wananchi wake, chama na wanachama wake na vilevile maslahi binafsi ya baadhi ya wanakundi hili ambao nao wamejenga vikundi uchwala vyenye lengo la kufanikisha fikira zao, utashi wao, muono ama maslahi yao binafsi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ili hilo lifanikiwe wanakundi hawa wamekuwa wakitumia mbinu mbali mbali halali na haramu kufanikisha mapambano au mikakati yao dhidi ya fikira na muono tofauti wa wanakundi wenzao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baadhi ya mbinu  ni kama kuanzisha vikundi uchwara ndani kundi kuu yaani CCM, kushirikiana na wanambinu mbalimbali kama vile wasomi, waandishi wa habari, viongozi wa kijamii, vyombo vya dola na hata wafadhili kutoka ughaibuni kueneza, kuzipamba na kuzilinda fikra zao kwa wananchi ili waweze kupata uhalali rasmi kutoka kwao.&lt;br /&gt;Lakini ili hili lifanikiwe ni lazima waweze kushika hatamu za madaraka ya dola kwa kumweka yule wamuonaye ni chaguo bora kuwaongoza katika kufanikisha utekelezaji wa fikra na maslahi yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa ndipo tunapokuja katika umuhimu wa suala zima la mbio za kugombea nafasi ya urais wa Tanzania kupitia kundi kuu la CCM na baadaye uongozi mkuu (uenyekiti) wa kundi hilo kama taratibu walizojiwekea ndugu hawa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upeo wa uchambuzi wangu wagombea wote wa CCM wanawakilisha makundi makuu matatu. La kwanza ni lile linawakilisha fikira za siasa za umaarufu, la pili ni lile linalowakilisha wanakundi wenye kuamini siasa za kihafidhina na la tatu ni lile linaloamini umuhimu wa siasa za umakini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ingawa kuna wagombea zaidi ya kumi lakini ukweli ni kuwa wote hawa ni wawakilishi wa moja ya makundi haya ambayo yana wagombea halisi na wagombea vivuli.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa wale waliosoma makala yangu iliyopita niliyoiita KIKWETE CHAGUO MAARUFU, SALIM CHAGUO MAKINI ni wazi wameshajua viongozi wa makundi mawili. Kundi la tatu ni lile linaloongozwa na mgombea mwingine machachari ndugu MALECELA.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wengi mnaweza kudhani kuwa chimbuko la makundi haya ni miaka miwili au mitatu ya hivi karibuni. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;La hasha, chimbuko hasa la siasa hizi za kimakundi ni miaka ya mwanzo ya themanini ambapo hata kama mimi binafsi nilikuwa mdogo sana kwa umri, lakini utundu wangu wa kuhoji uliweza kuniangaza na kung’amua mwanzo wa mwisho wa CCM imara na hata Tanzania ya amani tuliyokuwa tunajivunia popote pale duniani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chimbuko hili mimi naliita chimbuko la falsafa ya UNYANG’AU iliyozaliwa rasmi kule katika visiwa vilivyokuwa vikijulikana duniani kote kama vya marashi ya karafuu na sasa vinaelekea kupata umaarufu wa kufananishwa na marashi ya damu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi ni visiwa vya Zanzibar ambako ndipo ule mkutano maarufu wa wateule wa mtetezi wa kweli wa siasa za upendo, heshima, maadili na umoja kwa jina la siasa za Ujamaa, waliamua kukaa chini na kuondokana na kile walichokiona ni ushamba wa kifikira wa hayati mzee wetu, Mwalimu Nyerere. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hili sio lingine bali ni azimio la Zanzibar la mwaka 1986 ambalo pamoja na mambo mengine liliondoa nguzo muhimu za uimara wa jamii yetu zilizokuwa zikisisitiza maadili ya kiuongozi na siasa nadhifu zenye kulinda na kupigania maisha mema kwa wote bila ya kujali hali ya kimaisha, nafasi ya kisiasa au kidola, tofauti za kidini na kabila au asili ya mtanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Falsafa hii ya unyang’au ndio iliyozaa makundi makuu mawili yaani kundi la siasa za kihafidhina na kundi la siasa za umaarufu. Matokeo ya kuchipua, kujikita na sasa uwezekano wa kushika hatamu kwa siasa hizi ndizo zilizopelekea kuzindukana na kutahayari kwa kundi la siasa za umakini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni wazi kuwa miongoni mwa wana makundi haya ndani ya CCM kwa njia moja au nyingine wameshiriki katika ile hafla ya kuzaliwa rasmi kwa falsafa ya unyang’au kule Zanzibar. Ama walikuwa miongoni mwa waliosimamia kupitishwa kwake au walikuwa katika nafasi ya utazamaji tu wakidhani kuwa wao ni vichuguu wasingeweza kupambana  na mibuyu ya wakati huo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini vilevile inawezekana walidhani kuwa zoezi hilo lilikuwa ni la busara ambalo kwa mahesabu yao lingewawezesha kuondokana na umasikini mali uliokuwa ukiwakumba wakati huo ambao kwa mtazamo wao ni falsafa za siasa za ujamaa ndizo zilikuwa chanzo kikuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Miaka kadhaa ya majaribio ya falsafa hii ya unyang’au ilipeleka baadhi ya wanakundi kuu kuanza kujiuliza kama falsafa hii ni bora na zaidi ina mnufaisha nani. Hapa ndipo lilipoibuka kundi la siasa za uhafidhina ambalo lilinza kujijenga na kujipanua katika miuondo mbinu yote ya kiutawala ili kuhakikisha kuwa falsafa hii ambayo iliweza kuwaonyesha nuru yao kimaslahi inabaki kutawala taifa letu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kundi hili lilitumia mbinu mbali mbali hata ikafikia wakati likawa tayari hata kuvunja muungano wa nchi yetu ilimradi kuondokana na kanguvu cha ajabu cha baba wetu wa taifa aliyeweza kung’amua hatari ya kusimikwa kwa falsafa hii ya unyang’au kwa kusingizia Utanganyika na Uzanzibari. Baba wa taifa alijaribu kupinga safari hiyo ya wahafidhina waliokuwa wakijaribu kushikisha hatamu kwa falsafa yao ya unyang’au wakati huo. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Upinzani ambao aliweza kuendeleza hadi katika uchaguzi wa mwaka 1995 lakini bila ya kujua akapigwa chenga ya mwili na wajanja wajanja wachache walioweza kumlaghai kuwa wao wana dawa ya tatizo lilikuwa likimuumiza kichwa chake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Matokeo yake hadi mzee wetu huyu alipoelekea dunia nyingine ambako hivi sasa nina uhakika amekuwa BIZE akipokea ripoti mbalimbali za hali mambo hapa kwetu kwa wajumbe waliomfuata hivi karibuni, Unyang’au umeendelea kishamiri na hivi sasa unajaribu kushika hatamu kwa sura mbii tofauti.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kushamiri kwa unyang’au na uwezo wake wa kuamsha chuki za kimfumo miongoni mwa watanzania wengi kumepelekea kuibuka kwa kundi la siasa za Umaarufu katikati mwa miaka ya tisini kama fikra mbadala za uny’angau uliokuwa ukiendeshwa na kulindwa na wanakundi la kihafidhina.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ama kwa uchungu wa nchi yetu na watu wake (fikira ambayo najaribu kuendelea kuiamini ingawa mengi yananielekeza tofauti) au kwa POLITICAL OPPORTUNISM, kundi la siasa za Umaarufu limeweza kuibuka ndani ya kundi kuu na kujaribu kuonyesha kuwa lenyewe linaweza kumalizia kazi aliyoianza baba wa taifa ya kuondoa unyang’au na manyanga’au wote kutoka katika mihimili ya kisiasa na kidola nchini mwetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kundi hili lilibahatika kupata baraka za wananchi wengi waliochoshwa na madhila ya unyang’au huu ambao umeleta umasikini na aibu za kimaisha zisiso na kifani miongoni mwa watanzania walio wengi. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni ukweli usiofichika kuwa kundi hili ambalo lilikuja usoni mwa watanzania wakati wa uchaguzi wa mwaka 1995 na kuzuiliwa kitaalamu na mwalimu Nyerere ambaye aliamini kuwa halijawa tayari kukabidhiwa majukumu makubwa ya kuongoza nchi yetu, lilikuwa limesheheni vijana wachache ambao ni wazi walikuwa na uchungu mkubwa kwa nchi yetu.&lt;br /&gt;Kwa bahati mbaya manyang’au wachache waliona hatari ya kundi hilo mbeleni hivyo kwa mwendo wa taratibu wakaanza kujipenyeza ndani ya kundi hili na hatimaye kushika miundo mbinu yote ya kisiasa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Manyang’au hawa ambao walijuwa wazi kuwa kamwe hawataweza kufanikisha ndoto yao ya kushika hatamu za kiutawala za nchi hii na hivyo kurutubisha neema zao bila ya kujipenyeza katika kundi hili. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wao walijuwa wazi kuwa kutokana na laana ya wazi ya baba wa Taifa aliyolipa kundi la siasa za kihafidhina, laana ambayo alikuwa akiendelea kuisisitiza hata katika matamshi yake ya mwisho kabla ya kukatwa kauli, kamwe wateule wao wasingekuwa na nafasi ya kushika hatamu ya taifa letu na kundi kuu yaani CCM hapo baadae.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hawa waliamua kuelekeza nguvu zao kwa mteule wa kundi la siasa za umaarufu wakijua kuwa kama watafanikiwa kushika hatamu za madaraka nchini na ndani ya CCM wataweza kuendeleza unyang’au wao kwa mgongo wa mteule wa kundi la siasa za umaarufu aliyetokea kuwa maarufu na hivyo kwa mawazo yao ni rahisi kushinda jaribio la ugombea wa urais wakati huu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa bahati mbaya ama kwa kudhani kuwa ni uamuzi sahihi, mteule wa kundi hili linaloamini siasa za umaarufu zenye mlengo wa kile kinachoitwa utawala mpya na mawazo mapya, amewaachia manyang’au hawa nafasi kubwa katika mkakati wake za kuchukua madaraka ya nchi yetu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndio maana imefika wakati watanzania kwa namba inayokuwa kila kukicha kuanza kuhoji kama kweli hata yeye binafsi ni suluhisho la madhila yanayowakumba na kama kweli anaweza kuundoa falsafa ya unyang’au wakati amekuwa akiwategemea manyang’au na kuachia mbinu za kinyanga’au kutawala mkakati wake kile wanachidai wa kujenga historia mpya hapa nchini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na mambo mengine, kutokana na hali hii ndipo likazuka kundi lingine ambalo ni dogo mno kwa hesabu lakini kubwa kwa kimkakati ambalo linadhani kuwa ni siasa za kanadhifu na kimaadili pekee ndizo zinaweza kutimiza ndoto za mwisho za baba wa Taifa za kuondokana na falsafa hii ya kinyang’au katika kundi kuu, yaani CCM na hivyo Tanzania kwa ujumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kundi hli ambalo linajumuisha watu mashuhuri ambao baadhi yao walikuwa na nafasi katika tawala mbili za mwanzo za taifa letu pamoja na wanasiasa wapya wenye kukerwa na mambo na msuguano wa makundi mengine mawili limejikita chini ya mgombea wamuonaye makini zaidi yaani Dr Salim.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwao wao wanadhani uzoefu, ustaarabu, umakini na uaminifu wa kimaadili alio nao mgombea huyu ambaye kwa mara kadhaa marehemu baba wa taifa alipendelea awe mrithi wake wa uongozi wa siasa zake za Kinadhifu, kiupendo na kimaadili, ndio kweli unaweza kutuepusha na madhila ya unyang’au. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Madhila ambayo kama wao hawatafanikiwa yanaweza kuongezeka zaidi endapo waumini wa falsafa hiyo ya unyang’au ndani ya kundi lao la CCM wataweza kushika hatamu ama wao binafsi au kwa kutumia mgongo wa kiongozi mwingine.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kundi hili linaamini siasa makini ndizo kama ndio silaha muhimu ya mwisho ya kunusuru ya kundi lao kuu (CCM) na Taifa letu na vilevile hatma ya watanzania kwa ujumla. Linaamini kuwa siasa za umakini zenye kuendeshwa na uaminifu wa uongozi wa kimaadili na wenye kung’amua hasara za siasa za kihafidhina na umaarufu sio tu unaweza kuondoa madhila ya unyang’au unao ota mizizi katika jamii yetu lakini vilevile kuepusha janga linalotujia mbeleni kutokana na msuguano wa hayo makundi mengine mawili.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika mtazamo wangu ninaamini kuwa angalao kundi hili ndilo linaloweza kutuokoa watanzania na kitimtimu kilichoko mbeleni cha wanamakundi mawili ya umaarufu na uhafidhina ambayo kwa kweli pamoja na mapungufu mengine yameonyesha chuki na uadui mkubwa ambao ni dhahiri ndio utakawo kuwa dira ya ama wateule wao wakuu au wateule wao vivuli watakaposhinda mpambano huu haramu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sio tu kwamba itawabidi kusafisafisha wale wanaodhani wanatofautiana na kifikira na kiutashi kuhusiana na vipi nchi yetu iendeshwe lakini vilevile ni dhahiri watalazimika kuwandoa au kuwanyamazisha wale wote waliokuwa wakiwaona ni maadui zao na pengine wakawa kikwazo kwao kufanikisha yale yaliyopelekea wao kuamua kupigania nafasi hiyo ya juu ya kimaamuzi ndani ya chama na jamii kwa ujumla endapo watashika hatamu zote zikiwemo za dola.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mimi kama nilivyodokeza hapo juu sina mahusiano ya ki-uwanachama na kundi hilo kuu linalojiita la chama cha mapinduzi hivyo kwa kile tunachosema ni kawaida isingenipasa kuingilia mpambano wa ndugu zangu hawa wa CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini nikiwa kama mtanzania na muafrika ninayeamini amani na upendo kama nguzo kuu za uanadamu na mwenye uchungu na nchi yangu hii ninamuomba mungu asikie vilio vya wengi vya kuwaamsha baadhi ya wapiga kura ndani ya CCM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndugu zetu ambao wamegubikwa na ushabiki na tama ya maslahi binafsi waweze kuzinduka na kuona umuhimu wa umakini katika kufikia uamuzi wao wa mwisho ili kuliepesha taifa letu na janga lunalotujia. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Janga la muendelezo wa falsafa ya unyang’au, ama kwa sura ya sasa ama sura, ambayo kwa muda wa sasa ndio imekuwa rutuba bora ya machafuko na ukosefu wa amani kwa taifa letu na hata majirani zetu. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatma ya watanzania ipo mikononi mwa ndugu hawa wachache ambao mpaka sasa wameweza kufanikiwa kutwaa utukufu wa kidunia wa kuwawezesha kutuamulia watanzania milioni 36 ni nani atakeyekuwa ameshika uhai wetu wa kifikira na kibailojia kwa miaka mitano ama kumi ijayo.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-5864551195441062226?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/5864551195441062226/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=5864551195441062226' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/5864551195441062226'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/5864551195441062226'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2007/08/mpambano-kati-ya-siasa-za-umaarufu.html' title='MPAMBANO KATI YA SIASA ZA UMAARUFU, UHAFIDHINA NA UMAKINI NDANI YA CCM: NINI HATMA YA MTANZANIA.'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-5767072575557432320</id><published>2007-08-02T10:37:00.001-07:00</published><updated>2007-08-02T10:37:54.016-07:00</updated><title type='text'>BARUA WAZI KWA WAPIGA KURA WA CCM..</title><content type='html'>@2005..published by RAI&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndugu watanzania wenzangu,&lt;br /&gt;Kwanza hongereni kwa kuweza kuwa miongoni mwa watanzania wachache ambao mungu amewajalia kuwa na nafasi ya juu kabisa nchini mwetu ya kuamua ni nani anakuwa kiongozi wa nchi yetu kwa miaka mitano au kumi ijayo.&lt;br /&gt;Vilevile nawapongezeni kwa kuwa wavumilivu wa madhila ya usumbufu wa hali ya juu kutoka kwa wale wanaowakilisha maslahi ya wakubwa wenzenu wanaotaka kuingia ikulu kwa makeke ya karne.&lt;br /&gt;Ndugu zangu mimi si mwanachama wa chama chenu kitukufu lakini kama mtanzania ninayejua wajibu wangu najua umuhimu mlio nao wakati huu katika kuamua maslahi yangu, ya ndugu zangu na watanzania wenzangu wote kwa ujumla.&lt;br /&gt;Ninajua kuwa chaguo lenu ndilo litakalofanikisha au kuvuruga ndoto zangu nyingi kuhusiana na nchi yangu na bara langu nilipendalo la Afrika.&lt;br /&gt;Ninajua kuwa ufunguo wa chembe ya uhuru ninayo jivunia hivi sasa na nikaweza kukaa hapa nilipo na kuandika barua hii kwenu mnao ninyi na ni ninyi ndio mtakaoamua kama nitaendelea kuwa nao hata baada ya usiku wa tarehe nne mwezi ujao.&lt;br /&gt;Ninajua kuwa ni ninyi wenye kushika mstakabali wa maisha yangu ya upendo na uvumilivu kwa watanzania wenzangu ambao daima nimekuwa nikiwapenda bila ya kujali dini zao, makabila yao, rangi zao ama hali zao za kimaisha.&lt;br /&gt;Ninajua kuwa kura zenu mtakazopiga wiki ijayo ndizo zitakazoamua kama na mimi nitabahatika kuoana na nimpendaye na kuzaa naye watoto wazuri watakaojivunia na Tanzania nitakayowachia.&lt;br /&gt;Ninajua kuwa wengi wenu tayari mmeshamua ni nani mngependa awe rais wa nchi yetu ama kutokana na mvuto wake, ukaribu wake nanyi, umaarufu wake, ucheshi wake, unyenyekevu wake na hata uchapakazi wake mnaodhani kuwa ni muhimu kwa uongozi wa nchi yetu kuondokana na hali tuliyonayo sasa.&lt;br /&gt;Ninajua kuwa wengi wenu mnadhani kuwa ni lazima kulipa fadhila kwa wale waliofanikisha ninyi kupata nafasi hii hata kama kwa masharti ya kudhalilisha kama kulazimika kumpigia kura mgombea wa yule aliyekusaidia kufanikisha mambo na wewe ukapata nafasi uliyona nayo.&lt;br /&gt;Ninajua kuwa wengi wenu mna deni la kulipa kutokana na misaada mbalimbali kama vile kumlipia mwanao ada ya shule, kulipia matibabu yako au ya mpendwa wako wakati akiumwa, au kukupa nafasi ya kwenda kusoma elimu ya juu ama pale mlimani ama kwengineko duniani. Haya yote mliyopata kutoka ama kwa wafadhili mbalimbali waliokaribu na mgombea Fulani ama hata mgombea mwenyewe.&lt;br /&gt;Najua kuwa wengine tayari mmeshaahidiwa nafasi kubwa kubwa za uongozi katika nchi yetu ili mradi mhakikishe kura yako inaandikwa jina la mgombea Fulani.&lt;br /&gt;Najua wengine mna amini kabisa kuwa kutokana na ukweli kuwa wagombea wengine wote ni ‘wachafu’ na wengine sio watanzania basi huna la kufanya ispokuwa kumpigia kura mgombea ambaye mnadhani kuwa ni msafi na hana hata tone la uchafu isipokuwa harufu ya neema tu.&lt;br /&gt;Ndugu watanzania wenzangu naomba uchukue muda huu hata vidakika vichache kwanza kufikiria kama hayo unayoamini kuhusu mgombea huyo ni kweli na hakuna uwezekano kuwa kuna upande mwingine wa mgombea huyo ambaye wewe hujapata nafasi ya kuujua kwa sababu wenye majukumu ya kukujulisha wamelazimika kutokujulisha.&lt;br /&gt;Halafu ndugu mtanzania mwenzangu naomba ufikirie kama kweli vigezo unavyotumia kuamua mtu wa kumpigia kura yako tukufu ni vigezo tosha vya kumpa mtu jukumu zito la kuwa rais wako mwenye nguvu za juu za kimaamuzi katika kila kona ya maisha yako kwa mika mitano ama kumi ijayo?&lt;br /&gt;Hivi vigezo hivyo vimeweza kukusaidia kutambua mtu ambaye kweli na sio anayejidai, ambaye atahakikisha chama chako kinaendelea kuwa na umoja na nidhamu ya kweli iliyowezesha kushinda mitihani mbalimbali ambayo kimekumbana nayo kwa miaka yote hii tangu kianzishwe na wazee wetu waliotutangulia?&lt;br /&gt;Hivi vigezo hivyo vilijitosheleza kukuongoza wewee kufikia uamuzi wako kwa umakini wenye kuhitajika kuamua mtu bora wa kumkabidhi hazina yetu, utamaduni wetu, uvumilivu wetu, upendo wetu, unoja wetu na zaidi maisha yetu na wote tuwapendao na watupendao.&lt;br /&gt;Hivi uamuzi wako umetilia maanani kama huyo utakayemchagua atakuwa ndiye anayetakiwa kukuongoza wewe na familia yako katika mapambano dhidi ya gonjwa la ukimwi kwa yeye mwenyewe kuwa mfano bora wa kubadili tabia.&lt;br /&gt;Hivi huyo mgombea umpendaye au unayelazimika kumchagua ndio kweli yeye atayeweza kuiongoza Tanzania katika dunia hii ya mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi kwa umakini wa hali ya juu wenye kutambua nini haswa kinatakiwa kifanyike ili nchi yetu iheshimike duniani na hivyo kusikilizwa matakwa yake.&lt;br /&gt;Hivi huyo mgombea anaweza kumlinda mdogo wako, dada yako, kaka yako, mpendwa wako, mwanao au rafiki yako mpendwa na masahiba ya utandawazi yaliyojaa ulaghai na utapeli wa kila aina.&lt;br /&gt;Ndugu yangu umejaribu kufikiri ikiwa ni mgombea wako anayeweza kutuokoa katika janga la kuvunjika kwa amani ya nchi yetu kutokana na tamaa ya madaraka ya baadhi ya wagombea ambao wameamua kutumia mbinu za chuki na visasi ili kufanikisha matamanio yao ya kidunia.&lt;br /&gt;Hivi ni kweli mgombea unayetka kumpigia kura yako anaweza kusema hapana kwa wababe wa dunia pale wanapotka kufanya nchi yetu ni tambara lao bovu la kufutia vinyesi vyao vinavyopita vikidondoka kila kukicha.&lt;br /&gt;Hivi kweli ndugu yangu hudhani kuwa hata kama una deni la kulipa fadhila za mgombea uliyeambiwa umpigie kutokana na mamilioni uliyopewa, maslahi ya ndugu zako pale nyumbani na watanzania kwa ujumla yana umhimu zaidi kuliko ya hao.&lt;br /&gt;Hivi kweli ndugu yangu unadhani kuwa mgombea uliyeambiwa umpigie kura ulipokuwa unapewa msaada ule wa kifedha ndiye atakeyeweza kukupunguzia kero la rushwa linalowasibu kila siku wewe na familia yako.&lt;br /&gt;Hivi ni kweli kuwa mgombea huyo uliyevutiwa naye anaweza kujenga nyufa za nguzo za dola letu zinazobomolewa na wapambe wake kila kukicha ili nao wapate kuingia ikulu bila ya appointment kuanzia mwezi wa kumi na moja mwaka huu.&lt;br /&gt;Hivi umefikiria jinsi kura yako inavyoweza kuwaingiza ikulu mabaradhuli, wezi, wauza nchi, waruka kodi, mafuska na walaghai ambao wankuja kwako na sura ya ucheshi lakini ndani imejaa ushetani wa hali ya juu kabisa.&lt;br /&gt;Ndugu yangu kwa kweli sipendi kukuchosha maana najua hapo ulipo unamajukumu makubwa mbele yako, lakini naomba ufikirie kidogo kama kura yako haiendi kwa mtu ambaye ameonyesha dhahiri kuwa hakubaliani kabisa na nyendo na maadili ya utanzania ambayo mwalimu wetu baba wa Taifa alituwekea kama vipimo vya mapenzi yetu ya kweli kwa nchi yetu.&lt;br /&gt;Mwisho ndugu yangu mpendwa naomba ufikiri hivi ni kweli kura yako haiwezi ikatoa chaguo bora zaidi litakalotuwezesha kuokoa taifa letu kutoka katika janga la kuangamia, litakalotuwezesha watanzania kwa mara nyingine kutembea vichwa juu kwa kujiamini, litakalotuwezesha kutuepusha kuwa na baraza la mawaziri lilojaa matapeli na walaghai watakaokuwa wakitudanganya kila kukicha, chaguo litakalotuletea viongozi waadilifu kwa mungu na kwetu sisi bila ya kujali hali zetu za kimaisha, chaguo litakalolinda thamani ya kila mtanzania, chaguo litakalotusaidia kuinua hali ya elimu ya nchi yetu kwa kujua thamani yake na zaidi chaguo litakalo simama kidete kuchukua maamuzi kwa utulivu na umakini wa hali ya juu ilojawa na busara za kiuongozi bila ya kuhatarisha maish yetu na wala kurubuniwa na wapambe uchwara.&lt;br /&gt;Ndugu yangu mwana CCM, ni wewe ndiye utakeyeamua ni Tanzania ya aina gani tutakayokua nayo wiki mbili zijazo.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-5767072575557432320?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/5767072575557432320/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=5767072575557432320' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/5767072575557432320'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/5767072575557432320'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2007/08/barua-wazi-kwa-wapiga-kura-wa-ccm.html' title='BARUA WAZI KWA WAPIGA KURA WA CCM..'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-7262482750522400904</id><published>2007-08-02T10:33:00.000-07:00</published><updated>2007-08-02T10:35:21.185-07:00</updated><title type='text'>DHANA YA ARI MPYA NA SIASA ZA MATUMBO</title><content type='html'>@2005...kuelekea uchaguzi mkuu. Published by Mtanzania Jumapili..&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya mbio za ugombea nafasi ya Urais katika Chama Cha Mapinduzi kutulia na anayedhaniwa kuwa mkombozi kupatikana sasa mapambano yamehamia katika nafasi za ubunge na udiwani.&lt;br /&gt;Katika siku za hivi karibuni sura nyingi mpya zimeibuka zikijitangaza kuwa na nia ya kuomba ama kupigania uwakilishi wa watanzania katika nafasi mbalimbali za uwakilishi zilizobadilishwa jina na wajanjawajanja wa sasa na kuitwa nafasi za uongozi na uheshimiwa.&lt;br /&gt;Tofauti na miaka iliyopita ambapo tulizoe sura Fulani fulani tu, mwaka huu mambo ni nguvu mpya tu.&lt;br /&gt;Ni dhahiri kuwa hivi sasa zaidi ya wakati mwengine wowote vijana wanawake kwa waume wamekuwa tayari zaidi kuwania nafasi za uongozi (uwakilishi) katika jamii zao kitu ambacho kwa upande mmoja ni kizuri na muhimu kwa taifa letu kwa ujumla.&lt;br /&gt;Ni wazi kuwa ushindi wa mgombea wa CCM aliyetumia jukwaa la ujana katika kujihakikishia nafasi hiyo umekuwa na athari kubwa katika mfumo mzima wa siasa ndani na nje ya CCM.&lt;br /&gt;Kwa kiasi Fulani ushindi huo umekuwa ni chachu kwa wanasiasa wachanga ambao hapo awali kamwe hawakuthubutu kusimama na kuhoji uhalali wa wazee wao pekee kuendelea kushika nafasi za kiutawala milele amina.&lt;br /&gt;Ushindi huu dhidi ya wale walioitwa wazee umeweza kuwatia moyo vijana kwa malaki kuwa hata wao wanaweza kupata uheshimiwa kama wataamua kama alivyoamua “kijana” mwenzao.&lt;br /&gt;Ushindi huo umeweza kuwaamsha vijana wote kwa pamoja, makini na wajanjawajanja, ambao kwa miaka kadhaa walikuwa katika ndoto ya kuweza ama kuwa wawakilishi makini au kuukwa uheshimiwa kama walivyo wengine.&lt;br /&gt;Kwa ujumla vijana wa kitanzania wameonyesha nia ya dhati ya kuacha kutumiwa kama ngazi za madaraka na wale wanaowaita wazee waliochoka na sasa wameamua kuingia uwanjani wao wenyewe.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Leo ningependa kuchambua suala zima la ari mpya na nguvu mpya katika taswira inayojengeka ya maelfu ya vijana kuonyesha nia na kuanza kampeni kubwa ili kuaminiwa na kupewa nafasi ya uwakilishi katika utawala ujao.&lt;br /&gt;Kati ya vijana waliojitokeza wapo vijana wa makundi mawili ama matatu.&lt;br /&gt;Wapo vijana wazee ambao ni zaidi ya miaka 35-40. Hawa wanatumia dhana ujana kama propaganda ya kukubalika katika jamii iliyogubikwa na ndoto ya “ujana ukombozi”. Hawa wengi wao ni vijana wa zamani kiumri lakini wanaweza kuwa vijana wa sasa kimatendo. &lt;br /&gt;Wao wamekuwa wakitumia nafasi walizonazo kisiasa, kiserikali ama kibinafsi kujikusanyia nguvu za kifedha (kiuchumi) ili wakati ukifika waweze kujichomeka ndani ya mioyo ya watanzania na ili ama wawatumikie watanzania au waweze kujiongozea walichonacho.&lt;br /&gt;Wengi wao ni wanajiita wasomi kwa kuwa wana digrii kadhaa hata kama zengine ni za kudesa na hazina uhusiano wowote na uongozi, mimi siwezi kuwaita wasomi. &lt;br /&gt;Kwa mahesabu yao ni kuwa kijana mwenzao akishapewa madaraka basi ni wazi atataka kushirikiana nao kutekeleza kauli mbiu ya “ARI MPYA, NGUVU MPYA NA KIZAZI KIPYA”&lt;br /&gt;Hivyo basi wao wanadhani ama wanadai wanamtayarishia mazingira kijana mwenzao ili atakapokuwa anatengeneza jeshi lake la makomando wa kichina aweze kuwaona na kuwasimika utukufu.&lt;br /&gt;Kundi la pili ni lile la vijana wenzangu wenye miaka kati ya 25-40 ambao kwa kweli wengi wao ni vijana kweli kiumri, kifikira na kimatendo.&lt;br /&gt;Wengi wao hawana elimu ya kutosha ya kujiita wasomi lakini wapo walio na digrii moja nao lakini wana ujasiri wa kujitanabahisha na kina Prof Shivji, Baregu na wengineo.&lt;br /&gt;Katika kundi hili wapo wengi ambao hadi hivi karibuni uongozi kwao ulikuwa  ni kupoteza muda na kuhatarisha maslahi yao binafsi. Hii iwe maofisini wanapofanya kazi, mashuleni wanaposoma na vilevile katika biashara zao binafsi haramu na halali.&lt;br /&gt;Katika kundi hili ambalo ni kubwa si haba, kuna wengine ambao uwezo wao wa kifedha ambao hata kama umetokana na kuibia serikali, kulisha watanzania vyakula vyenye sumu, kuuza siri za nchi, kutetea majambazi na wezi wa mali za umma, kusainisha nchi mikataba ya kihuni na machafu mengineyo, umewapa jeuri kuwa hakuna cha kuwazuia na wao kuwa waheshimiwa.&lt;br /&gt;Kwao wao kujiingiza kwenye siasa ilikuwa ni mwiko eti watahatarisha maslahi yao. Wengi wa hawa katika siku za nyuma kamwe hawajawahi kujitokeza kipigania hai ya yeyote yule hata kama ni motto ananyanyaswa katika daladala. Kwao wao ilikuwa ni bora wao wamekaa kwenye viti ya wengine shauri yao. &lt;br /&gt;Wengi wa hawa siku hizi ndio wamekuwa wakombozi kila sehemu mradi kuna wapiga kura wanawaona.&lt;br /&gt;Kundi la tatu ambalo ni dogo mno lakini ndilo muhimu kwa taifa letu ni la wale vijana wa kati ya umri wa miaka 20-35 ambao katika maisha yao yote ya nyuma wamekuwa mstari wa mbele katika kupigania maisha mema kwa watanzania wote.&lt;br /&gt;Katika kundi hili wapo wenye elimu ya kutosha na elimu ndogo kama tukipima kwa vigezo vya madarasa. &lt;br /&gt;Lakini zaidi wana elimu ya matitizo ya kijamii na kisiasa yaliyomzunguka mtanzania na kwa miaka kadhaa sasa wamekuwa mstari wa mbele kuyaongelea kila pale inapowapasa kufaya hilo.&lt;br /&gt;Kwa vitendo wameweza kuonyesha umma jinsi gani walivyoweza kujitoa mhanga katika nyakati mbalimbali kwa ajili ya kutaka kuona watanzania wenzao wakiacha kuteseka na kuonewa kwa kunyimwa haki zao mbalimbali.&lt;br /&gt;Tatizo ni kuwa kundi hili halina fedha za kufanya kile tunachokiita kampeni hivyo kuna hatari kubwa ya kushindwa ama kununuliwa na wenye fedha hivyo kushindwa kutekeleza kile wanachofikiria kukifanikisha.&lt;br /&gt;Watashindwa kwa kuwa tayari na kuna wajanja wajanja ambao kwa ufanisi wa hali ya juu wameweza kubadilisha kabisa maana nzima ya uongozi na kiongazi. &lt;br /&gt;Hawa wamefanikiwa kutumia mwanya wa demokrasia kufanya mchakato mzima wa kuchagua wawakilishi wetu kutoka kuwa wa kutafuta yule mwenye sifa za kuongoza wenzie kwa umakini hadi kuwa kama vile kazi ya kuchagua bidhaa katika mfumo huu tunaouita wa soko huria. &lt;br /&gt;Mfumo ambao hivi sasa ndio unatopatia viongozi wa kila aina kwa kuwa unaruhusu yeyote yule kuweza kushinda kuwa kiongozi mradi ana uwezo wa kujiuza na kuulaghai umma kwa nguvu kuwa yeye ndio anameremeta hata kama kwa kutumia mkorogo tunaouita takrima.&lt;br /&gt;Bahati mbaya zaidi wapiga kura wa sasa tumeondokana na umakini wa kuhoji ubora wa bidhaa kama hizo na kukubali kuvutiwa na mwonekano wake tu eti kuwa Fulani anakubalika.&lt;br /&gt;Kwa kweli wanaotoka katika kundi hili ni wachache mno lakini wapo wakijaribu nafasi yao hata wakijua kuwa wanacheza katika uwanja huu wa kisiasa uliojaa visiki na mbigili. &lt;br /&gt;Wao ndio pekee wanaoweza kuwambia watanzania ni kipi wamekifanya kwa faida ya jamii wakati wakiwa bado wachanga kiumri na kisiasa hata kama hawakuwa na uwezo wa kutosha. Hawa ndio wanaweza kuwaambia wananchi ni maslahi mangapi binafsi wameyapoteza kwa kujaribu kusimamia ukweli pale inapobidi.&lt;br /&gt;Mfano wa hawa ni kijana mwenzangu mmoja mwenye umri wa miaka ushirini na nne ambaye siku alipojitokeza kutangaza kugombea ubunge jimbo fulani jijini Dar es Salaam, vyombo vya habari vilimkejeli kuwa ni motto na kumchora akiwa na nyonyo mdomoni akidai haki yake ya kupigiwa kura.&lt;br /&gt;Pamoja na umri wake mdogo kwa kipimo cha uwana siasa wa Tanzania, kijana huyu niliyotokea kumjuwa wakati bado akiwa mwanafunzi wa kidato cha tano lakini tayari mpambanaji shupavu wa haki za binadamu na vijana kwa ujumla ndio mfano wa wale haswa wanaoweza kutekeleza kwa dhati ari mpya hii tunayoahidiwa endapo ni ari ya kumkomboa mtanzania kama wengi tunavyodhania.&lt;br /&gt;Nasema hivyo kwa kuwa tofauti na hao wengine wanaotaka kutumia dhana ya Ujana ama ari mpya , nguvu mpya na kizazi kipya, kwa bahati mbaya au nzuri ndio waliojazana katika uwanja wa CCM, vijana wa namna hii ni nadra sana katika jamii yetu iliyogubikwa na siasa za ndio mzee kwa miaka mingi sasa.&lt;br /&gt;Ni nadra kuwaona kwa sababu nyingi tu lakini moja ya wazi ni ile hali ya kutopenda kuingia katika mpambano wa kisiasa kama unaoendelea hivi sasa kwa kuwa umejaa uchafu ambao wengi wao wasingependa kujitambulisha ama kujihusisha nao.&lt;br /&gt;Bahati mbaya ni kuwa kwa kufanya hivyo ndipo wanaacha mwanya kwa “vijana” wa aina ya kundi la kwanza na la pili ambao ni wachache mno ndio wenye uchungu wa kweli na taifa letu ukiachilia mbala na swala zima la sifa za kiuongozi waliaonazo, kuweza kutawala ulingo wa kisiasa nchini.&lt;br /&gt;Ingawa nakubali kuwa wapo wachache walio tofauti, wengi wa vijana wenzangu hawa wa kundi la kwanza na la pili kwa kweli ukiwauliza ni kwa nini wanataka kupewa nafasi kwa kweli hawana jipya zaidi ya yaleyale tuliyoyazoea na hadithi nyingine za kizazi kipya&lt;br /&gt;Kwa kweli hawana ajenda mpya kabisa zaidi ya kuukwaa uheshimiwa ili waweze kuyafanya kwa ufanisi zaidi yale mambo hovyo waliyokuwa wakiyafanya wakati huu wasipokuwa na nguvu za kisiasa.&lt;br /&gt;Kwao wao nguvu za kisiasa ni muhimu sasa ili kujihakikishia nafasi yao katika mfumo wa kinyanga’u uliojaa rushwa, ufuska, uonevu, ufujaji wa mali za umma na uozo wa kila aina tunaojitahidi kuusimika katika jamii yetu. &lt;br /&gt;Yupo msomi mmoja ambaye alikuwa akijaribu kuangalia aina ya siasa katika upande wetu huu wa dunia. Yeye aliita aina za siasa za dunia ya tatu kama nchi yetu ilivyo ni siasa za matumbo.&lt;br /&gt;Siasa ambazo kwanza zinajali matumbo ya wachache walio na nguvu na suala la kusaidia jamii linakuja pale tu kura zao zinapohitajika ili kuendeleza nafasi ya utawala kwa wale waliomo na kutoa mwanya ya kuingia kwa wale wajanjwajanja wengine waliochoka kula mabaki.&lt;br /&gt;Kwa kweli kwa kutumia dhana hii ndipo ikanijia washawasha ya kujaribu kufuatilia mchakamchaka huu wa vijana wenzangu katika kugombea nafasi za uwakilishi ambao wao kwao ni nafasi za uheshimiwa.&lt;br /&gt;Hapo ndipo nilipochukua juhudi zaidi za kujua nani na nani anayetaka uheshimiwa hapo mwezi Oktoba na kwa nini yeye na nini sifa zake.&lt;br /&gt;Kitu kimoja ambacho uchambuzi wangu unaniambia ni kuwa kuna hatari ya kuwa badala ya kutengeneza safu ya wachezaji wa kweli wenye kuweza kuweza kutimiza ndoto ya taifa jipya kama tunaloambiwa na kuishia kubadili sura za manyag’au tu.&lt;br /&gt;Na ubaya ni kuwa manyang’au wa damu mpya huwa daima wanakuwa hatari zaidi kwa jamii kutokana na ukweli kuwa wametumia muda wa mwingi kusoma siasa chafu ambazo daima ndizo watakazotumia kufanikisha malengo yao binafsi na kuwanyamazisha wale watakaukuwa na kuburi cha kuhoji machafu yao hapo mbeleni.&lt;br /&gt;Tofauti na tuliowazoea, hawa manyang’au watarajiwa ni wazi kima chao cha kuridhika ni kigumu kufikika na hivyo ari na nguvu watakazotumia kushibisha matumbo yao na ya wapambe wao zitakuwa ni za kutisha mno kuliko tunazoziona hivi sasa.&lt;br /&gt;Si ajabu kuona kuwa aina hii ya vijana kwa wingi wapo katika chama tawala. Jibu ni rahisi mno. &lt;br /&gt;Kwao wao kugombea kwa chama tawala kunawahakikishia usalama wao wa kutuanikwa machafu yao, kunawahakikishia ushindi kama wataweza kuteuliwa, kunawapa nafasi kubwa zaidi ya kukumbukwa na Rais ajaye ambaye kwa mahesabu yao ni lazima atoke huko na vilevile hata wakishindwa bado maslahi yao yatendelea kulindwa kwa kuwa wameonyesha kuwa wenzi wa watawala.&lt;br /&gt;Kwa kifupi hawana jeuri ya kujaribu kubadili mfumo kwani siku nyingi wameshakubali yaishe, dhana yao ni kuwa huu ni wakati wa kucheza na timu ya ushindi ili kufanikisha mambo.&lt;br /&gt;Kwa kweli ukiangalia mwenendo huu kwa ujumla ni wazi hatima ya Tanzania yetu ipo katika hatihati kwani kwa jinsi hali inavyokwenda ni dhahiri vijana wa kundi la kwanza na la pili ndio watakaoibuka washindi. &lt;br /&gt;Hii ni kwa kuwa wazee wetu walishabadili mfumo wa siasa ndani na nje ya chama cha mapinduzi kuweza kufanya iwe rahisi kwa aina hiyo ya wanasiasa kupenya katika nafasi za uongozi katika jamii yetu.&lt;br /&gt;Ni watanzania wenye ujasiri wa hali ya juu tu ndio wanaoweza kuwazuia hawa jamaa wanapita wakitufitinisha na kila aliye na umri mkubwa ili wao waoenekane ndio watakatifu.&lt;br /&gt;Kama vijana wachache wenye uchungu wa kweli na taifa lao wataamua kusimama kidete na kuwapinga hawa walaghai wanaotumia madhila yetu kwa faida ya matamanio yao binafsi ni wazi makali yake yanaweza kupunguzwa kabla hawajafika mbali.&lt;br /&gt;Ni wazi tukiamua hilo litafanikiwa kwani hawa tuko nao mitaani, viwanjani, mashuleni, majumbani na hata kwenye taasisi mbalimbali za umma na binafsi walipojaza historia ya machafu ya kila aina.&lt;br /&gt;Kusimama na kuwaelezea machafu yao kwa wapiga kura ni wajibu wetu sote kwani ushindi wao ni balaa kwetu na salama yetu inategemea ujasiri wetu.&lt;br /&gt;Tukiwaacha hawa malaghai wa kizazi chetu ni wazi tutakuwa tunajipotezea nafasi hii tuliyoipata baada ya muda mrefu wa kulalama kuwa vijana tunanyiomwa haki yetu ya kujiongoza na kuongoza taifa letu.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-7262482750522400904?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/7262482750522400904/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=7262482750522400904' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/7262482750522400904'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/7262482750522400904'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2007/08/dhana-ya-ari-mpya-na-siasa-za-matumbo.html' title='DHANA YA ARI MPYA NA SIASA ZA MATUMBO'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-2227781187931798673</id><published>2007-08-02T10:21:00.000-07:00</published><updated>2007-08-02T10:28:14.489-07:00</updated><title type='text'>KIKWETE CHAGUA MAARUFU, SALIM CHAGUO MAKINI. (Sehemu ya pili)</title><content type='html'>CCM inavuna ilichopanda..........&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wiki iliyopita nilijaribu kuwaelezea wagombea wawili na kwa nini wameweza kuonekna kwa upeo wa wengi kuwazidi wenzao wengine katika nafasi ya umaarufu sio tu ndani ya CCM bali kwa watanzania kwa ujumla. Leo napenda kuendelea uchambuzi wangu kwa kuongelea siasa za uchaguzi kwa ujumla kama zinavyoendelea.&lt;br /&gt;Tofauti na wenzetu katika demokrasia zilizoendelea kule ughaibuni yaani sehemu kubwa ya Ulaya na Amerika kaskazini, Watanzania na Tanzania kama nchi na dola lake wana vigezo tofauti kidogo katika kumchagua kiongozi wa aina yoyote ile katika medani ya kisiasa. Kama ingekuwa ni suala la uzoefu na mvuto tu ndio turufu pekee basi kama nilivyosema wakati ule, mbio za uchaguzi zingekuwa zimekwisha. Lakini kwa jinsi ninayoona mimi, siasa za uchaguzi za CCM na Tanzania kwa ujumla kwa wakati huu zimejitwika katika maeneo kadhaa yafuatayo.&lt;br /&gt;Moja kubwa ni nafasi ya matakwa binafsi ya mtanzania mmoja mmoja bila ya kujali maslahi ya taifa kwa ujumla, ukiachilia bara la afrika na dunia yetu. Hili limejitokeza sana katika mijadala mbalimbali inayoendelea katika kila pande ya nchi yetu. Suala la mimi nitafaidka na nini kutoka kwa nani ndilo haswa limejikita kati ya wapiga kura wa CCM katika vikao vikuu vya chama ambavyo ndivyo vitateua mwakilishi wao katika kugombea nafasi ya Urais hapo Oktoba. &lt;br /&gt;Suala hili ambalo kwa kiasi kikubwa limechangia kuweko kwa uchambuzi unaolenga zaidi majina ya wagombea na sio vigezo vya wagombea bora ndilo pia limekuwa dira ya uchaguzi miongoni mwa watanzania wa ngazi na kada zote nchini, kuanzia wafanyabiashara wa aina zote, kubwa na ndogo, halali na haramu, wasomi, wafanyakazi na wasio na kazi, wakulima na wafugaji, na zaidi waandishi wa habari wetu. &lt;br /&gt;Wengi wetu tumegubikwa na kuangalia upatikanaji wa kirahisi wa mahitaji yetu binafsi ya muda mchache na kusahau au kutotilia umuhimu mahitaji ya muda mrefu ya taifa letu tukufu. Hili limetufanya tuongelee siasa kwa msingi wa majina zaidi ya uwezo na vipaji vya wenye majina hayo kwani kwetu bora ni yule tunayemuona tunashabihiana naye kama  ni kidini, kikabila, kirika, kifikira, kijamii, kiuchumi na hata kirangi!!!.&lt;br /&gt;Hata hivyo itakuwa ni dhambi kubwa kwa kuwalaumu watanzania kwa kosa hili, yaani kutumia maslahi binafsi kama ndio dira pekee ambayo watanzania tulio wengi tunaitumia kuamua nani anafaa na nani hafai. Dira hii potofu ya uchaguzi iliyotanda katika fikra za watanzania walio wengi, sio tu inatawala katika suala zima la kuchagua rais kwa sasa lakini pia hata katika masuala mengine yoyote ya kimaisha iwe rafiki, thamani za nyumba, kazi, aina ya elimu, na memnngineyo mengi kma sio yote.&lt;br /&gt;Dira hii ambayo imepandwa na kupaliliwa na dhana ya kihafidhina inayoendeshwa na falsafa ya unyang’au yenye kupitia njia ya BORA ELIMU, ambayo ndiyo iliyozaa taifa lenye upungufu wa umakini, tupende tusipende ina nafasi kubwa ya kuiamulia CCM nani anakuwa mgombea wao na si nani mgombea bora kutoka kwao.&lt;br /&gt;Tafiti mbali mbali zimefanywa na wasomi wetu na zimeonyesha wazi kuwa watanzania kwa kiasi kikubwa wamepunguza umakini wao katika kuchagua kinachowafaa na hivyo kujiweka VULNERABLE na siasa za kiujanja ujanja ambazo zina mvuto wa faida au mapato  ya kirahisi rahisi na sio yenye umakini wa kutufaidisha kwa muda mrefu. &lt;br /&gt;Hili linatokana na sera ya BORA ELIMU inayoendeshwa na wakubwa hawa kwa muda mrefu sasa ambayo inalenga kupata watanzania wa aina ya ndiyo mzee na sio wakorofi wenye chachu ya kuhoji. Sera ambayo umuhimu wake mkubwa umetokana na kuporomoka kwa uwezo wa kiutawala wenye kuamini maadili ya uongozi na umakini wa kiuongozi kitu ambacho kimefuatana kwa pamoja na mfumuko wa madhila ya kimaisha ambao umepelekea kumomonyoka kwa uhalali wa kisiasa wa tabaka tawala la nchi yetu.&lt;br /&gt;Ninasema kuwa CCM inavuna ilichopanda kutokana na hali inayojionyesha hivi sasa ya kuwa njia panda iliyojikuta imewekwa na kampeni za baadhi ya wagombea wake. Hali ambayo imewaweka katika hatari ya kupata bora mgombea atakeyewahakikishia ushindi wa kishindo na sio mgombea bora ambaye sio tu atahakikisha kujenga nyufa zinazojitokeza ndani ya muhimili ya chama na dola bali pia atarudisha sifa ya chama hiki kinachoelekea kaburini kwa mwendo wa mwanga wa taa. Mtu ambaye kutokna na haiba, upeo na mtazao wa kimaadili atweza kukirudishia chama hiki sifa iliyopotea ya kuwa ni chama imara, chenye nidhamu na kinachiaminika kama kimbilio la wengi na wananchi.&lt;br /&gt;Ukifuatilia kwa ndani sana mwenendo wa siasa ndani ya chama hicho hasa matamshi ya viongozi wa juu wa chama hicho, ni dhahiri kuwa kama jadi yake tangia enzi za Baba wa Taifa, hayati mwalimu Nyerere, tayari watukufu wachache wamekwishaamua nani anakuwa mrithi wa rais Benjamin Mkapa. &lt;br /&gt;Hata kama manung’uniko ni mengi miongoni mwao lakini ni wazi hali ya kampeni zinazoendelea zimewapelekea kuamua kuchukua uamuzi mzito mno miongoni mwao wa kuhakikisha chama kinatoa mgombea makini ambaye sio tu kwa uzoefu wake na haiba ya yake ya umakini ataweza kupambana na uasi wa watanzania kama watakosea kuchagua, lakini pia uasi ndani ya chama ambao ndio tishio kubwa zaidi kuliko mengine.&lt;br /&gt;Lakini kwa jinsi hali ilivyo, ingawa kuna mabadiliko ya upepo wa kisiasa unaotokea kwa kasi kubwa ambayo haikutegemewa na walio wengi, kazi ya kuwabadilisha mawazo watanzania walio wengi na hasa wapiga kura wa CCM inakua ngumu mno kama si ya hatari sana. Ni wazi wengi wao wameshaweka msimamo wao, na utmaduni wa mtanzania kwa kweli ni wa kutokuwa tayari kufanya mabadiliko makubwa ya kimaamuzi kwa urahisi(conservatism) hivyo majaribio haya ambayo ukiyatazama kwa undani ni yenye nia njema kabisa ya kuwahakikishia wana CCM na na hasa watanzania kwa ujumla,  kuwa chaguo litakaloletwa na CCM ambao wao (watukufu wachache) tayari wamelikubali ndilo bora zaidi na makini kwa CCM na watanzania kwa ujumla, limekumbwa na ugumu wa kipekee kabisa.&lt;br /&gt;Ugumu huu unatokana na kuwa chaguo hilo sio lile ambalo wengi wamekwisha amua kuwa ndio la manufaa yao na hivyo kudhani kuwa ndio la manufaa ya taifa. Vilevile dhana ya uwezekano wa uasi wa kiasiasa wa wananchi na wana CCM walio wengi kwa ujumla wakiwemo nuru ya tamaa ya mabadiliko kwa walio wengi, yaani baadhi ya wagombea vigogo, inawafanya watukufu hawa ndani ya medani za juu za CCM kuwa na mtihani mzito mno.&lt;br /&gt;Kwa ujumla ugumu huu chanzo chake kikuu kinatokea katika aina ya usomi wa watanzania walio wengi ambao umewapelekea kuamini mengi bila ya uchambuzi wa kina na wa makini hivyo kiurahisi kabisa kuamua nani atakayewatatulia madhila yao kwa wale waliogubikwa nayo na kuwaongezea zaidi wale walifaonikiwa kwa kiasi, ambao wangependa kufika juu zaidi na kuwapiku wale waliojisimika huko kwa muda mrefu mno. &lt;br /&gt;Kama watukufu hawa wangeona kuna umuhimu wa kuendeleza ELIMU BORA yenye kugubikwa na dhana na fikira za uzalendo wa kweli wenye kuneemeshwa na chachu ya kuhoji, basi kazi ya kuwashawishi wana CCM na watanzania walio wengi kuwa chagua wanalowapa ndilo bora zaidi kwao na kwa Tanzania kwa ujumla sio tu kwa wakati huu bali hata kwa wakati ujao, isingekuwa ngumu na ya hatari kama inavyonekana hivi sasa.&lt;br /&gt;Kazi nyengine ambayo ndiyo kubwa zaidi inayowagubika wakuu hawa wa CCM ni kupambana na upinzani mkali utakaotoka kwa wapambe wa mgombea maarufu ambaye inaonyesha tayari wameshamuona kuwa ni hatari kwa maslahi ya nchi kama waonavyo wao ingawa wanakubali kuwa ndio mgombea maarufu kuliko wote. &lt;br /&gt;Wapambe hawa ambao wengi wana upeo wa hali ya juu wa propaganda za kisiasa wakisaidiwa na nafasi ya kukubalika kwao ingawa sio wote katika jukwaa la vijana walio wengi ambao ndio nguzo ya umaarufu wa CCM, ni dhahiri hawatakuwa tayari kuona kuwa wanapokonywa nafasi ya wao pia kupenya na kuchukua nafasi za juu kisiasa nchini kutoka kwa wanasiasa wakongwe au wazee kwa lugha maarufu hivi sasa. &lt;br /&gt;Hata kama mgombea wao waliyeweza kumhakikishia umaarufu wake kwa wananchi walio wengi mno kwa utaalamu wa hali ya juu wa kipropaganda halali na haramu, atakubali yaishe ile naye ajihakikishie kuendelea kwa nafasi na umuhimu wake kisiasa kwa gharama nafuu, ni wazi wapambe hawa wanajua wazi kuwa ndoto zao nyingi hazitafanikiwa na pengine hata wakapoteza umuhimu wa kisiasa na kijamii wanaotmba nao hivi sasa. &lt;br /&gt;Hofu hii inaonekana wazi hivi sasa kiasi ya kuwa wale wachache ambao wanasukumwa na uzalendo wao kwa nchi zaidi ya mafanikio yao binafsi wameshaanza kuona umuhimu wa kujenga daraja kati yao na mgombea makini ambaye kwa njia moja au nyingine ndiye kimbilio lao.&lt;br /&gt;Lakini hili nalo linaweza kuwa tatizo kwa watukufu wa CCM wanaojaribu kuhalalisha uamuzi wao wa kumrithisha mgombea wanayemuona ni makini na bora zaidi kwa chamaa kwanza na jamii kwa ujumla. Ni tatizo kutokana na kuwa endapo daraja hili litajengeka vema na mgombea maarufu ambaye hadi sasa ana uhakika mkubwa wa kushinda kinyang’anyiro hicho endapo hakutakuwa na kile wengi wanakiita mizengwe na wasomi wanaita ukweli wa kisiasa, na akakubali yaishe mapema. Ni wazi kuwa kundi lengine la wagombea ndani ya CCM halitakubali kushindwa kirahisi. Kundi hilo linawahusisha wagombea wengine wawili au watatu ambao kwa hali ilivyo linaweza kuondoa uwezekano wa kumaliza uchaguzi mwezi Mei na kufanya uendelee hadi Oktoba na pengine zaidi ya hapo kutokana na uwezekano mkubwa wa kuamsha upinzani wa hali ya juu kutoka kwa watanzania walio wengi ambao wamejengewa dhana ya kuwa hao ni maadui wa amani na maendeleo yao.&lt;br /&gt;Kundi hili linaweza kuleta madhara makubwa kwa CCM na watanzania wote kwa ujumla, kutokana na ukweli ulio wazi kuwa muungano au makubaliano yoyote kati ya MGOMBEA MAARUFU na MGOMBEA MAKINI unaweza au yanaweza kuwahakikishia wengi wao mwisho wao kisiasa, kitu ambacho kwa siasa za dunia yetu ya tatu kama ilnavyojionyesha kwa majirani zetu, maana yake inaweza hata ikawa mwiso wao kimaisha. &lt;br /&gt;Kundi hili litajaribu kutumia kila aina ya mbinu, halali na haramu kujaribu kuzuia hali hiyo, kitu ambacho kitaendeleza mpasuko ndani ya CCM na mbaya zaidi kwenye vyombo muhimu na nyeti vya dola ambavyo ndivyo kwa miaka mingi sasa vimekuwa mihimili muhimu kwa tabaka tawala na taifa kwa ujumla.&lt;br /&gt;Wapo wanaofikiri kuwa mpasuko ndani ya CCM utakuwa neema kwa watanzania kwani utawezesha wananchi walio wengi ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakitafuta chama mbadala na kushindwa kukiona nje CCM, kuamini kuwa upinzania unaweza kuwa nusura yao.&lt;br /&gt;Dhana hii ina ukweli wake lakini kwa bahati mbaya kwa jinsi mambo yanavyokwenda, kuvunjika kwa CCM kwa staili inayojionyesha ni wazi kutafuatana na kuvunjika kwa dola hivyo kusababisha hasara kubwa kwa Taifa kwa ujumla. &lt;br /&gt;Hii inatoka ukweli kuwa tofauti na katika nchi za wenzetu kama Kenya na kwengineko, hapa kwetu CCM si chama tawala tu bali ni chama dola. Pale inapotokea kinavunjika kwa siasa za chuki na visasi kama tunazoziona sasa ni dhahiri viongozi wa juu wa CCM hawataweza kuhakikisha usalama wa dola ambalo kwa bahati mbaya limeachana na wajibu wake wa kuwa msimamizi wa siasa ndani ya chama tawala na kuwa sehemu ya ushindani wa kisiasa ndani ya mpambano huu. &lt;br /&gt;Suala hili la hatari ya kuvunjika kwa dola ndilo haswa limepelekea sio tuu viongozi wa kisiasa makini wa nchi yetu pamoja na viongozi wa kidini na kielimu kujawa na woga wa hali juu na kujikukuta wako njia panda katika kutimiza wajibu wao wa kulinda tabaka tawala na hivyo jamii kwa ujumla. &lt;br /&gt;Hii inatokana na ukweli kuwa ni wazi hata kama mambo yakawa shwari hata baada ya CCM kuchagua yeyote yule wanayempenda na wanaona anawafaa, kuna hatari kubwa kuwa mara baada ya mmoja wa hawa wanaochuana kwa nguvu zote atakapokabidhiwa dhamana ya ulinzi na usalama wa taifa wa nchi yetu, itambidi kuchukua hatua za kusafisha chama na dola na kuondokana na vile vinasaba vilivyokuwa vikimpinga waziwazi alipokuwa anawania kuteuliwa na chama au hata wakati wa kuelekea uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba. &lt;br /&gt;Hilo halitakuja tu kwa ajili ya chaguo maarufu kujihakikishia usalama wake bali pia litambidi kufanya hivyo kwa ajili kujaribu kukidhi hamu kubwa ya wafuasi wake waliompigia debe na kumshindisha kwa kishindo. Hamu ambayo imejengwa katika dhana ya usafi wa kisiasa na uthabiti wa ki hulka ambao wengi weu tunadhani ni silaha muhimu katika kuondoa unyang’au huu unaotukumba hat kama kuna hatari gani itayoukumba hapo mbeleni. Wanasayansi wa kisiasa kuchambua dhana hii kama mwisho unahalalalisha njia (ends justifies the means). &lt;br /&gt;Na endapo atapita mtu anayetoka kwenye upande ule mwingine, yaani wale ambao CCM inaona watakuwa mzigo mzito ku-ubeba lakini kutokana na nguvu mbalimbali zikiwemo za dola na udhaifu wa baadhi ya viongozi wa vyama kadhaa pinzani wa CCM, wanaweza kushinda mwezi Oktoba, ni wazi itabidi wajikoshe kwa watanzania ili kujihalalishia nafasi zao. Hapa pia kuna hatari ya kuwaona kina Mutharika wengine ambao ingawa wao wenyewe ni wachafu wa kutupwa lakini wangependa kuwabebesha wengine lawama ili wao waonekane ni malaika. Hili lazima litaleta vurugu zaidi miongoni mwa tabaka tawala na kuathiri uthabiti wa mhimili wa amani yetu yaani dola.&lt;br /&gt;Kwa hali hiyo hapo juu na sababu nyingine kadhaa wa kadhaa, ni wazi CCM kwa sasa inavuna ilichopanda kwa kujikuta njia panda baada ya kushindwa kwa viongozi wa juu ambao daima ndio wamekuwa watoa uamuzi wa kweli wa nani anamrithi nani, kusimama wazi na kuwaonyesha wana CCM na watanzania kwa ujumla chaguo wanaloliona wao kuwa makini na bora zaidi dhidi ya chaguo maarufu zaidi, na wangependa wananchi kupitia watukufu wachache kule DODOMA kuridhia chagua hilo kwa kile waonavyo wao nap engine kuna ukweli, ni kwa manufaa ya taifa. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ilikuwa ni makala maalumu wakati tunaelekea kule Chimwaga mwaka 2005..&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-2227781187931798673?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/2227781187931798673/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=2227781187931798673' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/2227781187931798673'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/2227781187931798673'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2007/08/kikwete-chagua-maarufu-salim-chaguo_02.html' title='KIKWETE CHAGUA MAARUFU, SALIM CHAGUO MAKINI. (Sehemu ya pili)'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-7977049251606748633</id><published>2007-08-02T10:19:00.000-07:00</published><updated>2007-08-05T09:14:42.151-07:00</updated><title type='text'>KIKWETE CHAGUA MAARUFU, SALIM CHAGUO MAKINI. (Sehemu ya kwanza)</title><content type='html'>Published by Mtanzania Jumapili@ 2005&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hata kama kuna wengi watakaokasirika, ni ukweli ulio wazi kuwa uteuzi wa mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia chama cha CCM utakaofanyika tarahe Mosi mwezi Mei 2005 kule DODOMA, ndio utakao amua kuwa harakati za kumtafuta rais wa Tanzania kwa miaka mitano au kumi ijayo zimekwisha au ndio kwanza zinaanza. &lt;br /&gt;Nasema hivi kwa kuwa ni wazi kati ya wagombea wote waliojitokeza kuna wagombea wawili au watatu ambao wakipitishwa, sio tu watatoa nafasi kwa vyama mbalimbali vya upinzani ambavyo bado havijaweza kujiuza vyema kwa watanzania kujitutumua kisiasa na kutoa upinzani mkali kwa baba wa dola, yaani CCM.&lt;br /&gt;Lakini vilevile kuna wagombea wengine wawili ambao kwa kweli CCM ikimpitisha mmoja wapo na mwingine kutopiga kelele za mizengwe, basi ushindi wa kishindo unakuwa tayari umeshajikita kwa ndugu zetu wa hawa, yaani CCM.&lt;br /&gt;Wawili hao si wengine bali ni Mtanzania mmoja maarufu hapa nchini na pande zote za dunia, Dr Salim Ahmed Salim na mwengine maarufu sana hapa nchini na maeneo mbalimbali katika maziwa makuu ya afrika, Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete.&lt;br /&gt;Ni ukweli usio fichika kuwa Ndugu Kikwete ni chaguo maarufu kabisa kupita wote waliojitokeza kuwania nafasi hii kupitia CCM, akifuatiwa kwa mbali ingawa hali inaonekana kubadilika kwa kasi mno, na Dr Salim Ahmed Salim. &lt;br /&gt;Sababu za umaarufu huu ambao kwa kweli ni muhimu kwa taifa linalozidi kupoteza mwelekeo kila kukicha, ni nyingi na mimi nitajitahidi kuzitoa kwa kadri ya niwezavyo bila ya unafiki.&lt;br /&gt;Ndugu Kikwete ambaye ni mwanasisa mkongwe ndani ya CCM tangia ujana wake, chini ya usimamizi wa Mwalimu Nyerere ambaye yeye anasahibiana naye kwa undugu wa kiapo, kwa wanaokumbuka mchango wa Sheikh Bharamiya wa kule Bagamoyo ambaye anasahibiana naye, kikwete ameweza kujitokeza kama mwnasiasa kijana tangia pale alipogombea na kushindwa nafasi hiyo mwaka 1995 akiwa na umri wa miaka 45. &lt;br /&gt;Hivi sasa ndugu huyu anakaribia miaka 55, lakini kutokana na kujitambulisha zaidi na vijana ambao ndio wengi wanaonekana kumzunguka, na hulka yake ya uhalisia “simplicity”, ndugu huyu ameweza kujitengenezea mhimili wa kisiasa katika jukwaa la vijana ambao ama kwa bahati au kwa makusudi wameweza kupenyeza ngome za CCM kwa wingi kuanzia mwaka 1998 na kuendelea. &lt;br /&gt;Wako wanaohoji kuwa yeye si kijana lakini ningependa kuwakumbusha kuwa ujana unaozungumziwa hapa si umri bali ni fikra, ambazo vijana walio wengi ambao ndio wamiliki halali wa taifa hili wanaamini kuwa Ndugu Kikwete pekee ndiye anayewakilisha ndoto zao za kuondokana na ufedhuli wa kimaisha unaotugubika.&lt;br /&gt;Kingine ambacho Ndugu Kikwete ameweza kukiwakilisha kwa jamii, ni dhana ya uasi wa ndani UASI WA NDANI ya mfumo wa kuhafidhina wenye kuendeshwa na falsafa ya rushwa iliyokithiri ndani ya Chama kinachojiita cha Mapinduzi. &lt;br /&gt;Ukiondoa karibia wote wanagombea nafasi hiyo ndani ya CCM, Ndugu Kikwete ndiye pekee mwenye kuonyesha kuwa ni kweli mwakilishi wa wakulima na wafanyakazi wa tabaka la kati na la chini kutokana na haiba yake ya uhalisia. Ndugu huyu ambaye ama kwa uthabiti wa kimaadili au mahesabu ya kisiasa, pamoja na mambo mengine ameweza kukataa “kuzawadiwa” nyumba zilizojengwa kwa jasho na damu za watanzania, kitu ambacho kinawapa matumaini vijana na wazee wengi kuwa ataweza kupambana na rushwa na hata kusafisha uozo huo ndani ya CCM na tabaka tawala kwa ujumla. &lt;br /&gt;Sifa nyingine aliyonayo Ndugu Kikwete ni suala la mvuto. Hili kwa kweli ni silaha kubwa ambayo hata wenzanke wakimdhihaki vipi, kamwe hawataweza kumuangusha. Suala la sura ya mvuto ni muhimu sana kwa jamii iliyokata tama kama Tanzania. &lt;br /&gt;Sio kwamba inampaa wapenzi wengi kisiasa hasa wale wa jinsia tofauti naye ambao ndio wenye kura nyingi zisizotetereka kirahisi ndani na nje ya CCM, sura na haiba ya mvuto ni silaha muhimu kwa kuongoza katika mwenendo wa siasa za kimaarufu “popular politics” ambazo wengi tunadhani zinahitajika ili kusafisha uozo wa kisiasa tulionao. Uozo ambao umejengwa na kulindwa na baadhi ya wagombea pinzani wa ndugu huyu ambao watanzania wengi hasa vijana wangependa kuona wanatoka katika medani za kisiasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sifa za Dr Salim duniani nadhani wote twazijua, sio tu kutokana na majukumu mbalimbali ya kitaifa na kimataifa ambayo aliwahi na bado amekabidhiwa na wanadunia, lakini pia haiba yake ya unadhifu wa kisiasa ya mfano wa Mwalimu wake kipenzi , hayati Mwalimu Nyerere ambayo kwa sasa imekuwa ni fimbo muhimu katika jaribio lake la kuomba dhamana ya kuwaongoza watanzania moja kwa moja kama Rais wa nchi yetu. Mengi yamesemwa kuhusu Dr Salim lakini mimi ningependa kwa kutumia kautaalamu kangu kadogo cha uchambuzi wa siasa wanachonipatia wasomi wetu pale mlimani kwa miaka kadhaa hivi sasa, kuongezea yale machache ambayo nadhani hayasemwi au hayajasemwa bado na vyopmbo vyetu vya habari.&lt;br /&gt;Kutokana na upeo wa juu alionao ndugu huyu kuhusiana na mambo ya siasa za kidunia, Wengi na hata kutoka vyama pinzani na CCM wanaona Dr Salim anaweza kuwa ndio tunu ya nchi yetu kutupeleka kwenye Demokrasia ya kweli na si kwa maneno tu bali kwa vitendo. &lt;br /&gt;Kwa wengi wanovutiwa naye, hilo kwake hakuna mjadala kwani ingawa wengi hubadilika na nguvu za madaraka, kwake yeye kama aliyewahi kuwa kiongozi wa mapambano dhidi ya unyonge, ukoloni na ubaguzi wa aina yeyote popote pale duniani pamoja na kuwa mpiga mbiu mkuu wa utawala wa demokrasia ya kweli barani Afrika, kufanya tofauti utakuwa ni unafiki ambao hata mtu asiye na aiba ya aibu hataweza kufanya hilo.&lt;br /&gt;Lengine ni kuwa uhusiano wake wa karibu na Baba wa Taifa letu, Hayati Mwalimu Nyerere ambye ndiye amekuwa dira yake kisisasa. Uhusiano huo na mwalimu pamoja na wale watukufu wengine wa zamani ( Disgruntled old guards) ambao walilitumikia taifa kwa adabu na heshima ya juu kwa wananchi. Hawa ni kama wazee wetu akina Judge Warioba, Mzee Ibrahim Kaduma na wengineo wachache lakini washupavu ambao hadi sasa wanajaribu kuwa nguzo na dira ya dhana ya utawala wa kamaadili ambao kwa kweli umemong’onyoka mno kama sio kuisha kabisa. Hawa wameweza kumpa Dr Salim imani ya kuwa ataweza kurudisha utawala wa nidhamu ya kimaadili nchini. &lt;br /&gt;Katika safari yake kuelekea uchaguzi, Dr Salim ameweza kuonyesha kuwa mbali na kusimamia ujenzi wa uchumi imara lakini anaweza kurudisha dhana ya maadili ambayo si tu tunaihitaji kwa kulinda haka kaamani ketu kwa kulinda utu wa kila mtanzania bila ya kujali nafasi yake kiuchumi, bali pia kutupunguzi janga la ukimwi ambalo kwetu sisi ni adui kama ilivyo ugaidi wa kidini kwa Taifa la Marekani hivi sasa.&lt;br /&gt;Kingine ambacho haka kaupeo kangu ka kuchambua masuala ya siasa kameweza kunionyesha ni kwa msomi kama Dr Salim ambaye sio tu wa darasani bali hata katika kufikia maamuzi yake, ni dhahiri atweza kusimamia kuona kuwa thamani ya usomi makini na wasomi wetu itarudishwa. Katika duru ya wasomi, ingawa si wote, wengi hata wale wanaompinga kwa sababu zingine wanaamini kuwa Dr Salim ataweza kutumia vyema nafasi ya kutuongoza kunusuru hali ya mbambo katika madhabahu zetu za kisomi na elimu, ambazo sio tu hali inatisha bali pia ni hatari kubwa kwa taifa letu hasa katika dunia hii ya ushindani usiokuwa na huruma wala haiba. &lt;br /&gt;Bila ya kuwa ni kiongozi anayethamini hali na mawazo wa wasomi, kutambua umuhimu wa ELIMU BORA na sio BORA  ELIMU, anayejiongoza kisiasa na kuwaongoza wananchi wake kwa lugha na mtindo wa kisomi, ni wazi hata tukiletewa malaika, safari ya tunapoelekea kusikojulikana itakuwa ya mwendo kasi na wa hatari mno.&lt;br /&gt;Lingine ambalo kwa kweli si ajabu kuona watanzania wengi wa kizazi chetu hawakioni ni kuwa watanzania kama washika dau wakuu wa dunia ya tatu, au kwa kifupi masikini wa dunia, hivi sasa tunakabiliwa na zoezi kubwa la kupambana kuweza kupata mfumo wa siasa za kimataifa ambo utatambua na kutetea zaidi maisha yetu kiuchumi na kijamii kwa miaka mingi ijayo. &lt;br /&gt;Hili ni suala la marekebisho mbalimbali katika mfumo wa umoja wa mataifa (UN) ambao kutokana na mchango wa Dr Salim na viongozi wenzake wengi wapatao kumi na tano pamoja na wasomi wetu kama Prof Mwesiga Baregu na Prof Haroub Othman , kuanzia mwezi September 2005 kule New York, Marekani na kwengine pote duniani., majadiliano makali yataendelea kujaribu kubadili mfumo wa kimataifa. &lt;br /&gt;Mfumo ambao kwa miaka mingi umekuwa ukiwapendelea mno mataifa makubwa na tajiri dunia na kukandamiza ndoto zetu za kupata ahuani ya kweli ya kimaisha. Kwa kweli kama hatutakuwa na kiongozi shupavu, makini, msomi, mwenye kuheshimika katika medani za kimataifa na mjuzi wa hali ya juu wa masuala haya, Tanzania ambayo ina jukumu la kuongoza sauti ya wanyonge kupitia nafasi yetu katika baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kama mwanachama wa muda kwa nika miwili kuanzia mwezi January mwaka huu, ni dhahiri mpambano huu tunaweza tukaupoteza hivyo tukawa tumejisaliti na kuwasaliti mabilioni ya wanadunia masikini na wanyonge wanaotegemea sauti yetu huko. &lt;br /&gt;Nasisitiza hili kwa sababu najua wazi kuwa bila ya kubadili mfumo wa siasa wa kimataifa, hata kama utaletewa malaika wa juu kabisa, kamwe mbio zetu zitaishia ukingoni na kuendelea na siasa za longolongo, kama wanavyosema vijana wa mjini.&lt;br /&gt;Ukiangalia hizo baadhi ya sifa za wagombea hawa wawili wa CCM hapo juu na nyingine nyingi zilisosemwa na zinazosemwa na watanzania mbalimbali, kama za kweli au za uongo, ni wazi kuwa mmoja kati yao ndiye turufu ya ushindi wa kirahisi kwa CCM.&lt;br /&gt;Kama siasa zingekuwa ni kufuata kigezo cha umaarufu tu na sio vinginevyo basi ni wazi kuwa wagombea wengine wangeshajitoa muda mrefu na kuupunguzi umma wa watanzania adha ya kufukiri sana kuhusu hatma ya maisha yao na nchi yao kwa ujumla. Lakini ukweli sio hivyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na: Omar S Ilyas&lt;br /&gt;University of Dar Es Salaam.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-7977049251606748633?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/7977049251606748633/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=7977049251606748633' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/7977049251606748633'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/7977049251606748633'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2007/08/kikwete-chagua-maarufu-salim-chaguo.html' title='KIKWETE CHAGUA MAARUFU, SALIM CHAGUO MAKINI. (Sehemu ya kwanza)'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-892575776834868185</id><published>2007-08-02T10:09:00.001-07:00</published><updated>2007-08-02T10:09:37.983-07:00</updated><title type='text'>Masikini Sumaye!</title><content type='html'>MASIKINI SUMAYE!!!!!&lt;br /&gt;@Mtanzania Jumapili Newspaper. 2005.&lt;br /&gt;Wakati kumebakia takribani wiki saba na siku chache kwa chama tawala cha CCM kuchagua mgombea wake wa kiti cha urais katika uchaguzi mkuu ujao hapa nchini, vimbwanga vya kisiasa vinazidi kushamiri. Kwa sisi wachambuzi wa masuala ya kisiasa kazi inazidi kuwa kama kiswahili cha mtaani kinavyosema “kuchanganyia”.&lt;br /&gt;Hivi karibuni baaada ya maneno mengi ya pembeni, mmoja wa wachangamkiaji wa nafasi hiyo ameamua kukata ngebe za wale aliowaita wapinzani wake “kisiasa” kwa kuudhihirishia umma kuwa baadhi ya mambo yanayosemwa kuhusu yeye ni kweli na wala sio umbea wa wadaku.&lt;br /&gt;Hapa ninamaanisha kujitangaza rasmi kwa Waziriri Mkuu wa sasa Bwana Mheshimiwa Fredrick Sumaye, mbunge wa jimbo la Hanang kupitia chama cha CCM.&lt;br /&gt;Ukiangalia kwa juu utakubaliana na mimi kuwa kitendo alichokifanya raisi mtarajiwa huyu kimeonyesha kile kitu ambacho wengi wamekuwa wakisema amekosekana nacho, yaani ushujaa wa hali ya juu.&lt;br /&gt;Nasema ushujaa wa hali ya juu kwa sababu kufuatana na taratibu walizojiwekea waheshimiwa hawa katika chama cha CCM ni kuwa ni haramu kwa mtu mwenye nia ya kugombea uraisi kuanza kufanya kampeni za nafasi hiyo kabla ya tarehe maalum zilizopangwa na chama na kujitangaza rasmi ni moja ya njia za kampeni kama ilivyoelezewa na taratibu za kichama.&lt;br /&gt;Vilevile kwa muangalio mwingine mheshimiwa huyu ameweza kuonyesha ujasiri wa kuwa mkweli na uwazi wa kuelezea dhahiri kwa umma wa watanzania kuwa ni kweli anajiandaa kwa nguvu zote kunyakua kiti hiko tofauti na hisia za walio wengi kuwa amekosa sifa hizo za kuwa mkweli na muwazi katika matendo yake.&lt;br /&gt;Lakini ukiangalia kwa undani zaidi unaweza kugh’amua jinsi gani mheshimiwa huyu amejiingiza mtegoni kwa kuudhihirishia umma wa watanzania ambao wengi wanauona kama wa wadanganyika, mapungufu ambayo kwa lugha yake mheshimiwa huyu maadui zake wa kisiasa wanamzushia.&lt;br /&gt;Mojawapo ya mapungufu hayo ni upeo wake wa kuona na kushungulikia mambo kama mwanasiasa mkomavu na aliye na uwezo wa kuendesha siasa kiufundi. Na hili sio tu ni mapungufu kwake yeye binafsi lakini na vilevile kwa wale waliomzunguka kutokana na kitendo chao kumwachia akiingia mtegoni kirahisi kama alivyofanya.&lt;br /&gt;Nasema ni upungufu kwa kuzingatia maswala afuatayo. Moja ni muda wa kutoa tangazo hilo, pili njia alizotumia kutoa tangazo hilo na tatu sababu alizosema kuwa zinampelekea kugombea nafasi hiyo.&lt;br /&gt;Kuhusiana na muda wa kutoa tangazo hili muhimu, hili nimgependa kiliainisha katika viwango viwili vifuatavyo.&lt;br /&gt;Kwa wale ambao wanatambua umuhimu wa kufuatitilia hatima ya nchi yetu tukufu hasa kwa kuzingatia utamaduni wa kinyang’au unaojitandaza katika jamii yetu hasa kenye medani ya siasa, ni wazi wamekuwa wakifuatilia mawazo ya wachambuzi wenzangu wa kisiasa ambao wamekuwa kama anavyodai mheshimiwa huyu wakimfuatafuata na kumzushia majungu kila kukichwa. &lt;br /&gt;Lakini katika gazeti la RAI la tarehe…..mwandishi mmoja wa siku nyingi aliandika makala ambayo kwa mara ya kwanza imekuwa imemchambua kwa wazi kabisa mheshimiwa huyu. Mwandishi huyu bila ya woga ameeleza kwa wazi kabisa baadhi ya mapungufu aliyonayo mheshimiwa huyu kiasi cha kuwa hafai kabisa kugombea nafasi ya urais. Mimi nisingependa kuyarudia hayo kwa sasa lakini kitendo cha mheshimiwa huyu kuripuka kujibu mapigo katika wakati kama huu ambao aliyoyasema mwandishi Salva bado yapo kichwani na kwa kawaida yasemwayo mwanzo ndio yenye uwezekano wa kuganda vichwani mwa watu, mheshimiwa Sumaye amejikuta akimsidia kazi ya kummaliza aliyoianza mwandishi huyo. &lt;br /&gt;Hili linaonyesha jinsi gani mheshimiwa ambaye mwandishi Salva amemwita MNYAPARA ALIYECHOKA asivyo makini. Badala ya kusubiri a ditect mazingira yeye ameruhusu mazingira kumditact yeye, kwa kiingereza ni kuwa ameonyesha kuwa REACTIONARY na siyo PROACTIVE kama wanasayansi wa siasa tunavyoamini mwanasiasa bora awe.&lt;br /&gt;Vilevile muda unamtupa mkono mheshimiwa huyu kwa upande wa taratibu za kichama. Kujitangaza wazi kwa mheshimiwa huyu ni wazi kumemuweka katika mazingira mabaya kwa wapinzani wake ndani ya vyombo husika vya chama kama vile Sekretarieti kuu yenye jukumu la kutoa maksi kwa kila mgombea kumnyima points muhimu kwa kosa hilo la kiutaratibu. Hili vilevile linaonyesha upeo mdogo wa kufikiria.&lt;br /&gt;Nikija pungufu la pili ambalo ni njia aliyotumia mheshimiwa huyu kujitangaza rasmi kuwa atagombea urais wa nchi hii nasema ni upungufu kutokana na mambo mawili. Ningelikuwa ni mimi ninayegombea katika hali mbaya ya kisiasa kama mtanzania mwenzangu huyu kamwe nisingelichagua mwandishi mjanja kama Manyerere ambaye sio tu hawakuwa na mahusiano mazuri hapo kabla kutokana na habari alizokuwa akiripoti hapo zamani. lakini vilevile hata kama anaona kuwa karibu magezeti yote isipokuwa gazeti lake la WAZO LA WIKI na la vijana wake la HOJA, hayamwandiki vizuri lakini sio gazeti alilotokea mwandishi huyu. &lt;br /&gt;Hivi mtu kama waziri mkuu anashindwa kujua washika dau wa magazeti yetu na kujua ni yapi mawazo yao kuhusiana na yeye. Hata kama gazeti hili katika siku zake za hizi za mwanzo linajitahidi kuwa mstari wa mbele kwa kutoa habari bila ya kuegemea upande wowote lakini kamwe si vigumu kung’amua chachu ya waandishi na wamiliki wa maagazeti yetu katika suala zima la kutengeneza mawazo ya jamii. Mheshimiwa Sumaye alitakiwa kuonyesha umakini kidogo katika hili na sio kuingia mtegoni kirahisi hivyo. &lt;br /&gt;Upungufu wa tatu kwa upande wa mheshimiwa huyu unaonekana katika sababu alizosema kuwa zinampelekea kugombea nafasi hiyo. Kwa mujibu wa muandishi Manyerere, mheshiwa huyu ametoa sababu kuu tatu zinazomfanya yeye agombee Urais, nazo ni kuendeleza siasa za uwekezaji, kudumisha aliyoyaita mafanikio ya rais mkapa na nafasi yake katika serikali ya sasa. &lt;br /&gt;Ni wazi kuwa hizo ndizo sababu zake za dhati kabisa kugombea nafasi hiyo na hapo lazima apongezwe kwa kuwa mkweli na muwazi wa hali ya juu. Lakini kama mwanasiasa ni umakini gani alioutumia kujiuza kwa wapiga kura wake ndani na nje ya chama chake kwa kudiriki kusema hadharani kuwa hizo ndizo sababu zinazompelekea kugombea nafasi ya urais wa nchi hii. &lt;br /&gt;Nasema ni upungufu kwa sababu hata kama ndio ukweli hizi ndio sababu kuu zinazompelekea yeye kugombea nafasi za urais, mwanasiasa makini kamwe asingeropoka kama alivyofanya yeye. Hivi ina maana hajui jinsi gani wananchi wa chini walio wengi walivyo na hasira dhidi ya hawa jamaa tunaowaita wawekezaji. Hata kama wamewezesha baadhi ya vijana wa kitanzania wachache tena wengi kati yao wenye majina “mazuri” na waliopelekwa kusoma elimu bora ughaibuni kupata ajira “nzuri” na kuweza kuendesha vigari vya mikopo na kujifaragua Sheraton, aaah ni Royal Palm, opss nini tena???. Ukiangalia kwa undani vijana hawa wengi wao wamefika huko ama kwa kodi ya walalahoi wetu au kile kinachoitwa “scholarship” zinazotolewa na hao waitwao wawekezaji.&lt;br /&gt;Hivi hizo ndio siasa za kuwaingia watanzania walio wengi wanaolala bila ya uhakika wa mlo wa kesho kwa sababu mzungu amepewa kijiardhi chake alichokuwa anajipatia shibe ya kutosha yeye na familia yake? Hivi mheshimiwa Sumaye anafikiri akitoa wale “vijana wake” wachache pale Mererani ambao wengi wao ni watoto wa “nyumbani”, ni nani kati ya wengine watakompigia kura au hata kutaka kusikia jina lake linaelekea ikulu? Hivi huyu jamaa ni makini kweli au anataka kuuza majimbo ya chama chake kwa CHADEMA au CUF kwa bei ya che. Au labda mheshimiwa huyu ana mpango wa kutoitisha uchaguzi wa wabunge na madiwani kule Bulyanhulu na kwengineko kama anavyofanya jimboni kwake Hanang hadi hivi sasa.&lt;br /&gt;Kwa kweli kama ni ajenda za kuwaomba Urais watanzania, na hata wanachama wa CCM pekee, sera ya wawekezaji iliyojawa utapeli kama hii ya kwetu si mojawapo kwa mtu makini kuingilia nayo uwanjani. Kwani hii ni moja ya sera iliyo wazi au ashakum si matusi, iliyo uchi zaidi kushutumiwa na wapinzani wake kisiasa kiasi ya wananchi wakamuona mheshimiwa huyu hana jipya zaidi ya kuendeleza “kuiuza” nchi yetu kwa makaburu na wazungu.&lt;br /&gt;Kuhusiana na ajenda ya kuendeleza mazuri yaliyofanywa na rais mMkapa hapa nako kuna utata. Ingawa ni kweli kama atatokea mtu kubadilisha kila kilichopo hata kama kweli ni vingi ni vibaya, kuna hatari kubwa ya nchi hii kukumbwa na janga kubwa la umasikini mara mia kuliko hivi sasa, lakini ni wazi kuwa mheshimiwa huyu kama waziri mkuu anayesifika kwa kutoa maamuzi mengi ya kupingana na sera za uchumi za CCM, kamwe hawezi kuwa chaguo la wananchi. Hivi akitokea mtu akaelezea jinsi Rais Mkapa alivyomfanya mheshimiwa huyu kuwa ni waziri mkuu wa pekee Tanzania ambaye alinyang’anywa madaraka mengi kuliko yeyote katika historia ya Tanzania baada ya uhuru, ajenda hii kweli itafanya kazi? &lt;br /&gt;Au wakitokea wapinzani wake wa ndani ya CCM wakatoa mahesabu ya maamuzi mangapi makubwa ya maana yaliyotolewa na Rais wetu na mheshimiwa huyu akahusika atasemaje? &lt;br /&gt;Hili na lile la kuwa yeye ndiye msaidizi wa karibu wa Rais Mkapa kwa miaka tisa na miezi kadhaa sasa ni ajenda dhaifu mno na rahisi kuwapa watu umaarufu wa kisiasa bure bure. Kwani rekodi inaonyesha wazi kuwa mheshimiwa huyu amekuwa akivurunda tu na ndio maana wapo baadhi ya wachambuzi wa kisiasa wanaona udhaifu wake kama waziri mkuu ndicho kilichomhakikishia kiti chake kwa muda mrefu kwani Rais Mkapa kama anavyonekana hakupenda kuwa na mtu atakeyemfunika ki umaarufu. Anaposema hivi anataka kutuambia rais Mkapa amechoka kuiona CCM madarakani hadi kufikiria kumrithisha mheshimiwa huyu Urais wa nchi hii. Ina maana viongozi wenzie waandamizi katika serikali hii ya tatu ni wabovu na hawawezi kuaminiwa kuendeleza yale yanayoitwa mafanikio ya serikali ya Rais Mkapa.&lt;br /&gt;Vile vile hoja hizi mbili kwa kweli zinawahakikishia watanzania kuwa yanayosemwa na wale anaowaita maadui zake kisiasa kuwa mheshimiwa huyu anataka nafasi hii ya Urais si kuwa ana dira bora kwa nchi yetu bali kulinda mafanikio yake binafsi aliyoweza kujikusanyia kwa miaka hii michache aliyokuwa madarakani kama waziri wetu mkuu. Haya ni pamoja na nafasi ya uheshimiwa ndani na nje ya jamii yetu na bila kusahau mashamba kule mvomero, majumba na viwanja kila pande ya nchi na miradi mingine inayochipuka bila ya uoga ama kwa jina lake binafsi, mama watoto wake, watoto au wafanyibiahsara walio karibu naye.&lt;br /&gt;Kwa kweli pamoja na kuwaonea huruma viongozi wenzie wa CCM wanaoshiba kwa chama chao kuwa madarakani bila ya upinzani wa maana, namuonea huruma sana Mheshimiwa huyu. Ni wazi mheshimiwa huyu hata kama mapungufu yake yamekuwa sio ya kuficha, inaonekana timu yake inayomsaidia kwenda ikulu, ukitowa mapesa bwerere waliyonayo hakuna watu makini wa kupanga mchezo wa kisiasa ambao wangemshauri asikurupukie mtego aliowekewa kirahisi kama alivyofanya.&lt;br /&gt;Kama nilivyoelezea hapo juu, kazi yangu mimi sio kumchambua sana mheshimiwa huyu na nafasi yake kama mgombea urais wa nchi yetu katika uchaguzi ujao bali kuchambua udhaifu alio uonyesha katika kile alichokisema kukata ngebe za wapinzani wake kisiasa. Si vibaya nikawanong’oneza wasomaji kuwa kazi ya kumchambua yeye na wenzanke wengineo ambao wao ama kwa kuheshimu taratibu walizojiwekea ndani ya chama chao au kwa mahesabu yao ya kisiasa wameamua kuendelea kutamba gizani, itakuja kwenu hivi karibuni.&lt;br /&gt;Napenda kuwakilisha uchambuzi wangu kwa wakubwa zangu katika fani hii. Karibuni.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-892575776834868185?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/892575776834868185/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=892575776834868185' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/892575776834868185'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/892575776834868185'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2007/08/masikini-sumaye.html' title='Masikini Sumaye!'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-6952646892572371748</id><published>2007-06-10T21:09:00.000-07:00</published><updated>2007-07-06T08:34:54.168-07:00</updated><title type='text'>My life, my identity</title><content type='html'>I was born in November 1976 from an African family of eleven members, humble, pious and righteous parents and nine siblings, five sisters and brothers. My parents are originally from beautiful Comorian Islands who moved to the spices islands of Zanzibar in early 20th century, before shifting to the slopes of Uluguru Mountains in Morogoro region in Tanzania where I was born and raised. I was lucky to grow up in a humble family endowed with love and happiness where strict religious and worldly education was number one priority to everyone. From this lovingly and supportive mother and our nations' stable and progressive intellectual savy environment, envisioned and moulded by our national hero, Mwalimu Nyerere, i have always been inspired with the world of critical knowledge and understanding of world events. My inspiration is  politics, leadership and service to humankind.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-6952646892572371748?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/6952646892572371748/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=6952646892572371748' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/6952646892572371748'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/6952646892572371748'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2007/06/my-life-my-identity.html' title='My life, my identity'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-8591774889123719684.post-6732648103121562927</id><published>2007-06-10T20:53:00.000-07:00</published><updated>2007-08-02T11:02:18.335-07:00</updated><title type='text'>The Intellectual and visionary me..</title><content type='html'>With all the challenges my beloved continent is faced there is a natural beauty that keep my spirit high and kicking. Since my childhood I have come to believe that if perform my duty efficiently and effectively as I can, one day I will proudly be sitting in the shadow of African trees reminiscing my worthwhile life humbly serving my beloved continent. It is from this spirit that for years now I have dedicated my precious life in thinking, developing and working on many ideas, visions and projects that target on enhancing the beautiful talents of my fellow young inspired Africans from my home country Tanzania to the streets of New York. I truly believe with discipline and hardworking and that together we have a chance to realize the grand strategy of our founding elders based on united Africa for better Africa for all.&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/8591774889123719684-6732648103121562927?l=omarilyas.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://omarilyas.blogspot.com/feeds/6732648103121562927/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=8591774889123719684&amp;postID=6732648103121562927' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/6732648103121562927'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/8591774889123719684/posts/default/6732648103121562927'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://omarilyas.blogspot.com/2007/06/better-africa-for-all.html' title='The Intellectual and visionary me..'/><author><name>My life, my identity</name><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry></feed>
